Toxic Lyrikali Apata Baraka za Nyashinski Baada ya Mafanikio ya ‘Cartman’ YouTube

Toxic Lyrikali Apata Baraka za Nyashinski Baada ya Mafanikio ya ‘Cartman’ YouTube

Msanii nyota wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Nyashinski, ameonyesha wazi kuunga mkono na kubariki kazi ya rapper chipukizi Toxic Lyrikali kupitia wimbo wake mpya uitwao “Cartman”. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Nyashinski alielezea kuvutiwa na ubunifu wa wimbo huo, akithibitisha kuwa anatambua na kuthamini kipaji cha msanii huyo anayeinukia. Kwa kutumia ushawishi wake mkubwa katika tasnia ya muziki, Nyashinski aliipa kazi ya Toxic Lyrikali msukumo wa kipekee, hatua ambayo imeibua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa hip hop. Kutoka kwa mashairi hadi uwasilishaji, wimbo huo umesifiwa kwa ubora wake na kuonekana kama hatua muhimu kwa msanii huyo chipukizi. Baraka kutoka kwa Nyashinski, ambaye anatambulika kama mmoja wa magwiji wa muziki wa Kenya, imechukuliwa na mashabiki na wadau wa muziki kama ishara ya matumaini kwa kizazi kipya cha wasanii. Wengi wamepongeza moyo wake wa kuinua vipaji na kuonyesha mshikamano katika kukuza muziki wa ndani. Wimbo wa Cartman unaendelea kupata umaarufu mitandaoni huku mashabiki wakimpongeza Toxic Lyrikali kwa kazi nzuri, na kumshukuru Nyashinski kwa kuonyesha mfano wa kuigwa katika kuendeleza muziki wa Kenya kwa kushirikiana na wale wanaochipuka Wimbo wa “Cartman” wa msanii Toxic Lyrikali hadi kufikia sasa, umefikisha zaidi ya 879,000 ya watazamaji kwenye YouTube tangu kuchapishwa kwake miezi saba iliyopita.

Read More
 Nyashinski awabariki mashabiki zake na EP mpya

Nyashinski awabariki mashabiki zake na EP mpya

Msanii mkongwe nchini Nyashinski ameachia rasmi EP yake mpya inayokwenda kwa jina la “THERAPY. THERAPY EP ambayo ina jumla ya ngoma nne za moto, haina collabo hata moja, kwani ngoma zote Nyashinski  kapita nazo mwenyewe. Ep hiyo ina ngoma kama Night School, Kabla Tudie, Showman,Tunnel Vision na inapatikana kwenye majukwaa yote ya ku-stream muziki duniani. Nyashinski ambaye amekuwa kimya kwa kipindi cha miezi kumi na moja, ameachia EP hiyo wakati huu yupo kwenye maandalizi ya tamasha lake la Shin City ambalo litafanyika Novemba 26 mwaka huu mjini Eldoret.

Read More
 Femi One adokeza ujio wa EP ya pamoja na Nyashinski

Femi One adokeza ujio wa EP ya pamoja na Nyashinski

Rapa Femi One ametangaza ujio wa EP yake mpya ambayo huenda akamshirikisha Nyashinsiki au Khaligraph Jones. Kwenye mahojiano na The Trend ya NTV rapa huyo ambaye anafanya vizuri na single yake mpya “Lip Service” amesema yupo mbioni kufanikisha hilo kwa kuwa tayari ameanza mazungumzo na marapa hao kuhusu mpango wa kufanya EP ya pamoja. Utakumbuka Femi One amefanya kazi ya pamoja na Nyashinski kupitia wimbo uitwao “Properly” na Khaligraph Jones kupitia ngoma inayokwenda kwa jina la “Blue Ticks”.

Read More
 NYASHINSKI ATANGAZWA BALOZI MPYA WA JOHNNIE WALKER

NYASHINSKI ATANGAZWA BALOZI MPYA WA JOHNNIE WALKER

Staa wa muziki nchini Nyashinski ameingia ubia wa kufanya kazi na chapa (brand) ya Johnnie Walker kama balozi mpya wa kinywa hicho. Kupitia mitandao yake ya kijamii Hitmaker huyo wa “Properly” ameshindwa kuficha furaha yake kwa kusema kwamba atatumia nafasi hiyo kukitangaza kinywaji hicho nchi nzima Awali uongozi wa Johnnie Walker ulisema umeamua kumchagua Nyanshinki kuwa balozi wao kutokana na umaarufu na ushawishi wake kwenye jamii ambapo ulidai atatumia nafasi yake ya usanii kukitangaza vyema.

Read More
 NYASHINSKI ATANGAZA UJIO WA ONESHO LAKE LA MUZIKI MWEZI APRILI MWAKA 2022

NYASHINSKI ATANGAZA UJIO WA ONESHO LAKE LA MUZIKI MWEZI APRILI MWAKA 2022

Msanii nyota nchini Nyashinski ametangaza kuja na onesho lake liitwalo Shin City ambalo litafanyika mwezi Aprili mwaka huu wa 2022. Kupitia mitandao yake ya kijamii Nyashinski ametusanua kuhusu ujio wa onesho la Shin City kwa kushare bango la onesho hilo ambalo kwa mujibu wake litafanyika Aprili 16 katika ukumbi wa Burudani wa Carnivore Jijini Nairobi. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Properly” ametoa wito kwa mashabiki zake kuanza kununua tiketi za Show hiyo mapema kupitia wavutia www.tokea.com. Tangazo la Nyashinski linakuja wiki kadhaa baada ya kudai kuwa ana mpango wa kujenga mji wake nchini Kenya katika siku za hivi karibuni kwenye moja performance yake jambo lilowaacha mashabiki na maswali mengi. Hata hivyo hatua ya rapa huyo kudai kuwa anakuja mji wake inaonekana kwamba ilikuwa ni njia kuwatangazia mashabiki zake kuhusu ujio wa onesho lake la Shin City.

Read More
 RAPPER  MKONGWE KUTOKA KENYA NYASHINSKI ADOKEZA MPANGO WA KUJENGA MJI WAKE

RAPPER MKONGWE KUTOKA KENYA NYASHINSKI ADOKEZA MPANGO WA KUJENGA MJI WAKE

Msanii nyota nchini Nyashinski ameahidi kujenga mji wake mpya  nchini Kenya, mji ambao utatumika na mashabiki zake Nyashinski ameyaweka wazi hayo Februari 13 mwaka huu kwenye moja ya performance yake iliyofanyika huko Two River Mall jijini Nairobi. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Properly” alienda mbali na kuwashauri wasanii wa muziki nchini watoa nyimbo zenye maudhui safi zitakazodumu kwa muda mrefu. Hata hivyo amewaacha mashabiki zake na maswali mengi mara baada ya kufuta post zake zote kwenye mtandao wa instagram jambo ambalo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa huenda rapa huyo ana matatizo ya kiakili huku wengine wakisema huenda ana mpango wa kuachia project yake mpya

Read More