Mwanamuziki Rabadaba afufua penzi lake na baby mama wake Sheila Ferguson

Mwanamuziki Rabadaba afufua penzi lake na baby mama wake Sheila Ferguson

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Rabadaba ameripotiwa  kufufua penzi lake na baby mama wake Sheila Ferguson ambaye  kwa pamoja wamejaliwa kuwapata watoto wawili. Chanzo cha karibu kimesema Rabadaba alianza kuwa kwenye mahusiano na Ferguson pindi tu alipotua nchini Uingereza na mke wake Maggie. Licha ya kuwa Maggie alitishia kumrejesha Rabadaba nchini kwao uganda kwa kumsaliti kimapenzi, mwanamuziki huyo kwa sasa inaonekana hana wasiwasi kwa sababu mama ya watoto wake Ferguson atamuokoa ikizingatiwa kuwa ana uraia wa uingereza. Ikumbukwe Rabadaba kwa wiki kadhaa sasa amekuwa kwenye vichwa vya habari kwa madai ya kumsaliti kimapenzi mke wake Nnalongo Maggie baada ya kudumu kwenye ndoa kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu. Rabadaba ambaye alihamia nchini Uingereza kukaa na Maggie baada ya kuhalalisha ndoa yao,  juzi kati mrembo huyo alijitokeza na kudai kuwa msanii huyo alimtumia vibaya kwa ajili ya kupata visa ya kwenda uingereza na baadae akamkimbia.

Read More
 Rabadaba kutimuliwa nchini Uingereza kwa kukiuka sheria za uhamiaji

Rabadaba kutimuliwa nchini Uingereza kwa kukiuka sheria za uhamiaji

Sakata la ndoa ya msanii Rabadaba limechukua sura mpya baaada ya mke wake Maggie kutishia kutumia nguvu kumrejesha nchini kwao Uganda kwa kile alichokitaja kuwa mwanamuziki huyo alitumia njia ya magendo kuhamia nchini uingereeza. Kwenye sauti inayosambaa mtandaoni Mrembo huyo amesema Rabadaba hakuwa na upendo wa kweli kwake kwani lengo lake kuu ilikuwa kutumia ndoa yao kujipatia uraia wa nchi ya Uingereza bila kuzingatia sheria za uhamiaji. Aidha Maggie ambaye kipindi cha nyuma alikuwa kwenye mahusiano na marehemu AK47, amesema kwa sasa wakili wake ameanza kulifanyia kazi suala la kumhamisha Rabadaba nchini kwao Uganda kwa kuwa hatomvulia kwa jinsi alivyomsaliti kimapenzi. Utakumbuka mwaka 2021 Rabadaba na Maggie walihalalisha mahusiano yao kwa umma na kisha baadae wakahamia jijini London Uingereza ambako wanaishi kwa sasa lakini ndoa yao inasemekana imevunjika kwa madai ya usaliti.

Read More
 RABADABA AFUNGUKA KUHUSU GHARAMA YA KUANDAA VIDEO ZA MUZIKI UGANDA

RABADABA AFUNGUKA KUHUSU GHARAMA YA KUANDAA VIDEO ZA MUZIKI UGANDA

Mwanamuziki wa Dancehall kutoka nchini Uganda Rabadaba anasema gharama ya kuaandaa video nchini Uingereza ni nafuu sana ikilinganishwa na Uganda. Katika mahojiano yake hivi karibuni Rabadaba Anasema waongozaji wa video nchini Uganda wanatoza wasanii pesa nyingi lakini wanashindwa kutayarisha video zenye ubora. “Utayarishaji wa video ni wa bei nafuu zaidi London ikilinganishwa na Uganda. Huko nyumbani, wakurugenzi wanadai pesa nyingi lakini wanazalisha kazi duni. Hapa London, kazi bora hutolewa kwa bei nafuu,” anaelezea katika mahojiano. Rabadaba amekuwa akiishi London kwa zaidi ya mwaka mmoja na juzi kati aliachia video mpya ya wimbo wake uoitwa “Ffe Banene” ambayo ilitayarishwa na kuelekezwa jijini London. Rabadaba alipata umaarufu mwaka wa 2009 baada ya kuachia wimbo wake uitwao ‘Bwekiri’. Na Ability akishirikiana na wasanii wa Goodlyfe.

Read More