PSG Yaitandika Real Madrid 4-0, Yatinga Fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu

PSG Yaitandika Real Madrid 4-0, Yatinga Fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) imeendeleza ubabe wake katika soka la kimataifa kwa kuifunga Real Madrid mabao 4-0 na kufuzu kwa fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu. Mechi hiyo ya kusisimua ilichezwa Jumatano usiku mjini New Jersey, Marekani. PSG walitawala mchezo huo tangu dakika za awali, huku Fabián Ruiz akifungua ukurasa wa mabao katika dakika ya 6, kabla ya Ousmane Dembélé kuongeza bao la pili dakika tatu baadaye. Ruiz alipachika bao la tatu dakika ya 24 kabla ya Gonçalo Ramos kukamilisha karamu hiyo ya mabao dakika ya 87. Real Madrid walionekana kuzidiwa mapema kabisa kwenye mchezo huo, wakiwa na umiliki wa mpira wa asilimia 28 tu katika kipindi cha kwanza. Mashabiki na wachambuzi wa soka wameelezea matokeo haya kama aibu kubwa kwa mabingwa hao wa kihistoria, huku makosa ya kocha mpya Xabi Alonso yakitajwa kama sababu mojawapo ya kipigo hicho. Ushindi huo unaiweka PSG katika nafasi ya kukutana na Chelsea katika fainali siku ya Jumapili, mechi inayotarajiwa kuwa ya kukata na shoka. Huu ni mwendelezo wa mafanikio kwa PSG, waliotwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya majuma machache yaliyopita kwa kuicharaza Inter Milan mabao 5-0 katika fainali iliyochezwa Mei 31, 2025. Timu hiyo kutoka Ufaransa sasa inaonekana kuwa na kiu ya kutwaa taji la dunia la vilabu na kukamilisha msimu kwa mafanikio ya kihistoria. Mashabiki wa soka duniani kote sasa wanasubiri kwa hamu kuona kama PSG wataendeleza moto wao huo dhidi ya Chelsea na kutwaa Kombe la Dunia la Vilabu kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo.

Read More
 Real Madrid Yamtambulisha Rasmi Xabi Alonso Kuwa Kocha Mpya

Real Madrid Yamtambulisha Rasmi Xabi Alonso Kuwa Kocha Mpya

Klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania imemtambulisha rasmi Xabi Alonso kuwa kocha mpya wa kikosi hicho, ambapo ataanza kazi yake kuanzia msimu wa 2025/2026. Alonso amesaini mkataba wa miaka mitatu ambao utamuweka klabuni hadi mwaka 2028. Xabi Alonso mwenye umri wa miaka 43 anarejea tena Real Madrid, safari hii kama kocha, baada ya kuichezea timu hiyo kati ya mwaka 2009 hadi 2014. Akiwa mchezaji wa Real Madrid, alishinda mataji mbalimbali kabla ya kuhamia klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani. Uongozi wa Real Madrid umeeleza kuwa unamatumaini makubwa kwa Alonso kutokana na mafanikio aliyoyapata akiwa kocha wa Bayer Leverkusen, ambapo alionyesha uwezo mkubwa wa kiufundi. Mashabiki wa Real Madrid sasa wanatarajia kuona mafanikio mapya chini ya uongozi wa nyota wao wa zamani

Read More
 Real Madrid Waagana na Luka Modric Baada ya Miaka 13 ya Mafanikio

Real Madrid Waagana na Luka Modric Baada ya Miaka 13 ya Mafanikio

Klabu ya Real Madrid jana imeaga rasmi kiungo wao nyota Luka Modric, baada ya kulitumikia kikosi hicho kwa miaka 13. Modric alijiunga na Madrid mwaka 2012 akitokea Tottenham Hotspur ya England, na tangu wakati huo amekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Los Blancos. Miongoni mwa mafanikio makubwa ya Modric akiwa Madrid ni pamoja na kutwaa Ballon d’Or mwaka 2018, na kushinda mataji sita ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League). Mchango wake katika safu ya kiungo umeisaidia Madrid kutawala soka la Ulaya kwa kipindi kirefu. Modric pia anasifika kwa uongozi, nidhamu, na ustadi wa hali ya juu ndani ya uwanja, akiwa mfano bora kwa wachezaji chipukizi. Kuondoka kwake kumeacha pengo kubwa lakini pia kumbukumbu ya mafanikio ya kipekee katika historia ya klabu hiyo. Katika mechi ya mwisho ya msimu, Real Madrid waliibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Real Sociedad, ambapo mashabiki walimshangilia Modric kwa heshima kubwa, wakimpa kwaheri ya kipekee kwa mchango wake mkubwa kwa miaka yote aliyovaa jezi nyeupe ya Madrid.

Read More