Kajala aweka wazi matamanio ya kupata mtoto

Kajala aweka wazi matamanio ya kupata mtoto

Mwigizaji wa filamu nchini Tanzania, Kajala ameweka wazi matamanio ya kupata mtoto wa pili ikiwa ni miaka 21 tangu kuzaliwa mtoto wake wa kwanza, Paula. Kupitia insta story yake amesema hatatumia tena madawa ya kuzuia mimba ya P2. “Nafikiri sasa ni muda sahihi wa kupata mdogo wako Dada Paula. Hakuna kutumia P2 tena, niko tayari kuwa mama tena”, unasomeka ujumbe wa Kajala Frida. Aidha, kwa sasa ni wazi Kajala amehamishia uzito wa penzi lake kwa watoto, na hilo amelithibitisha kwa kumfanyia (Suprise) binti yake Paula Kauli ya Kajala inakuja wiki kadhaa baada ya kuachana na Mchumba wake, Harmonize. Ikumbukwe mtoto wa kwanza, Paula, Kajala alizaa na Prodyuza wa muziki wa Bongofleva, P Funk Majani kutoka Bongo Records, lakini walikuja wakaachana baada mahusiano kukumbwa na migogoro.

Read More
 PAULA KAJALA AMUITA HARMONIZE BABA KWA MARA YA KWANZA

PAULA KAJALA AMUITA HARMONIZE BABA KWA MARA YA KWANZA

Hatimaye mtoto wa mpenzi wa mwanamuziki Harmonize, Kajala Masanja, aitwaye Paula kwa mara ya kwanza amemtambua Harmonize kama baba yake hadharani kupitia ukurasa wake wa instagram (insta story yake). Paula amemtaja Harmonize kama baba yake akishare kionjo cha wimbo mpya wa Harmonize uitwao Amelowa. Kupitia Instastory yake Paula amepost video hiyo na kisha kuandika “Baba unajua mpaka unajua tena”. Paula hakuishia hapo ameenda mbali zaidi na kuandika, “Utaweza kukomoana na Jeshi wewe?”. Utakumbuka wawili hao wamewahi kuwa katika tofauti kubwa kiasi cha Paula kutomtambua Harmonize kama baba yake alipomvisha mama yake Kajala Masanja pete ya uchumba, kitendo kilichopelekea walimwengu kuhisi kuwa bado ana kinyongo na baba yake Harmonize.

Read More
 JAY MELODY AFUNGUKA KUMTAKA KIMAPENZI PAULA

JAY MELODY AFUNGUKA KUMTAKA KIMAPENZI PAULA

Hit Maker wa Nakupenda, msanii Jay Melody amefunguka juu ya hisia zake kwa Paula Kajala. Hii imekuja baada ya kumpost Mrembo huyo kwenye Ukurasa wake wa Instagram na Kuifuta baada ya Muda. Akiwa kwenye kipindi cha Refresh cha Wasafi TV ametolea ufafanuzi mpaka kupost picha ya Mrembo huyo na baAdae kuifuta hakuwa na nia mbaya kwa Paula kwani alikuwa anamuonyesha upendo wa kawaida. “Mimi therealpaulahkajala Nampenda kama watu wengine ninavyowapenda naziona picha zake nzuri ndio maana nikaamua kumpost lakini nilichokiandika havihusiani na picha yake ndio maana nilitanguliza picha yangu. Hakuna ubaya katika hilo. “Hakuna mtu yoyote alienicheki lakini picha niliifuta baada ya kuona Coment zimekuwa Nyingi hadi wajomba zake nikaona sina haja ya kumtengenezea mtoto wa watu Mawazo nikaona ni bora niifute” Amesema Jay Melody.

Read More