Nyashinski Atangaza Tarehe Rasmi ya Albamu Mpya “Yariasu”

Nyashinski Atangaza Tarehe Rasmi ya Albamu Mpya “Yariasu”

Mwanamuziki nguli wa Kenya, Nyashinski, amethibitisha kuwa albamu yake mpya itajulikana kwa jina “Yariasu” na itaingia sokoni tarehe 19 Septemba 2025. Albamu hiyo inabeba jumla ya nyimbo 13, ambazo msanii huyo amezitaja kuwa za moto na zimeandaliwa kwa ubora wa kimataifa. Kupitia mitandao ya kijamii, Nyashinski amewataka mashabiki wake kufanya pre-order ya albamu hiyo mtandaoni ili kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuisikiliza mara tu itakapotoka. Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wake wameonekana kutaka zaidi, wakimhimiza kuachia albamu yote kwa pamoja badala ya kutoa ngoma moja moja. Licha ya maoni hayo, tayari Nyashinski ameachia nyimbo mbili kutoka kwenye albamu hiyo, ambazo ni “Tai Chi” na “P.i.c”, zilizopokelewa kwa shangwe na mashabiki wake. Albamu ya “Yariasu” inatarajiwa kuwa miongoni mwa matoleo makubwa zaidi ya mwaka huu, ikidumisha nafasi ya Nyashinski kama mmoja wa wasanii wakubwa na wabunifu zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Read More
 Nyashinski Atangaza Album Mpya ya Kiwango cha Kimataifa

Nyashinski Atangaza Album Mpya ya Kiwango cha Kimataifa

Mwanamuziki kutoka Kenya, Nyashinski, ametangaza ujio wa album yake mpya ambayo kwa mujibu wake itakuwa na kiwango cha kimataifa. Akizungumza kuhusu mradi huo, Nyashinski amesema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akiwaburudisha mashabiki wa Afrika Mashariki kupitia nyimbo zake, lakini sasa ameamua kupeleka muziki wake kwenye jukwaa la dunia. Msanii huyo amefichua kuwa amekuwa akirekodi album hiyo kwa takribani miezi minane, na kwa sasa yupo kwenye hatua za mwisho kukamilisha video za nyimbo zitakazojumuishwa kwenye kazi hiyo. Kwa mujibu wa tracklist iliyoichapishwa mtandaoni na Nyashinski, album hiyo inatarajiwa kuwa na jumla ya nyimbo 13, ikiwemo ngoma zinazojulikana kama Tai Chi na P.I.C. Amewataka mashabiki wake kujiandaa kwa safari ya kipekee ya muziki, akiwahimiza kuisikiliza album hiyo kuanzia wimbo wa kwanza hadi mwisho, akiahidi itakuwa tofauti na kazi zake za awali. Hii inakuja wiki chache baada ya kujiunga na kampuni kubwa ya muziki, Sony Music, hatua inayotajwa kufungua milango ya kimataifa kwa safari yake ya kisanii.

Read More
 Nyashinski Asaini Mkataba wa Kihistoria na Sony Music

Nyashinski Asaini Mkataba wa Kihistoria na Sony Music

Mwanamuziki nyota wa Kenya, Nyashinski, amesaini mkataba wa kihistoria na kampuni kubwa ya muziki duniani, Sony Music, hatua inayotajwa kama msukumo mkubwa kwa muziki wa Afrika Mashariki kuingia kwenye jukwaa la kimataifa. Sony Music imemsifu Nyashinski kama msanii halisi na mwenye vipaji vingi ambaye muziki wake wa kipekee unaweza kugusa watu wa tamaduni mbalimbali. Kampuni hiyo inaamini kuwa ubunifu wake utasaidia kuinua zaidi hadhi ya muziki wa eneo hilo duniani. Mkataba huo pia unampa Nyashinski nafasi ya kuonyesha vipaji vya Afrika Mashariki kwa hadhira ya kimataifa, pamoja na kurejesha nyimbo zake maarufu kwenye majukwaa ya muziki mtandaoni kote duniani. Hatua hii itawawezesha mashabiki wa zamani na wapya kufurahia nyimbo zake zote bila vikwazo. Makubaliano haya yanaonekana kama hatua ya kihistoria kwa sekta ya muziki wa Afrika Mashariki, yakifungua milango zaidi ya wasanii wa eneo hili kushirikiana na soko la kimataifa.

Read More
 Toxic Lyrikali Apata Baraka za Nyashinski Baada ya Mafanikio ya ‘Cartman’ YouTube

Toxic Lyrikali Apata Baraka za Nyashinski Baada ya Mafanikio ya ‘Cartman’ YouTube

Msanii nyota wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Nyashinski, ameonyesha wazi kuunga mkono na kubariki kazi ya rapper chipukizi Toxic Lyrikali kupitia wimbo wake mpya uitwao “Cartman”. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Nyashinski alielezea kuvutiwa na ubunifu wa wimbo huo, akithibitisha kuwa anatambua na kuthamini kipaji cha msanii huyo anayeinukia. Kwa kutumia ushawishi wake mkubwa katika tasnia ya muziki, Nyashinski aliipa kazi ya Toxic Lyrikali msukumo wa kipekee, hatua ambayo imeibua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa hip hop. Kutoka kwa mashairi hadi uwasilishaji, wimbo huo umesifiwa kwa ubora wake na kuonekana kama hatua muhimu kwa msanii huyo chipukizi. Baraka kutoka kwa Nyashinski, ambaye anatambulika kama mmoja wa magwiji wa muziki wa Kenya, imechukuliwa na mashabiki na wadau wa muziki kama ishara ya matumaini kwa kizazi kipya cha wasanii. Wengi wamepongeza moyo wake wa kuinua vipaji na kuonyesha mshikamano katika kukuza muziki wa ndani. Wimbo wa Cartman unaendelea kupata umaarufu mitandaoni huku mashabiki wakimpongeza Toxic Lyrikali kwa kazi nzuri, na kumshukuru Nyashinski kwa kuonyesha mfano wa kuigwa katika kuendeleza muziki wa Kenya kwa kushirikiana na wale wanaochipuka Wimbo wa “Cartman” wa msanii Toxic Lyrikali hadi kufikia sasa, umefikisha zaidi ya 879,000 ya watazamaji kwenye YouTube tangu kuchapishwa kwake miezi saba iliyopita.

