Odi wa Murang’a atuhumiwa kuiba wimbo wa Shekina Karen

Odi wa Murang’a atuhumiwa kuiba wimbo wa Shekina Karen

Mrembo anafanya vizuri na wimbo wa “Daidai” Shekina Karen amebuika na kumtuhumu msanii Odi wa Muranga kwa kuiba ubunifu wa wimbo wake uitwao “Iende” aliouachia miezi sita iliyopita. Mrembo huyo amesema yeye ndiye wa kwanza kurekodi wimbo huo ambao alikuwa amemshirikisha Smady wa Mbogi Genje lakini alishangazwa na hatua ya Odi kuchukua mashairi pamoja na jina la wimbo wake huo bila ridhaa yake na kuutumia kwenye wimbo uitwao “Sugu Iendee” aliowashirikisha wasanii Micharazzo na Smady. Kwenye mahjiano na podcast ya KIPAWA amesema licha ya kuwasilisha lalama zake kwa msanii huyo ameingiwa na jeuri ya kutochukua simu zake, jambo ambalo anadai limeumiza sana kiasi cha kulia kila mara wimbo wake wa “Iendee” unapochezwa redioni. Hata hivyo amesema kutokana na Odi wa Muranga kumdhulumiwa haki yake amemuachia mwenyezi kwa kila kitu kwa kuwa ana uwezo wa kupishana na ambaye amekataa kumrudishia fadhila licha ya kutumia ubunifu wa wimbo wake bila makubaliano yeyote kati yao. Mpaka sasa Odi wa Muranga, Micharazo na Smady hawajajibu tuhuma zilizoibuliwa na mrembo huyo dhidi yao ila ni jambo la kusubiriwa.

Read More
 ODI WA MURANG’A AMCHANA VDJ JONES KISA EDU MADOXX WA BOONDOCKS GANG

ODI WA MURANG’A AMCHANA VDJ JONES KISA EDU MADOXX WA BOONDOCKS GANG

Msanii Odi wa Murang’a amemtolea uvivu VDJ Jones baada ya DJ huyo kudai kuwa msanii wa Boondocks Gang Edu Madoxx alizembea kwenye muziki kutokana na kuathirika na matumizi ya dawa za kulevya. Katika mahojiano na Mungai Eve Amemtaka VDJ Jones aache suala la kutumia stori ya Edu Madoxx kujitafutia kiki na badala yake ajishughulisha na mambo yatakayomsaidia maishani kwani angekuwa mtu mwema angekuwa amewasaidia wasanii wanaothirika na dawa za kulevya. Lakini pia hajamzaza msanii wa Sailors Gangs Cocos Juma kwa kuhoji kuwa mbona hakuzungumza masaibu yake na lebo ya Black Market Records kabla Maddox hajaweka wazi stori yake akiwa chini ya Boondocks gang ambapo ameenda mbali Zaidi na kusema kwamba Cocos Juma sio msanii kwani watu wanafahamu kama mtu wa kupiga mayowe. Kauli ya Odi wa Murang’a mara baada ya yeye pamoja na msanii Exray kujitokeza na kukanusha madai ya kumtelekeza Edu Maddox katika kundi la Boondocks Gangs.

Read More