Parroty Afufua Bifu na Toxic Lyrikali Kupitia Picha ya Siri

Parroty Afufua Bifu na Toxic Lyrikali Kupitia Picha ya Siri

Msanii wa muziki wa gengetone, Parroty Vunulu, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuwaomba mashabiki wake kumsaidia kutambua picha ya mwanaume asiyejulikana ambaye amekuwa akijitokeza mara kwa mara kwenye sehemu ya maoni ya mitandao yake ya kijamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Parroty aliahidi kumpa zawadi ya KSh 1,000 shabiki atakayefanikisha kumtambua mwanaume huyo. Ingawa hakumtaja moja kwa moja, mashabiki wengi wamehusisha picha hiyo na rapa Toxic Lyric Kali, anayejulikana kwa wimbo Backbencher. Inadaiwa kuwa Parroty na Toxic Lyric Likali hawako kwenye uhusiano mzuri baada ya madai kwamba rapa huyo alimuaibisha Parroty mtandaoni alipomwomba kufanya kolabo. Tukio hili limeendeleza mvutano wa chini kwa chini kati ya wasanii hao, huku mashabiki wakisubiri kuona kama Toxic Lyrikali.

Read More
 Parroty Awakosoa Watu Maarufu kwa Ukimya wao Katika Masuala ya Kijamii

Parroty Awakosoa Watu Maarufu kwa Ukimya wao Katika Masuala ya Kijamii

Msanii maarufu wa muziki wa Gengetone, Parroty, ameibua mjadala mkali baada ya kuwakosoa vikali watu maarufu nchini Kenya kwa kutochukua msimamo kuhusu changamoto za kijamii zinazolikumba taifa. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa Instagram, Parroty alieleza kusikitishwa na kile alichokiita kupuuza kwa makusudi matatizo ya wananchi na kuweka mbele maslahi binafsi. Alisema kuwa kuna ongezeko la wasanii, wachekeshaji, wanamitandao maarufu na wanamichezo ambao wanachagua kukaa kimya kuhusu masuala nyeti kama umasikini, ukosefu wa haki, ufisadi, na ukatili wa polisi, wakijikita zaidi katika maisha ya anasa na biashara binafsi. Kwa mujibu wa Parroty, watu maarufu wamekuwa wakitumia majukwaa yao kwa malengo ya kibinafsi badala ya kuhamasisha mabadiliko ya kijamii. Alielezea kuwa hali hiyo imesababisha mwanya mkubwa kati yao na mashabiki wanaowategemea kama sauti ya mabadiliko. Katika ujumbe wake, Parroty alitumia maneno makali kuwaelezea watu maarufu wanaoweka mbele matumbo yao kuliko utu na haki za wananchi. Alisisitiza kuwa umaarufu unapaswa kutumika kama jukwaa la kuhamasisha jamii na kushinikiza mabadiliko chanya. Kauli yake imekuja katika kipindi ambapo taifa linakumbwa na hasira kufuatia kifo cha bloga Albert Ojwang, aliyeripotiwa kufariki akiwa mikononi mwa polisi. Tukio hilo limezua maandamano na hisia kali miongoni mwa wananchi waliotaka uwajibikaji na haki kutendeka. Ujumbe wa Parroty umeungwa mkono na sehemu kubwa ya wananchi mitandaoni, wengi wao wakielezea kuwa ni wakati muafaka kwa watu mashuhuri kuacha kukaa kimya na kuchukua hatua madhubuti katika kupigania ustawi wa jamii.