Read More
 Nyashinski awabariki mashabiki zake na EP mpya

Nyashinski awabariki mashabiki zake na EP mpya

Msanii mkongwe nchini Nyashinski ameachia rasmi EP yake mpya inayokwenda kwa jina la “THERAPY. THERAPY EP ambayo ina jumla ya ngoma nne za moto, haina collabo hata moja, kwani ngoma zote Nyashinski  kapita nazo mwenyewe. Ep hiyo ina ngoma kama Night School, Kabla Tudie, Showman,Tunnel Vision na inapatikana kwenye majukwaa yote ya ku-stream muziki duniani. Nyashinski ambaye amekuwa kimya kwa kipindi cha miezi kumi na moja, ameachia EP hiyo wakati huu yupo kwenye maandalizi ya tamasha lake la Shin City ambalo litafanyika Novemba 26 mwaka huu mjini Eldoret.

Read More
 Femi One adokeza ujio wa EP ya pamoja na Nyashinski

Femi One adokeza ujio wa EP ya pamoja na Nyashinski

Rapa Femi One ametangaza ujio wa EP yake mpya ambayo huenda akamshirikisha Nyashinsiki au Khaligraph Jones. Kwenye mahojiano na The Trend ya NTV rapa huyo ambaye anafanya vizuri na single yake mpya “Lip Service” amesema yupo mbioni kufanikisha hilo kwa kuwa tayari ameanza mazungumzo na marapa hao kuhusu mpango wa kufanya EP ya pamoja. Utakumbuka Femi One amefanya kazi ya pamoja na Nyashinski kupitia wimbo uitwao “Properly” na Khaligraph Jones kupitia ngoma inayokwenda kwa jina la “Blue Ticks”.

Read More
 NYASHINSKI ATANGAZWA BALOZI MPYA WA JOHNNIE WALKER

NYASHINSKI ATANGAZWA BALOZI MPYA WA JOHNNIE WALKER

Staa wa muziki nchini Nyashinski ameingia ubia wa kufanya kazi na chapa (brand) ya Johnnie Walker kama balozi mpya wa kinywa hicho. Kupitia mitandao yake ya kijamii Hitmaker huyo wa “Properly” ameshindwa kuficha furaha yake kwa kusema kwamba atatumia nafasi hiyo kukitangaza kinywaji hicho nchi nzima Awali uongozi wa Johnnie Walker ulisema umeamua kumchagua Nyanshinki kuwa balozi wao kutokana na umaarufu na ushawishi wake kwenye jamii ambapo ulidai atatumia nafasi yake ya usanii kukitangaza vyema.

Read More
 NYASHINSKI ATANGAZA UJIO WA ONESHO LAKE LA MUZIKI MWEZI APRILI MWAKA 2022

NYASHINSKI ATANGAZA UJIO WA ONESHO LAKE LA MUZIKI MWEZI APRILI MWAKA 2022

Msanii nyota nchini Nyashinski ametangaza kuja na onesho lake liitwalo Shin City ambalo litafanyika mwezi Aprili mwaka huu wa 2022. Kupitia mitandao yake ya kijamii Nyashinski ametusanua kuhusu ujio wa onesho la Shin City kwa kushare bango la onesho hilo ambalo kwa mujibu wake litafanyika Aprili 16 katika ukumbi wa Burudani wa Carnivore Jijini Nairobi. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Properly” ametoa wito kwa mashabiki zake kuanza kununua tiketi za Show hiyo mapema kupitia wavutia www.tokea.com. Tangazo la Nyashinski linakuja wiki kadhaa baada ya kudai kuwa ana mpango wa kujenga mji wake nchini Kenya katika siku za hivi karibuni kwenye moja performance yake jambo lilowaacha mashabiki na maswali mengi. Hata hivyo hatua ya rapa huyo kudai kuwa anakuja mji wake inaonekana kwamba ilikuwa ni njia kuwatangazia mashabiki zake kuhusu ujio wa onesho lake la Shin City.

Read More
 RAPPER  MKONGWE KUTOKA KENYA NYASHINSKI ADOKEZA MPANGO WA KUJENGA MJI WAKE

RAPPER MKONGWE KUTOKA KENYA NYASHINSKI ADOKEZA MPANGO WA KUJENGA MJI WAKE

Msanii nyota nchini Nyashinski ameahidi kujenga mji wake mpya  nchini Kenya, mji ambao utatumika na mashabiki zake Nyashinski ameyaweka wazi hayo Februari 13 mwaka huu kwenye moja ya performance yake iliyofanyika huko Two River Mall jijini Nairobi. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Properly” alienda mbali na kuwashauri wasanii wa muziki nchini watoa nyimbo zenye maudhui safi zitakazodumu kwa muda mrefu. Hata hivyo amewaacha mashabiki zake na maswali mengi mara baada ya kufuta post zake zote kwenye mtandao wa instagram jambo ambalo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa huenda rapa huyo ana matatizo ya kiakili huku wengine wakisema huenda ana mpango wa kuachia project yake mpya

Read More