Noti Flow Awatuhumu Maandy na Ssaru kwa Kuiga Ubunifu Wake

Noti Flow Awatuhumu Maandy na Ssaru kwa Kuiga Ubunifu Wake

Rapa wa Kenya, Noti Flow, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kuwatupia lawama wasanii wenzake Maandy na Ssaru, akiwatuhumu kwa kuiga ubunifu wake kwenye muziki. Sakata hilo limeanza siku chache tu baada ya Noti kuachia wimbo wake mpya aliofanya na mpenzi wak, Colonel Mustafa, ambao uli-sample melody kutoka kwenye hit single ya kundi The Vultures, kundi ambalo mpenzi wake huyo alianzisha miaka ya nyuma. Hata hivyo, kufuatia ujio wa kazi hiyo, Maandy na Ssaru pia waliibuka na wimbo wao mpya unaoitwa Zetu Zetu, ambao umesample kibao maarufu Monalisa cha kundi hilo. Hatua hiyo imeonekana kumkera Noti Flow, ambaye amedai kwamba wawili hao wanajaribu kuendeleza mtindo aliouanzisha yeye mwenyewe. Kupitia mitandao ya kijamii, Noti Flow hakusita kueleza hasira zake kwa maneno makali, akiwaita Maandy na Ssaru “copycats” kwa kile alichokitafsiri kama kuiga moja kwa moja mbinu na ubunifu wake.

Read More
 Colonel Mustafa Adai Kuwasaidia Huddah na Noti Flow Kufikia Umaarufu

Colonel Mustafa Adai Kuwasaidia Huddah na Noti Flow Kufikia Umaarufu

Msanii mkongwe wa muziki nchini Kenya,Colonel Mustafa, amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa muda aliowahi kutumia na mastaa wa kike kama Huddah Monroe na Noti Flow uliwasaidia kupenya kwenye anga la umaarufu, wakati walipokuwa bado hawajatambulika sana katika tasnia ya burudani. Akizungumza kwenye podcast ya Alex Mwakideu Live, alisema kwamba mahusiano yake na wanawake hao yalimsaidia kuwapa mwanga wa mafanikio waliokuwa bado hawajaufikia kwa wakati huo. Kwa mujibu wa msanii huyo, jina lake lilihusishwa na mastaa hao kabla ya wao kung’aa, na hivyo mchango wake haupaswi kupuuzwa. Kauli hiyo imeibua hisia mseto mitandaoni. Wapo wanaoamini kuwa Mustafa alikuwa sehemu ya safari ya mafanikio ya Huddah na Noti Flow, huku wengine wakimtuhumu kwa kujitafutia kiki na kutumia majina ya watu maarufu kurudi kwenye ramani ya burudani. Hadi sasa, Huddah Monroe na Noti Flow hawajajibu madai hayo, lakini mashabiki wanazidi kufuatilia kwa makini endapo wahusika watajitokeza kuweka wazi upande wao wa simulizi hii. Mustafa, anayekumbukwa kwa kazi zake akiwa na kundi la Deux Vultures, anaonekana kurejea tena kwenye vyombo vya habari si kwa muziki, bali kwa matamshi yenye utata kuhusu mahusiano ya zamani.

Read More
 Noti Flow afunguka kuhusu afya ya mpenzi wake King Alami

Noti Flow afunguka kuhusu afya ya mpenzi wake King Alami

Rapa Noti Flow ameweka wazi namna mpenzi wake King Alami anaendelea hospitali mara baada ya kupata majeraha mabaya alipojirusha kutoka kwa jumba la ghorofa 7. Kupitia instastory yake amesema mrembo huyo anaendelea kupata nafuu na huenda madaktari wakamruhusu kurudi nyumbani hivi karibuni. Lakini pia amewataka mashabiki kumpa nafasi King Alami pindi atakaporejea kwenye mitandao ya kijamiii. Ikumbukwe kisa cha Kinga Alami kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa saba kisa kukataliwa na Noti Flow lilimpelekea kupoteza mkono wake wa kulia huku goti lake la mguu wa kulia likivunjika.

