MUME WA ZAMANI JENIFFER LOPEZ ATOA YA MOYONI KUHUSU NDOA MPYA YA MWANAMAMA HUYO
Aliyewahi kuwa mume wa mwanamuziki Jennifer Lopez, Bw. Ojani Noah halioni penzi na ndoa ya Ex wake JLo na Ben Affleck likidumu, anadai wataachana tu. Ojani Noah amesema ndoa ya wawili hao haitodumu kutokana na tabia ya mwanamama Jennifer Lopez kuwahi kuzama kwenye mapenzi yaani mwepesi wa kupenda kwa haraka. Kupitia mahojiano na Dail Mail, Ex wa JLO, Ojani Noah ambaye alifunga ndoa na Jlo mwaka 1997 na kuachana baada ya miezi 11 baadae, ameliambia gazeti hilo kuwa, “Namtakia yeye na Ben kila la kheri, lakini sishawishiki kama ndoa itadumu, nahisi ni mtu ambaye ataolewa mara 7 au 8. Sioni akitulia na mtu mmoja”. Ikumbukwe, ndoa ya JLO na Ben Affleck ni ndoa ya NNE kwa JLO, walifungua ndoa hiyo Julai mwaka huu.
Read More