Ommy Dimpoz Azua Gumzo Mtandaoni Kuhusu mipaka ya mahusiano ya kimapenzi

Ommy Dimpoz Azua Gumzo Mtandaoni Kuhusu mipaka ya mahusiano ya kimapenzi

Msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz, ameingia kwenye vichwa vya habari baada ya kuchapisha ujumbe wenye utata kupitia Insta Story yake, ambao umewasha moto wa mijadala mitandaoni kuhusu maadili, uaminifu, na mipaka ya mahusiano ya kimapenzi. Katika ujumbe huo, Ommy alionyesha msimamo wake kuhusu wanawake wanaokubali msaada wa chakula kutoka kwa wanaume ambao si wapenzi wao, akifananisha kitendo hicho na usaliti. ”Kumruhusu mwanaume ambaye sio boyfriend/mwanaume wako akununulie chakula huko napo nikucheat ni kwasababu una njaa unashindwa kuelewa,” Aliandika Instagram. Kauli hiyo imechochea mijadala mikali kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii, huku wengi wakitoa maoni yanayotofautiana kuhusu uhalali na uzito wa hoja hiyo. Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii wameunga mkono mtazamo wa msanii huyo, wakieleza kuwa ni muhimu kwa mtu aliye kwenye mahusiano kuwa na mipaka ya wazi ili kulinda uaminifu na heshima ndani ya uhusiano. Wengine, hata hivyo, wamekosoa kauli hiyo wakisema kuwa inaleta tafsiri potofu ya usaliti, na kwamba kusaidiwa chakula au huduma ndogo kutoka kwa mtu mwingine haipaswi kuchukuliwa kama usaliti, hasa ikiwa hakuna hisia za kimapenzi zinazohusika. Hadi kufikia sasa, Ommy Dimpoz hajatoa ufafanuzi zaidi kuhusu dhamira ya kauli hiyo, lakini mjadala unaoendelea unaonesha kuwa masuala ya mahusiano, msaada wa kijamii na mipaka ya kijinsia bado ni mada nyeti katika jamii ya sasa.

Read More
 Ommy Dimpoz anyosha maelezo juu ya kuwashirikisha wasanii wa kifaransa kwenye album yake mpya

Ommy Dimpoz anyosha maelezo juu ya kuwashirikisha wasanii wa kifaransa kwenye album yake mpya

Msanii wa Bongofleva, Ommy Dimpoz amesema wamewashirisha Fally Ipupa kutokea DR Congo na DJ Kerozen wa Ivory coast katika albamu yake ili kupata wasikilizaji wengi kwenye nchi zinazozungumza Kifaransa. Albamu hiyo inayokwenda kwa jina la Dedication ilitoka Ijumaa hii ikiwa na nyimbo 10, hii imesimamiwa na Rockstar Africa na Sony Music Africa. Wasanii wa Bongofleva walioshirikishwa katika albamu hiyo ni Nandy na Marioo. Ommy Dimpoz amesema DJ Kerozen ni msanii maarufu sana Afrika Magharibi wanapozunguza sana Kifaransa, hivyo anaamini hiyo itaibeba vilivyo albamu yake, hivyo hivyo upande wa Fally Ipupa.

Read More
 Ommy Dimpoz aachia rasmi album yake mpya

Ommy Dimpoz aachia rasmi album yake mpya

Mwimbaji nyota wa muziki nchini Tanzania, Ommy Dimpoz ameachia rasmi album yake mpya iitwayo Dedication kupitia majukwaa mbalimbali ya ku-stream muziki mitandaoni. Album hiyo yenye jumla ya ngoma 15, imewakutanisha wanamuziki wengine kama Marioo na Nandy toka Tanzania, na nje ya Tanzania ni Blaq Diamond, Fally Ipupa, The Ben, DJ Maphorisa, DJ Kerozen, Kabza na Julio Masidi. Mtayarishaji mkuu wa album hiyo ni ommydimpoz mwenyewe ikiwa pia ndio album yake ya kwanza kuiachia katika safari yake ya muziki.

