Nina Roz Akanusha Tetesi za Kutoka Kimapenzi na Ziza Bafana

Nina Roz Akanusha Tetesi za Kutoka Kimapenzi na Ziza Bafana

Msanii maarufu wa muziki wa Afrobeat, Nina Roz, amejitokeza wazi na kukanusha vikali uvumi unaosambaa mitandaoni kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na rapa Ziza Bafana. Katika mahojiano maalum na vyombo vya habari, Nina Roz alisema kuwa hana uhusiano wa kimapenzi na Bafana, akisisitiza kwamba wao ni marafiki wa kawaida tu na hakuna chochote kinachoendelea kati yao. “Sijawahi kuwa na uhusiano wowote wa kimapenzi na Ziza Bafana. Ni rafiki yangu wa kawaida tu, na tunaheshimiana kama wasanii,” alisema Nina Roz kwa msisitizo. Tetesi hizo zimekuwa zikienea mitandaoni, zikidai kuwa wawili hao wamekuwa wakionekana mara kwa mara pamoja, hali iliyoibua maswali miongoni mwa mashabiki. Hata hivyo, Nina ameweka wazi kuwa kukutana kwao kunatokana na ushirikiano wa kazi na si mapenzi. Msanii huyo pia alitumia fursa hiyo kuwakumbusha mashabiki wake kuhusu uhusiano wake wa awali na msanii mwenzake Daddy Andre, ambaye kwa sasa hawako pamoja. Nina alifafanua kuwa tangu alipoachana na Daddy Andre, hajahusika tena na uhusiano wa kimapenzi wa hadharani.  “Sijui lolote kuhusu hizo taarifa za mimi kutoka na Ziza Bafana. Sina muda wa kupoteza kwenye tetesi za mitandaoni,” aliongeza. Kwa sasa, Nina Roz anasema ameweka mkazo kwenye kazi yake ya muziki, akiandaa miradi mipya itakayozinduliwa hivi karibuni.

Read More
 Nina Roz Afichua Sababu za Kujiondoa UNMF, Amsuta Vikali Eddy Kenzo kwa Kuwa Mbinafsi

Nina Roz Afichua Sababu za Kujiondoa UNMF, Amsuta Vikali Eddy Kenzo kwa Kuwa Mbinafsi

Mwanamuziki maarufu na mwanasiasa chipukizi, Nina Roz, ameibua mjadala mpya katika tasnia ya muziki nchini Uganda baada ya kufichua sababu zilizomfanya kujiondoa kwenye Shirikisho la Kitaifa la Wanamuziki nchini humo (UNMF) Katika mahojiano aliyofanya hivi karibuni na vyombo vya habari, Nina Roz alieleza kuwa walibuni shirikisho hilo pamoja na  Eddy Kenzo kwa madhumuni ya kuwatetea wasanii, kusimamia haki zao, na kuendeleza ustawi wa sekta ya muziki nchini Uganda. Hata hivyo, alidai kuwa hali hiyo ilianza kubadilika muda mfupi baada ya kuanzishwa kwa shirikisho hilo mwaka 2023.  “Nilidhani tunaunda jukwaa la kweli la kuwaunganisha wasanii na kuwatetea, lakini baadaye nikabaini kuwa viongozi, hususan Eddy Kenzo, walikuwa na maslahi binafsi pamoja na ajenda za kisiasa ambazo hazikuwiana na malengo ya awali,” alisema Nina Roz. Nina, ambaye aliwahi kushika wadhifa wa kusimamia masuala ya maadili ndani ya UNMF, alieleza kuwa shirikisho hilo lilianza kupoteza dira na kuonyesha ukaribu usiofaa na serikali. Kwa maoni yake, hali hiyo ilikuwa kinyume na misingi ya uhuru wa kujieleza na uhuru wa kisanii. Tangu kujiondoa kwake, Nina Roz amekuwa mkosoaji wa wazi wa shirikisho hilo, akilituhumu kwa kile alichokitaja kuwa ni siasa za upendeleo katika tasnia ya muziki. Anadai kuwa wasanii wanaoonekana kukosoa serikali wamekuwa wakibaguliwa katika upatikanaji wa fursa, mikataba, na msaada kutoka kwa taasisi hiyo. “UNMF haikuwakilisha tena maslahi ya wasanii wote. Iligeuka kuwa jukwaa la upande mmoja, ambapo wale waliokuwa karibu na serikali ndio walipewa kipaumbele,” aliongeza. Kwa sasa, Nina Roz anajiunga na orodha ya wasanii wakubwa kama King Saha, Ziza Bafana, na Spice Diana, ambao wote wamejitenga na UNMF, wakieleza kutoridhishwa  na namna taasisi hiyo inaendeshwa.

