NINCE HENRY AFUNGUKA KUHUSU UHUSIANO WAKE NA MENEJA CHAGGA

NINCE HENRY AFUNGUKA KUHUSU UHUSIANO WAKE NA MENEJA CHAGGA

Msanii Nince Henry kutoka Uganda amekanusha kuingia kwenye ugomvi na meneja wake wa zamani Chagga. Hii ni baada ya madai kusambaa mtandaoni kuwa wawili hao hawana maelewano mazuri kutokana na ugomvi wa pesa. Katika mahojiano yake hivi karibuni Nince Henry amesema madai hayo hayana ukweli wowote kwa sababu bado anafanya kazi na Chagga. Chagga ambaye alimtambulisha nince henry kwenye muziki anajianda kuachia album yake ya kwanza baada ya kufanya kazi ya kuwasimamia wasanii kwa miaka mingi.

Read More
 NINCE HENRY AWAJIA JUU WASANII WA MAKINDYE UGANDA KWA MADAI YA USHIRIKINA

NINCE HENRY AWAJIA JUU WASANII WA MAKINDYE UGANDA KWA MADAI YA USHIRIKINA

Msanii Nince Henry amewatolea uvivu wasanii wote wanaoishi Makindye nchini Uganda kwa tuhuma za kuwadhamini sana waganga wa kienyeji. Kupitia mitandao yake ya kijamii Nince Henry amesema wasanii wanaoshi eneo hilo wanafanya vitendo vya ushirikina kama njia moja ya kusafisha nyota yao kwenye shughuli zao za muziki. Nince henry ametoa changamoto kwa wasanii wenzake kutoishi makindye kutokana na kuongezeka kwa visa vya ushirikana miongoni mwa wasanii ambapo ameenda mbali zaidi na kumtaka msanii Spice Diana ahamie maeneo salama kama Ntide. Utakumbuka Makindye ni eneo ambalo kuna makaazi ya wanamuziki wengi maarufu nchini uganda ambao wanafanya vizuri kimuziki Afrika Mashariki lakini pia ni sehemu ambayo kuna maeneo mengi ya burudani.

Read More
 NINCE HENRY AMCHANA GRAVITTY OMUTUJJU KISA KUJIGAMBA KUWA AMEINGIZA PESA NYINGI KUMLIKO MSANII YEYOTE UGANDA

NINCE HENRY AMCHANA GRAVITTY OMUTUJJU KISA KUJIGAMBA KUWA AMEINGIZA PESA NYINGI KUMLIKO MSANII YEYOTE UGANDA

Msanii na mwandishi wa nyimbo kutoka nchini Uganda Nince Henry amemtolea uvivu rapa Gravitty Omutujju mara baada ya rapa huyo kujinasibu kuwa yeye ni moja kati ya wasanii waliopata shows nyingi baada ya uchumi wa nchi ya uganda kufunguliwa. Katika mahojiano yake na Galaxy FM Nince Henry amesema ameshangazwa na kitendo cha omuttujju kujigamba mitandaoni ambapo amesema  hakutarijia msanii huyo anaweza fanya jambo kama hilo ikizingatiwa kuwa umri wake hamruhusu kujihususha na mambo ya kijinga. Hitmaker huyo wa “Cinderella” amehoji kuwa baadhi ya wasanii wamepata shows nyingi kutokana na tasnia ya muziki nchini Uganda kufungwa kwa miaka miwili kufuatia janga la Corona, hivyo haoni kitu cha maana ambacho Gravitty Omutujju anajigamba nayo. Utakumbuka wiki iliyopita rapa Gravitty Omutujju alitangaza kuwa ameingiza pesa nyingi kutokana na shows ambazo amezipata licha ya watu kuubeza muziki wake ambapo alienda mbali na kusema kuwa haoni wasanii wanaodai muziki wao ni mzuri wakipata shows. Jambo hilo lilizua mjadala mzito kwenye mitandao ya kijamii huku kila mtu akitoa maoni tofauti juu ya suala hilo.

Read More