Omah Lay Aonya Kuhusu Mafundisho Potofu Katika Dini

Omah Lay Aonya Kuhusu Mafundisho Potofu Katika Dini

Mwanamuziki maarufu kutoka Nigeria, Omah Lay, ametoa maneno ya ushauri kwa mashabiki wake, akiwataka kuzingatia maisha yao binafsi na kutafuta ukweli. Katika ujumbe wake Instagram, msanii huyo alisema wazi kuwa watu hawapaswi kuendeshwa kiholela na baadhi ya viongozi wa kidini, akiwataja kuwa “wajinga” wanaoweza kupotosha na kuondoa watu kwenye njia ya ukweli. Omah Lay alisisitiza kwamba kila mtu anapaswa kujipenda, kujitambua na kutafuta ukweli, badala ya kuishi maisha ya hofu yanayochochewa na mafundisho yasiyo na msingi. Aidha, nyota huyo wa muziki alionekana kulenga moja kwa moja tabia ya baadhi ya waumini wanaokubali kila wanachoambiwa bila kuhoji, jambo alilolieleza kama kikwazo cha maendeleo binafsi na kijamii. Kauli hii imezua hisia mseto miongoni mwa mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii. Wengine wameunga mkono wakisema ni wito wa kuamsha fikra huru na kupunguza unafiki wa kidini, huku wengine wakimshutumu kwa kutumia maneno makali dhidi ya imani.

Read More
 PENZI LA TANASHA DONNA NA OMAH LAY  LAKOLEA MITANDAONI

PENZI LA TANASHA DONNA NA OMAH LAY LAKOLEA MITANDAONI

Moja kati ya headlines zinazo gonga vichwa vya habari mtandaoni ni issue inayomtaja mwanamuziki wa Nigeria Omah Lay kutoka kimapenzi na staa wa muziki nchini Tanasha Donna, sakata ambalo kila mtu analizungumzia katika namna yake. Katika nyakati tofauti tofauti kwa pamoja kupitia insta story zao kwenye mtandao wa Instagram Wawili hao wameshare picha zinazo onekana kushabihiana eneo moja ikiwemo hoteli wanaodaiwa kuwa wamekuwa wakijivinjari huko Mombasa huku wote wakipost kwenye muda unao tofautiana dakika moja tu. Vyanzo vya karibu na Tanasha, vinadai Hitmaker huyo wa “Gere” na Omah Lay wamekuwa pamoja mjini Mombasa tangu msanii huyo atue nchini Kenya jambo linalodaiwa kuwa lilimpelekea Omah Lay kususia kutumbuiza katika tamasha la Beach Fest  kwenye mkesha wa kuamkia mwaka mpya kutokana na kulewa na penzi la Tanasha Donna. Tetesi za Tanasha na Omah Lay kuwa kwenye mahusiano zilianza mwaka jana walipoonekana pamoja nchini Nigeria na Sudan Kusini wakiwa wanakula bata pamoja lakini pia walikuwa wakiachia comment za mahaba kwenye picha zao kwenye mtandao wa instagram jambo liliwaaminisha mashabiki kuna kitu kinaendelea kati yao. Hata hivyo hakuna mmoja kati yao amejitokeza kuthibitisha kama kweli wapo kwenye mahusiano ila ni jambo la kusubiriwa maana waswahili wana msemo wao unaosema penzi ni kikozi na halifichiki.

Read More