Read More
 Pallaso Aweka Wazi Msimamo Wake Kuhusu Siasa

Pallaso Aweka Wazi Msimamo Wake Kuhusu Siasa

Msanii maarufu wa muziki nchini Uganda, Pius Mayanja almaarufu Pallaso, amesema kwa sasa hana mpango wa kujiingiza kwenye masuala ya siasa, akisisitiza kuwa bado anajikita kikamilifu katika taaluma yake ya muziki. Akizungumza katika mahojiano ya hivi karibuni, Pallaso alieleza kuwa hajatimiza malengo aliyojiwekea katika muziki, na hivyo anataka kuyakamilisha kabla ya kufikiria kuchukua jukumu lolote jipya katika maisha yake ya kitaaluma.  “Sihitaji kuingia kwenye siasa kwa sasa. Niko katika harakati za kutimiza ndoto yangu ya muziki, na nataka kuikamilisha kikamilifu kabla ya kufikiria jambo lolote jingine.” Ingawa hajajitosa rasmi katika siasa, Pallaso alisema anaendelea kutumia muziki wake kama chombo cha kuwasilisha ujumbe wa kijamii na kisiasa. Anaamini kuwa muziki ni jukwaa lenye nguvu kubwa la kufikisha ujumbe, na ndilo eneo analolielewa vyema. “Siasa ni wito. Binafsi bado sijaupata. Nikihisi moyoni kwamba ni wakati wa kuingia katika siasa, nitafanya hivyo. Lakini kwa sasa, ninaendelea kuwasilisha ujumbe wangu kupitia muziki.” Kauli ya Pallaso inajiri wakati ambapo baadhi ya wasanii nchini Uganda wameanza kujitosa katika siasa, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi. Miongoni mwao ni Big Eye na Nina Roz, ambao tayari wametangaza nia ya kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa. Ingawa Pallaso hana pingamizi kwa wasanii kuingia katika siasa, amesema ataingia katika ulingo huo pale tu atakapohisi kwa dhati kuwa ni wito wake wa kweli kulitumikia taifa. Kwa sasa, anabaki kuwa mmoja wa wasanii wanaotumia kazi zao kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Read More
 NINA ROZ AAHIDI KUMSAIDIA WEASEL KUONDOKANA NA URAIBU WA DAWA ZA KULEVYA

NINA ROZ AAHIDI KUMSAIDIA WEASEL KUONDOKANA NA URAIBU WA DAWA ZA KULEVYA

Msanii kutoka Uganda Nina Roz amehapa kumsaidia msanii mwenzake Weasel Manizo kuondokana na uraibu wa dawa za kulevya. Katika mahojiano yake Roz amesema ana uhusiano mzuri na msanii huyo hivyo ana mpango wa kuanza mazungumzo naye ili aweze kuacha kabisa kutumia dawa za kulevya na arudi tena kujishughulisha na masuala ya muziki. Mrembo huyo amedai vitendo vya Weasel kumnyanyasa kijinsia baby mama wake Sandra inatokana na msanii huyo kutumia mihadarati kupindukia. Utakumbuka Nina Roz alikuwa muathiriwa wa dawa za kulevya lakini baada ya kupelekewa kwenye kituo cha kurekebisha tabia ya waraibu wa mihadarati aliweza kuacha kutumia dawa hizo na kuamua kuokoka hivyo amekuwa akitumia muda wake mwingi kanisani akihubiri injili.

Read More
 NINA ROZ AFUNGUKA KUHUSU UTATA UNAOZINGIRA NYIMBO ZAKE

NINA ROZ AFUNGUKA KUHUSU UTATA UNAOZINGIRA NYIMBO ZAKE

Msanii kike kutoka nchini Uganda Nina Roz amethibitisha kwamba ana hakimiliki za nyimbo ambazo alifanya na prodyuza Daddy Andre kabla hajavunja mkataba wake. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Nina Roz amesema hana deni la mtu kwenye shughuli zake za muziki, hivyo ataendelea kutumbuiza nyimbo zake kwenye shoo zake. Nyimbo ambazo Daddy Andre na Nina Roz wanagombania ni pamoja na Nagana, Billboard Kipande, Andele, na Enyonta zote zikiwa zimetayarishwa na Daddy Andre chini ya lebo ya muziki ya Blackmarker Records. Wiki iliyopita Daddy Andre alitishia kumfungulia kesi  Nina Roz kwa madai ya kuvunja mkataba wake bila kufuata sheria stahiki. Kupitia barua ya kampuni ya mawakili ya  GM Kibirige and Co. Advocates, prodyuza Daddy Andre alidai kwamba Novemba mwaka wa 2021 Nina Roz alisitisha mkataba wake wa miaka 5 ambao alitia sahihi Juni 8 mwaka wa 2020. Nina Roz hata hivyo alitakiwa amlipe Daddy Dndre shillingi millioni 120 kwa hasara aliyomsababisha na pia asitumie nyimbo alizofanya Daddy Andre kwenye shoo zake la sivyo atamtupa jela.

Read More