RICH MAVOKO AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA
Msanii wa Bongofleva Rich Mavoko ameachia rasmi albamu yake mpya iitwayo “Fundi” na tayari inapatikana kupitia majukwaa yote ya ku-stream muziki mtandaoni. Albamu hiyo yenye jumla ya ngoma 16, ina kolabo 7 pekee, akiwa amewapa mashavu wasanii kama Fid Q, Masauti, Saraphina, , Hart the band, Big Zulu na Ssaru. Hii inakuwa ni albamu ya kwanza kwa mtu mzima Rich Mavoko tangu aanze muziki wake kando na EP yake iitwayo Rich Mavoko minitape ambayo aliingia sokoni Agosti mwaka wa 2020.
Read More