Read More
 Noti Flow ajutia kuvunja uhusiano wake na King Alami

Noti Flow ajutia kuvunja uhusiano wake na King Alami

Mwanamuziki mwenye utata nchini Noti Flow amekiri kuumia na kujutia kitendo cha kuvunja mahusiano yake na aliyekuwa mpenzi wake, King Alami. Kupitia ukurasa wake wa instagram Noti flow amesema mahusiano yao hayangevunjika huenda tukio la king alami kutaka kujiua kwa  kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa tano alingefanyika. Aidha amefichua kuwa watu wengi mitandaoni wanamlaumu kuwa yeye ndio chanzo cha kisa hicho kutokea huku akisema kuwa jumbe hizo zimemfanya ajihisi vibaya zaidi kwa hatua ya kumkimbia mrembo huyo ambaye walikuwa wanashiriki pamoja mapenzi ya jinsia moja. “We gon pray for you my baby We’ve been praying for you day & night . You’re strong my G & you’re still the coolest stud I fell in love with I love you more everyday Nothing’s changed & I’m with you thru it all.. I’m here for you forever my love. Quick recovery my baby you are loved and cherished ( for those who are blaming me thank you very much for making me feel worse & guilty than I already I’m. Y’all are right tho, it’s my fault cz if I was with her she’d be OK & safe like she’s always been so crucify me”. Ameandika Kauli yake imekuja siku moja baada ya kuwaomba wafuasi wake wamsaidie kuchangisha pesa za kugharamia matibabu ya aliyekuwa mpenzi wake, King Alami ambaye kwa sasa bado amelazwa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta.

Read More
 Noti Flow aomba mchango wa kugharamia matibabu ya ex wake King Alami

Noti Flow aomba mchango wa kugharamia matibabu ya ex wake King Alami

Rapa Noti Flow ametoa wito kwa mashabiki na wahisani kuchangisha fedha za kugharamia matibabu ya mpenzi wake wa zamani King Alami. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amechapisha bango ambalo limetoa taarifa zote ya jinsi mashabiki wanaweza fanikisha mchakato mzima wa kutoa mchango wao kwa mrembo huyo ambaye anadaiwa alijirusha kutoka kwa jumba la ghorofa 5 mwishoni mwa juma lililipota. Kuhusu hali ya King Alami ambaye amelazwa katika hospitali moja jijini Nairobi, Noti flow amedai kuwa kwa sasa hana ufahamu wa nini hasa kilimtokea Alami ila amewaachia maafisa usalama kufanya uchunguzi. Hata hivyo amewataka wanablogu kukoma kueneza propanganda mitandaoni kuhusu King Alami na badala yake wameweke kwa maombi wakati huu mgumu.

Read More
 Noti Flow awataka mashabiki kumuombea Ex wake King Alami baada ya kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa tano

Noti Flow awataka mashabiki kumuombea Ex wake King Alami baada ya kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa tano

Rapa Noti Flow ametoa wito kwa mashabiki zake kumuweka kwa maombi mpenzi wake wa zamani King Alami baada ya kudaiwa kuwa alijiangusha kutoka kwa jumba la ghorofa tano katika barabara ya Lumumba drive jijini nairobi. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Noti Flow ambaye hajathibitisha madai hayo, amewataka walimwengu kuacha kueneza taarifa za uongo mtandaoni na badala yake wamuombee Alami na familia yake kwani kwa sasa wanapitia kipindi kigumu. Taarifa za King Alami kujiangusha kutoka kwa ghorofa zilitoka jana mara baada ya mtumiaji mmoja wa mitandao wa kijamii kuifahamisha mtandao wa udaku wa Nairobi Gossip kuwa mrembo huyo amekimbizwa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta ambako anauguza majeraha mabaya. ” I understand there’s a lot of rumors going around the blog about my X gal. Kindly stop spreading unconfirmed info. The family is kindly requesting for privacy and prayers as we go through this tough time. My heart isbroken & I’m devastated but I’m staying positive and prayerful. Kindly do the same She needs it. I still hope its a dream,” Aliandika Instagram. Hata hivyo hajajulikana ni kitu gani hasa kilimpelekea King Alami kujirusha kutoka kwa jumba la ghorofa tano ila ni jambo la kusubiriwa. Utakumbuka juzi kati King Alami alijitokeza kwenye mitandao ya kijamii na kumuomba msamaha Noti Flow waweze kurudiana kwani amelikosa penzi lake baada ya mahusiano yao kuvunjika miezi 6 iliyopita kwa madai ya usaliti.

