Rapudo Amkingia Kifua Amber Ray Kufuatia Kashfa ya Obinna

Rapudo Amkingia Kifua Amber Ray Kufuatia Kashfa ya Obinna

Mfanyabiashara maarufu na mume wa sosholaiti Amber Ray,Kennedy Rapudo, amejitokeza hadharani kumtetea mkewe dhidi ya tuhuma alizoelekezewa na mwanahabari na mchekeshaji Oga Obinna. Kupitia video iliyosambazwa mitandaoni, Rapudo alieleza kutoridhishwa na jinsi Obinna alivyomkosoa Amber Ray hadharani. Rapudo alisema kuwa mke wake ni mwanamke anayejiheshimu na mchapakazi wa kweli, na kwamba hatakubali mtu yeyote kumvunjia heshima kwa misingi ya binafsi au ya kikazi. “Amber ni mke wangu na najua jinsi anavyojituma. Mtu yeyote anayemjua anajua kuwa anajiheshimu. Sitakubali mtu yeyote kumchafua hadharani,” alisema Rapudo kwa msisitizo. Kauli ya Rapudo ilikuja saa chache baada ya Oga Obinna kudai kuwa Amber Ray alifika kwenye shughuli ya kurekodi maadhui akiwa katika hali isiyofaa, akimtuhumu kuwa alikuwa amelewa kiasi na hivyo kuathiri utaratibu wa kazi. Obinna alidai kuwa hali hiyo ilisababisha ucheleweshaji na sintofahamu kazini. Amber Ray, kwa upande wake, alikanusha madai hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiyataja kama ya uongo na yenye lengo la kumharibia jina. Alisisitiza kuwa anajiheshimu na hajawahi kwenda kazini akiwa katika hali isiyo ya kitaaluma. Mvutano huu umeibua maoni tofauti miongoni mwa mashabiki wa burudani, huku baadhi wakiunga mkono msimamo wa Rapudo na Amber, na wengine wakitaka Obinna kutoa ushahidi wa madai yake au kuomba msamaha

Read More
 Amber Ray Aonekana na Rapudo Licha ya Tetezi za Kuvunjika kwa Ndoa

Amber Ray Aonekana na Rapudo Licha ya Tetezi za Kuvunjika kwa Ndoa

Sosholaiti maarufu wa Kenya, Amber Ray, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kushiriki video akiwa na mumewe Kennedy Rapudo, siku chache tu baada ya Rapudo kufuta akaunti yake ya Instagram, jambo lililoibua uvumi kwamba huenda kuna misukosuko katika ndoa yao. Katika video hiyo fupi iliyopakiwa kwenye Instagram Stories ya Amber Ray, wawili hao wanaonekana wakifurahia muda wao pamoja kwa bashasha, hali iliyotafsiriwa na wengi kama ishara kwamba huenda mambo bado ni shwari baina yao. Hapo awali, mashabiki walikuwa wameshtushwa na hatua ya Rapudo kujiondoa ghafla Instagram bila maelezo, hali iliyochochea maswali mengi mitandaoni. Hii si mara ya kwanza kwa wanandoa hao kujipata katikati ya minong’ono ya mitandaoni kuhusu uhusiano wao. Katika nyakati tofauti, wamekuwa wakiweka wazi maisha yao ya kifahari na familia, lakini pia hawajakosa migogoro ya hadharani ambayo huwavuta zaidi kwenye macho ya umma. Hadi sasa, Kennedy Rapudo hajarejesha akaunti yake ya Instagram, wala wawili hao hawajatoa tamko rasmi kuhusu kilichotokea. Hata hivyo, video hiyo imeonekana kuwatoa wasiwasi baadhi ya mashabiki waliokuwa na hofu kuhusu mustakabali wa ndoa yao. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu kuona iwapo kutakuwa na maelezo zaidi au hatua nyingine kutoka kwa wawili hao maarufu mitandaoni.

Read More