Read More
 Ommy Dimpoz kuachia album yake mpya mwezi Novemba mwaka huu

Ommy Dimpoz kuachia album yake mpya mwezi Novemba mwaka huu

Mwanamuziki Ommy Dimpoz ametangaza rasmi jina la Album yake mpya na ya kwanza kwenye Muziki, inaitwa ‘Dedication’ na itakuwa na Jumla ya nyimbo 15. Album hiyo ambayo itaachiwa November 4 mwaka huu, Dimpoz amewapa shavu wakali wa Afrika akiwemo Nandy, Fally Ipupa, Blaq Diamond, The Ben na wengine. Aidha, kupitia ukurasa wake wa Instagram, ameeleza kwamba haikuwa rahisi kuikamilisha album hiyo ukizingatia mapito aliyoyapitia miaka ya hivi karibuni. Hata hivyo ametoa shukrani zake za dhati kwa wote waliomsaidia kufika alipo leo ikiwemo familia yake pia.

Read More
 OMMY DIMPOZ AKIRI KUWAHI KUWEKEA SUMU ILI AFE

OMMY DIMPOZ AKIRI KUWAHI KUWEKEA SUMU ILI AFE

Nyota wa muziki nchini Tanzania, msanii Ommy Dimpoz amekiri mbele ya mashabiki kuwahi kuwekewa sumu ili afe, katika tukio lilitokea mwaka 2018 lililomfanya akafanyiwa oparesheni tatu kubwa ya koo lake akipambania kuokoa maisha yake. Akiwa na mwimbaji Christian Bella, ndani ya ‘Break Point’ Makumbusho, waliitumbiza pamoja kolabo yao “Nani Kama Mama” ambapo kwenye verse yake Ommy Dimpoz alisikika akisema, “Sumu Waliniwekea, Bado Nusu Nikufuate Mama” akiwa na maana kwa sasa angekuwa marehemu, kwani ilibaki kidogo amfuate mama yake ambaye ameshatangulia mbele za haki. Ommy Dimpoz ambaye ameuanza vyema mwaka huu akiwa tayari ameachia ngoma mbili, aliwahi kusema athari ya koo lake ni matokeo ya sumu. Na kwenye interview yake na Millard, Ommy alisimulia sauti yake ilivyorudi, ni kabla hajapelekwa Ujerumani alikofanyiwa oparesheni ya tatu ambayo ilikuwa ya mwisho. Ikumbukwe, ni takribani miaka mitatu sasa imepita Dimpoz hakuonekana jukwaani akitumbuiza. Hata hivyo hii inakuwa mara yake ya pili baada ya Machi 20 mwaka huu, kutumbuiza kwenye tamasha lake aliloliita “Cheusi Cheupe” lililofanyika katika viwanja vya Zakhem, Mbagala jijini Dar es salaam.

Read More
 OMMY DIMPOZ AFUNGUKA SABABU YA KUTOWEKA WAZI MAHUSIANO YAKE YA KIMAPENZI

OMMY DIMPOZ AFUNGUKA SABABU YA KUTOWEKA WAZI MAHUSIANO YAKE YA KIMAPENZI

Msanii wa Bongofleva, Ommy Dimpoz amesema kuwa wasichana wengi wanatamani kuolewa na yeye na kila mara amekuwa akipokea maombi yao. Ommy Dimpoz amesema hayo kwenye Podcast ya Lil Ommy ambapo ametaja hiyo ni moja ya sababu ya kutomuweka wazi mpenzi wake rasmi kwani anajua kufanya hivyo atawaumiza wengi. “Kuna wasichana wengi sana kila siku wanalia nioe mimi, hizo nishazoea, ni kawaida, nina uhakika na watu wengine inawatokea lakini mimi naweza kuwa baba yao kwenye suala hilo” amesema Ommy. “Lakini katika suala hilo (kuoa) mimi Muislamu naruhusiwa hao wanne, kwa hiyo inawezekana hata sasa hivi nina hao wanne wa kuwapima, kwa hiyo time itakapofika haina shida,” amesema. Ommy Dimpoz anayefanya vizuri kwa sasa na wimbo wake mpya, Umeniweza, ameongeza kuwa kwa sasa hana mtoto lakini kabla ya mwaka huu kuisha mambo yanaweza kuwa mazuri, yaani kupata mtoto.

Read More