Meneja wa Otile Brown awapa mapromota utaratibu mpya wa kumpata msanii wake

Meneja wa Otile Brown awapa mapromota utaratibu mpya wa kumpata msanii wake

Meneja wa Otile Brown, Noriega amewapa utaratibu mpya mapromota wa kimataifa watakaompatia msanii wake shows. Kupitia instastory Noriega amewataka wahakikishe kuwa wanamtumia Otile Brown na timu yake ndege binafsi. Aidha amesema nyakati za Otile brown kugharamikia nauli ya ndege kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya shows zimepita na wakati huku akisema kuwa ni lazima ndege binafsi itajumuishwa kwenye mkataba kati ya uongozi wa Otile na mapromota wa kigeni. ” This before … Sahizi ni Private Jet kwa contract,” Ujumbe wa Noriega unasomeka instastory. Kauli ya Noriega imekuja mara baada ya promota aliyempa mwaliko msanii otile brown nchini marekani kugharamia usafiri wa msaniii huyo kupitia ndege binafsi ya daraja la juu.

Read More
 MENEJA WA OTILE BROWN AFUNGUKA JUU YA KUFUTWA KWA NYIMBO ZA STAA HUYO YOUTUBE

MENEJA WA OTILE BROWN AFUNGUKA JUU YA KUFUTWA KWA NYIMBO ZA STAA HUYO YOUTUBE

Meneja wa otile brown Noriega amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kufutwa kwa nyimbo za msanii huyo kwenye mtandao wa youtube. Akiwa kwenye moja ya interview meneja huyo amesema kama uongozi wa otile brown wameshangazwa na hatua ya nyimbo za staa huyo kufutwa kwenye mtandao wa youtube na aliyezi-upload ambapo ameahidi kulifuatilia jambo hilo kwa ukaribu ili kuhakikisha waliohusika wanakabiliwa kwa mujibu wa sheria. Hata hivyo Noriega amepuzilia mbali madai yanayotembea mitandaoni kuwa otile brown anatumia suala la nyimbo zake kufutwa kwenye mtandao wa youtube kuupromote kazi yake mpya kwa kusema kwamba suala hilo sio kiki kama inavyodaiwa kwani otile brown huwa hatumii kiki kutangaza muziki wake. Nyimbo ambazo zilifutwa kwenye channel ya youtube ya msanii huyo ni pamoja na Dusuma, Such Kinda of love, Chaguo la moyo wangu, Aiyana na nyingine nyingi.

Read More