Nikita Kering’ Atetea Wasanii wa Kenya Katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika, Ataka Malipo ya Haki na Ulinzi wa Haki Miliki

Nikita Kering’ Atetea Wasanii wa Kenya Katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika, Ataka Malipo ya Haki na Ulinzi wa Haki Miliki

Mwanamuziki wa Kenya, Nikita Kering’, ameonyesha ujasiri na kujitolea kwa maslahi ya wasanii Wakenya kwa kutoa wito kwa viongozi wa Afrika kuhakikisha wasanii wanalipwa kwa haki na kulindwa kisheria dhidi ya matumizi holela ya kazi zao. Akizungumza katika makao makuu ya Umoja wa Afrika (AU) huko Addis Ababa, Ethiopia, Nikita alitoa hoja kali kuhusu umuhimu wa kuwepo kwa sera thabiti za kulinda haki miliki na kuhakikisha wasanii wanapata fidia stahiki kwa kazi zao. Katika hotuba yake, Nikita alisisitiza kuwa licha ya mchango mkubwa wa wasanii katika uchumi na utamaduni wa bara Afrika, wengi wao wanaendelea kukumbwa na changamoto za wizi wa kazi, malipo duni, na ukosefu wa mifumo rasmi ya kuwalinda.  “Wasanii wetu sio tu wachangiaji wa burudani, bali pia ni wahifadhi wa historia, tamaduni, na utambulisho wa Kiafrika. Ni wakati sasa serikali na taasisi za bara hili ziwaheshimu kwa kuhakikisha haki zao zinalindwa,” alisema Nikita mbele ya wajumbe wa AU na viongozi wa sekta ya ubunifu kutoka nchi mbalimbali. Mbali na kutetea maslahi ya wasanii wa Kenya, Nikita alizungumzia haja ya ushirikiano wa bara zima katika kuweka viwango vya pamoja vya malipo, usimamizi wa mirabaha (royalties), na mikataba ya haki kwa wasanii. Ushiriki wa Nikita katika majukwaa ya kimataifa unaashiria hatua mpya kwa wasanii wa Afrika Mashariki kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya sera na uundaji wa mifumo bora kwa ajili ya sekta ya sanaa na burudani. Kwa sasa, Nikita anaendelea kuwa sauti ya mabadiliko, akionyesha kuwa muziki sio tu burudani  bali pia ni chombo cha mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.

Read More
 Nikita Kering afunguka kuhusu utambulisho wa muziki wa Kenya

Nikita Kering afunguka kuhusu utambulisho wa muziki wa Kenya

Mwanamuziki kutoka Kenya Nikita Kering amefuguka sababu za muziki wa Kenya kukosa utambulisho wake kwenye ramani ya dunia. Kupitia mitandao ya kijamii Nikita amesema Kenya ilitawaliwa zaidi na wakoloni kiasi cha kupoteza utambulisho wake kwenye nyanja mbali mbali. Mrembo huyo mshindi wa Afrimma amesema jambo hilo limewapa wadau wa muziki nchini kuzingumkutu kwenye suala la kubuni jina litakalotangaza muziki wa Kenya kimataifa. “If Kenyan music was to hit, we still don’t know what Kenyan music is. I think we were heavily colonized that our music identity didn’t even show. Our identity lacks in very many things,” Alisema.

Read More
 Nikita Kering ashindwa kuficha furaha yake kwa kutumbuiza kwenye Afrobeat Concerto ya BBC Radio 1Xtra.

Nikita Kering ashindwa kuficha furaha yake kwa kutumbuiza kwenye Afrobeat Concerto ya BBC Radio 1Xtra.

Msanii Nikita Kering ameshindwa kuficha furaha yake baada ya kutumbuiza katika shoo ya kituo cha habari BBC 1Xtra mwishoni mwa wiki pamoja na baadhi ya wasaniii makubwa ya tasnia ya muziki dunia. Kupitia ukurasa wake wa instagram amewashukuru mashabiki zak kwa upendo ambapo ameenda mbali Zaidi kuahidi ataendelea kuwapa muziki mzuri “A dream come true😭✨ @sofresh254 thank you for making this track with me🙏🏾I have so much to learn, can’t wait to see what Better looks like!,” Aliandika. Mafanikio yake makubwa na kutumbuiza kwenye jukwaa la kimataifa inakuja baada ya kutangazwa kama balozi wa programu ya EQUAL kwa mwezi wa Novemba na mtandao wa kusikiliza muziki  waSpotify. Mwanamuziki huyo aliyeshinda tuzo na mtunzi wa nyimbo wiki kadhaa zilizopita aliangaziwa kwenye bango la New York Times Square nchini Marekani kwa hisani ya Spotify na pia kabla ya yeye kutumbuiza kwenye sshoo ya Afrobeat Concerto Iliyotayarishwa na kituo cha BBC Radio 1Xtra.

Read More
 Nikita Kering aachia rasmi EP yake mpya

Nikita Kering aachia rasmi EP yake mpya

Mwanamuziki kutoka Kenya Nikita Kering ameachia rasmi EP yake mpya inayokwenda kwa jina la The Other Side. EP hiyo iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki ina jumla ya ngoma sita za moto ambazo amezifanya bila kumshirikisha msanii yeyote. The Other Side EP ina ngoma kama Save Me, Get Through, Fallling Down, Unrelatable, Love Outside, On Yah na inapatikana exclusive kwenye majukwaa yote a kupakua na kusikiliza muziki mitandaoni. Hii ni EP ya pili kwa mtu mzima Nikita Kering baada ya A Side of Me iliyotoka mwaka 2021 ikiwa na jumla ya mikwaju saba ya moto. Utakumbuka juzi kati Nikita Kering’ alisaini mkataba wa Ubalozi na mtandao wa kusikiliza muziki wa Spotify kupitia mpango wa muziki uitwao EQUAL. EQUAL ni mradi ambao unalenga kuleta usawa wa kijinsia kwenye muziki lakini pia kuwasaidia wasanii wa kike na watengeneza maudhui katika mitandao kijamii kutanua wigo wa kazi zao ili iwafikie watu wengi duniani.

Read More
 Nikita Kering alamba shavu la ubalozi Spotify

Nikita Kering alamba shavu la ubalozi Spotify

Mwimbaji wa RNB na Pop kutoka Kenya Nikita Kering’ anazidi kuchana mbuga kimataifa mara baada ya kusaini mkataba wa Ubalozi na mtandao wa kusikiliza muziki wa Spotify. Nikita ametangazwa kuwa balozi wa mpango wa muziki uitwao EQUAL ambao unaendeshwa na mtandao wa kustream muziki  wa spotify kwa mwezi wa Novemba. Mrembo huyo ambaye yupo mbioni kuachia EP yake mpya anajiunga na orodhaa ya wasanii wa kike kutoka Afrika ambao wamewahi kuwa mabalozi mpango huo hapo awali. Wanamuziki wengine wa kike kutoka nchini Kenya ambao hapo awali walitajwa kuwa mabalozi wa mpango wa EQUAL ni pamoja na Muthoni Drummer Queen na Sylvia Ssaru. Kupitia ukurasa wao wa Instagram, Spotify wamechapisha habari iliyosomeka “There’s nothing #Unrelatable about November’s #EQUALAfrica ambassador @nikita_kering  Listen to all the incredible voices of #EQUALAfrica at the link in bio.” EQUAL ni mradi ambao unalenga kuleta usawa wa kijinsia kwenye muziki lakini pia kuwasaidia wasanii wa kike na watengeneza maudhui katika mitandao kijamii kutanua wigo wa kazi zao ili iwafikie watu wengi duniani.

Read More