Msanii Petra Aolewa Na Mr. Hamza Katika Harusi ya Kuvutia

Msanii Petra Aolewa Na Mr. Hamza Katika Harusi ya Kuvutia

Msanii wa muziki wa rap kutoka Kenya, Petra, ameanza rasmi maisha mapya ya ndoa baada ya kufunga pingu za maisha na mpenzi wake Bw. Hamza katika sherehe ya kifahari iliyofanyika tarehe 14 Septemba 2025 Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Petra alitangaza habari hiyo njema kwa mashabiki wake akipakia picha za harusi na ujumbe wa kugusa moyo uliodhihirisha imani yake kwa Mungu. Alieleza kuwa yeye na mume wake waliombeana mbele za Mungu, na hatimaye wakabarikiwa kuunganishwa kama mume na mke kama ilivyo katika Mathayo 18:19. Katika ujumbe wake, Petra alifafanua pia maana ya jina la Kiebrania Hamza, ambalo tafsiri yake ni “mkono wa ulinzi” unaohusishwa na Jicho la Mungu, ishara ya baraka na kinga ya kiungu. Alisema kwao, jina la Bwana na Bi Hamza ni zaidi ya cheo cha kifamilia, bali ni alama ya agano takatifu lililotiwa muhuri wa ulinzi wa Mungu. Aidha, alimalizia kwa kumshukuru Mungu Mwenyezi, Bwana Yesu Kristo na Roho Mtakatifu kwa kuwa msingi wa ndoa yao, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni ushuhuda wa neema na utukufu wa Mungu. Tangazo hilo liliibua wimbi la pongezi kutoka kwa mashabiki na wasanii wenzake waliompongeza kwa kuanza ukurasa mpya wa maisha yake kama Bi. Hamza. Harusi hii imekuwa hatua muhimu kwa Petra, ikionyesha sura mpya si tu katika maisha yake ya kifamilia, bali pia katika safari yake ya kiroho na kisanii

Read More
 Petra Awataka Vijana Kuacha Maudhui Yenye Aibu Mitandaoni

Petra Awataka Vijana Kuacha Maudhui Yenye Aibu Mitandaoni

Msanii wa muziki Petra ameibuka na ujumbe mzito unaosisitiza umuhimu wa maadili na uadilifu katika safari ya mafanikio, akisema kuwa mtu hahitaji kushiriki katika maudhui ya ngono au kupoteza utu wake ili kufanikiwa kwenye tasnia ya burudani. Kupitia mitandao ya kijamii, Petra ameeleza kuwa kizazi kipya kinahitaji kuamini kuwa mafanikio ya kweli hayaji kwa njia za kudhalilisha utu. Ameeleza kuwa haijalishi kiwango cha umaarufu mtu alicho nacho kwa sasa, kilicho muhimu ni kusimama na ukweli, akiamini kuwa Mungu anaweza kukuinua bila kuingia kwenye maovu. Kauli ya Petra imekuja baada ya watu wengi mitandaoni kuonekana kupuuzilia mbali wito wa Katibu wa Mazingira jijini Nairobi, Geoffrey Mosiria, aliyeshutumu vikali video ya mwanamitandao maarufu Alicia Kanini iliyosambaa mitandaoni na kubeba maudhui ya ngono. Mosiria aliitaja video hiyo kuwa hatari kwa maadili ya kijamii, akisema ni mfano mbaya kwa vijana, hasa wasichana wadogo. Wito wake umeibua maoni tofauti mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa kusimamia maadili, huku wengine wakihisi kuwa tasnia ya burudani inahitaji uhuru wa kujieleza. Hata hivyo, mjadala huu unaonyesha wazi kuwa suala la maadili katika mitandao ya kijamii na sanaa linaendelea kuwa muhimu hasa kwa kizazi kipya kinachotegemea mtandao kama jukwaa la kuonyesha vipaji.

Read More