Read More
 Msanii Tipsy Gee Amshutumu Militan wa Mbogi Genje kwa Kukata Dreadlocks za Parroty kwa Mabavu

Msanii Tipsy Gee Amshutumu Militan wa Mbogi Genje kwa Kukata Dreadlocks za Parroty kwa Mabavu

Msanii wa muziki wa Arbantone, Tipsy Gee, amezua mjadala mkali mtandaoni baada ya kumkemea vikali Militan, mmoja wa wanachama wa kundi la rap maarufu Mbogi Genje, kwa kile alichokiita kitendo cha kumvamia yeye na rafiki yake, Parroty, na kumnyoa dreadlocks zake kwa nguvu bila ridhaa yake. Tukio hilo lilitokea baada ya Parroty awali kuahidi kukata rasta zake endapo timu yake ya Manchester United ingefungwa na Tottenham Hotspur. Hata hivyo, licha ya Tottenham kushinda mechi hiyo, Parroty alibadilisha msimamo wake na kuomba msamaha kwa mashabiki, akisema kuwa angeacha kuishabikia Manchester United badala ya kukata rasta zake. Kwa mujibu wa Tipsy Gee, Militan alichukua sheria mkononi kwa kumshambulia Parroty na kumkata nywele bila makubaliano, kitendo ambacho kimezua hasira na lawama kutoka kwa wafuasi wa Parroty na wapenzi wa muziki wa mtaa. Mashabiki wengi wamejitokeza mitandaoni kulaani tukio hilo, wakilitaja kama ukiukaji wa haki ya mtu binafsi na ukosefu wa heshima. Wengine wameitaka Mbogi Genje kutoa msimamo rasmi kuhusu tukio hilo, huku wengine wakitaka hatua za kisheria zichukuliwe. Hadi sasa, Militan hajatoa tamko lolote rasmi kuhusiana na madai hayo. Tukio hili linaendelea kuzua mjadala mpana kuhusu mipaka ya mizaha, ahadi za mashabiki wa soka, na heshima kwa maamuzi ya mtu binafsi.

Read More
 Parroty Vunulu Aomba Msamaha kwa Kukataa Kunyoa Dreadlocks Zake Baada ya Manchester United Kupoteza

Parroty Vunulu Aomba Msamaha kwa Kukataa Kunyoa Dreadlocks Zake Baada ya Manchester United Kupoteza

Msanii wa Gengetone nchini Kenya, Parroty Vunulu, ameomba radhi kwa mashabiki na umma baada ya kutotimiza ahadi yake ya kunyoa rasta zake iwapo klabu ya Manchester United ingepoteza mechi dhidi ya Tottenham Hotspur. Parroty, ambaye alikuwa ameapa kunyoa dreadlocks zake alizozilea kwa miaka tisa endapo United wangeshindwa, amebadili msimamo wake na kusema hawezi kupoteza utambulisho wake kwa sababu ya matokeo ya mpira. “Heri niache kusupport Manchester United lakini nisipoteze image yangu,” alisema Parroty katika ujumbe aliouweka mitandaoni, akichanganya ucheshi na ukweli kuhusu uamuzi wake wa kutokata nywele hizo. Akiendelea kueleza sababu za kubadili uamuzi wake, Parroty alisema kuwa dreadlocks hizo ni sehemu muhimu ya chapa yake ya kisanii na kimtindo, na kwamba kunyoa nywele hizo kungemgharimu shughuli nyingi za kibiashara. “Nawaomba mashabiki wanielewe. Hizi rasta ndizo zimenitambulisha kwenye game, na kwa kweli zimenisaidia sana kibiashara. Nikizikata, ni kama najifuta kwenye ramani ya muziki,” aliongeza Parroty. Msanii huyo pia alifichua kuwa ana mpango wa kuandaa sherehe maalum ya kusherehekea miaka tisa ya kulea dreadlocks zake mwezi Septemba, kama njia ya kutambua safari yake ya kipekee ya mitindo ya nywele na kujieleza kisanii. “Niko na plan ya birthday kali Septemba. Sitaki tu kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali pia juhudi za kulea hizi rasta kwa miaka yote hii,” alisema kwa msisimko. Wakati baadhi ya mashabiki walichukulia hali hiyo kwa utani, wengine walimkumbusha umuhimu wa kushikilia ahadi. Hata hivyo, wengi walionekana kuelewa msimamo wake, wakitambua umuhimu wa muonekano katika kazi yake ya sanaa. Parroty Vunulu anaendelea kuwa mmoja wa wasanii wa Gengetone wanaovutia kutokana na ubunifu, ucheshi na uaminifu kwa mtindo wake wa maisha.

Read More