Read More
 Kng Alami akiri kutamani penzi la mpenzi wake wa zamani Noti Flow

Kng Alami akiri kutamani penzi la mpenzi wake wa zamani Noti Flow

Mrembo King Alami amekiri kulitamani penzi la mpenzi wake wa zamani msanii Noti Flow ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu jini mkata kamba alipoingilia mahusiano yao na kuwatenganisha. Kupitia video aliyochapisha kwenye ukarasa wake wa Instagram amesikika akijutia kuliacha penzi la Noti Flow kwa kusema kwamba tangu mahusiano yao yalipovunjika hajawahi pata furaha maishani kutokana na majuto ya vitendo vya usaliti alivyokuwa akishiriki kwa siri. Hata hivyo amemuomba radhi Noti Flow pamoja na mashabiki zake kwa hatua ya kwenda kinyume na kiapo cha mahusiano yao huku akimsihi ampe nafasi nyingine ya kumpenda kwani hatokuja kumuacha asilani. Utakumbuka King Alami na Noti Flow ambao wamekuwa gumzo nchini kwa kushiriki mapenzi ya jinsia moja, walikuwa kwenye mahusiano kwa muda wa miezi 6 kabla ya penzi lao kuingiwa na ukungu kwa madai ya usaliti. Kipindi wawili hao wapo pamoja kama wapenzi walionyeshana upendo kiasi cha kila mmoja kuchora michoro ya tatoo kwenye miili yao lakini pia kuzawadiana vitu vya thamani ikiwemo gari kama njia ya kulifanya penzi lao libaki imara.

Read More
 NOTI FLOW AKIRI KUTESWA NA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KULA

NOTI FLOW AKIRI KUTESWA NA TATIZO LA KUKOSA HAMU YA KULA

Rapa wa kike nchini Noti flow amefunguka kuhusu tatizo la kiafya ambalo limekuwa likimsumbua kwa muda sasa. Kupitia mfululizo wa instastory yake kwenye mtandao wa Instagram mrembo huyo amekiri kuwa amekuwa akipata shida sana kwenye suala la kula chakula, jambo ambalo limemuathiri kiafya kiasi cha kupungua kimwili. Noti Flow amesema licha ya kupata maelekezo kutoka kwa daktari ya namna ya kukabilia na tatizo hilo, alishindwa kufuata taratibu alizopewa na mhudumu wake wa afya kutokana na yeye kukosa hamu ya kula. Hata hivyo ameahidi kufanya kila awezalo kuhakikisha anashirikiana kwa ukaribu na daktari kwa ajili ya kuuweka mwili wake sawa.

Read More
 NOTI FLOW AMTAMBULISHA MPENZI WAKE MPYA

NOTI FLOW AMTAMBULISHA MPENZI WAKE MPYA

Mwanamuziki aliyegeukia mapenzi ya jinsia moja nchini Kenya Noti Flow amemtambulisha mpenzi wake mpya siku chache baada ya kutangaza kuwa yupo single. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram mrembo huyo ameposti video akiwa anajiachia kimahaba na mchumba wake huyo huku akisindikiza na ujumbe unaosomeka “Too hot to stay single. kuingia soko na kutoka” Huyo anakuwa mpenzi wake wanne ndani ya mwaka huu baada ya jaribio lake la kuingia kwenye mahusiano mengine tofauti kukatishwa na jini mkata kamba. Hata hivyo walimwengu mitandaoni wameonekana kushangazwa na mienendo ya Noti Flow kukwamilia kwenye mahusiano ya jinsia moja wakati wanaume wapo wengi ambapo wameenda mbali zaidi na kuhoji kuwa huenda mrembo huyo ameshindwa na muziki ndio maana amegeukia mtindo huo wa maisha ambao labda unamuingizia pesa nyingi. Utakumbuka Noti Flow kwenye moja ya mahojiano yake aliwahi kunukuliwa akisema kwamba hatokuja kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na mwanaume yeyote hadi mwisho wa dunia kwani alipitia kipindi kigumu akiwa na mpenzi wake wa zamani ambaye alimdhulumu kijinsia.

Read More
 COLONEL MUSTAFA AMVUA NGUO EX WAKE NOTI FLOW, AMWITA MWIZI

COLONEL MUSTAFA AMVUA NGUO EX WAKE NOTI FLOW, AMWITA MWIZI

Msanii mwenye utata nchini  Colonel Mustafa kwa mara nyingine amedai kuwa aliyekuwa mpenzi wake Noti Flow alimuibia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram. Hitmaker huyo wa ngoma ya ‘Hey Baby’ amedai noti flow alichukua akaunti yake ya Instagram kwa njia ya mabavu kipindi wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi. Akizungumza kwenye the Trend ya NTV  Mustafa amefichua kuwa masaibu yake yalianza wakati alitumia simu ya Noti Flow kuingia kwenye mitandao ya kijamii kwa sababu alikuwa amepoteza simu yake. Kulingana Mustafa Noti Flow alichukua maamuzi ya kubadilisha kila kitu kwenye ukurasa wake wa instagram bila ridhaa yake na akaanza kuchapisha vitu vyake binafsi jambo lilompelekea kufungua akaunti nyingine. “She stole my Instagram account. Nililog in kwa simu yake, at that time I had lost my phone for  like 2 to 3 weeks, so she wanted to post something aka change email address and everything so akaanza kupost vitu zengine zenye hazinihusu so nikaona hapa tu nikuchorea,” Amesema. “She did not return the account, she took it, she changed it to her fan page so I had to find another one.” Ameongeza Mustafa amesema kitendo cha kuachana na noti flow iliathiri maisha yake kiasi cha kuwafanya wasanii aliokuwa anafanya nao muziki kumpita kisanaa. “I was not in peace…yaani ilifika point nikaona inanirudisha nyuma instead ya kuenda mbele…ata watu nilikuwa nao niliona wananipita,” amesema Mustafa. Hata hivyo ameongeza kuwa yeye na noti flow sio marafiki kwa sasa na hajazungumza nae kwa muda mrefu.  

Read More
 BENZEMA AFUNGUKA KUHUSU UTATA UNAOZINGIRA WIMBO WA FOTO MOTO

BENZEMA AFUNGUKA KUHUSU UTATA UNAOZINGIRA WIMBO WA FOTO MOTO

Msanii wa kundi la Ochungulo Family Benzema amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya Noti Flow kudai kuwa hajawahi faidi na mirabaha ya wimbo wao wa “Foto Moto. Katika mahojiano na Mungai Eve, Benzema amesema kipindi walimaliza kurekodi wimbo huo Noti Flow alimuambia kwamba ana haja na wimbo wa Foto Moto kwa kuwa muziki wa Kenya haulipi, jambo lilimfanya achukue wimbo huo na kuuweka kwenye mitandao ya kupakua na kusikiliza muziki. Benzema amesema kwa sasa anaendelea kuingiza kipato kupitia mirabaha ya wimbo wa Foto Moto,  hivyo Noti Flow ndio wakulaumiwa kwa kuwa alikata tamaa mapema juu ya wimbo huo. Utakumbuka wimbo wa Foto Moto wake Noti Flow akiwa amemshirikisha Benzema ilitoka mwaka wa 2020 na video yake kwenye mtandao wa youtube ina zaidi ya views millioni 4.5.

Read More
 PENZI LA NOTI FLOW NA MCHUMBA WAKE KING ALAMI LAINGIWA NA UKUNGU

PENZI LA NOTI FLOW NA MCHUMBA WAKE KING ALAMI LAINGIWA NA UKUNGU

Rapa kike nchini noti flow amesikitishwa na kitendo cha mpenzi wake king alami kushiriki kwenye biashara ya ngono mtandaoni licha ya kumhakikisha kuwa atafuta akaunti yake aliyofungua kwenye tovuti moja. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa instagram noti flow amesema ameumizwa na hatua ya mpenzi wake huyo kufuta akaunti aliyokuwa anaijua na kisha akafungua akaunti nyingine kwenye mtandao mmmoja wa biashara ya ngono bila ufahamu wake. Noti Flow ameenda mbali zaidi na kusema kwamba Alami amechapisha picha zake walizozipiga kipindi cha uchumba wao kwenye ukurasa wake mpya wa tovuti ya biashara ya ukahaba aliyofungua majuzi. Kulingana na Noti Flow, tabia hiyo imemfanya aamue kutomsamehe Alami, licha ya kutaka kumsamehe kutoka kitendo chake cha nyuma cha kutoka kimapenzi na mwanaume mmoja tajiri. “Woow… Nilikuwa nikifikiria kukusamehe lakini sasa… Karibu Kanairo ambapo unampelekampenzi wako kwenye mtoko na kumpiga picha ili yeye tu azitumie picha hizo kwenye tovuti ya ukahaba,” Noti Flow aliandika kwenye Instagram yake. Hata hivyo, imekuja siku chache baada ya Alami kumuandikia noti flow ujumbe mzito wa mapenzi kupitia ukurasa wake wa Instagram akisindikiza na jina la Noti Flow. “Kuna wakati utaniudhi na kunisababishia hasira zisizohitajika, lakini hata iweje, nitakupenda daima. Kuna maneno ya kikatili unaweza kusema ambayo yataniumiza na kuniletea huzuni…Katika maisha, kuna mapambano, mabishano na changamoto ambazo tutalazimika kuvumilia lakini haijalishi nini kitatokea… Ninaweza kuwa nalia sasa lakini niko sawa,” Ujumbe wa Alami ulioandikwa kwa mkono umesomeka

Read More