Rose Muhando ashinda tuzo mbili za kimataifa Australia

Rose Muhando ashinda tuzo mbili za kimataifa Australia

Baada ya Malkia wa muziki wa injili Tanzania Mtumishi wa Mungu Rose Muhando kufunga mwaka 2022 kibabe kwa kutoa Album yake iitwayo Secret Agenda ambayo hadi hivi sasa imepata mapokezi makubwa mnoo kwa wadau na wapenzi wa muziki wa injili. Sasa mwaka 2023 pia Mungu ameendelea kuwa upande wake kwa kufungua mwaka kwa kupata Tuzo mbili kubwa na za kimataifa zinazoitwa RSW AWARDS Tuzo hizo zinazotolewa huko Australia. Rose Muhando  ameshinda Tuzo mbili kupitia kipengele cha African Female Gospel Vocalist pamoja na kipengele cha African Gospel collaboration, Tuzo hizi zimepangwa kutolewa huko Australia in Adelaide, South AUSTRALIA on 18th Februari 2023.

Read More
 ROSE MUHANDO AKANUSHA TUHUMA ZA KUTOKA KIMAPENZI NA LORD MUTAI

ROSE MUHANDO AKANUSHA TUHUMA ZA KUTOKA KIMAPENZI NA LORD MUTAI

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka nchini Tanzania Rose Muhando amejitenga na tuhuma za kutoka kimapenzi na mwanablogu mwenye utata nchini Lord Mutai. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Rose Muhando amekanusha madai hayo kwa kusema kwamba hayana msingi wowote ikizingatiwa kuwa hamfahamu kabisa Lord Mutai. Kauli Rose Muhando imekuja mara baada ya mtumiaji mmoja wa mtandao wa Twitter kwa jina la Bookten kudai kuwa hitmaker huyo wa ngoma ya  “Nibebe” aliwahi kutoka kimapenzi na mwanablogu maarufu wa Twitter nchini Kenya Lord Mutai huko mjini Thika kwenye moja ya Hoteli aliyokuwa akifanya kazi. Bookten alienda mbali zaidi na kusema kwamba alimfumania Lord Mutai akimsindikiza Rose Muhando hadi kwenye chumba kimoja cha hoteli hiyo ambapo walilala hadi asubuhi. Hata hivyo baada ya taarifa hiyo kuzua gumzo mitandaoni Lord Mutai aliibuka na kujitenga na madai hayo kwa kusema kuwa hajawahi kutoka kimapenzi  na Rose Muhando katika hoteli yoyote mjini Thika ambapo alienda mbali zaidi na kutishia kumfungulia mashtaka Bookten kwa hatua ya kumpaka tope.    

Read More
 MR T AKIRI KUMUOMBA MSAMAHA MSANII WA NYIMBO ZA INJILI ROSE MUHANDO BAADA YA KUMVUNJIA HESHIMA 2021

MR T AKIRI KUMUOMBA MSAMAHA MSANII WA NYIMBO ZA INJILI ROSE MUHANDO BAADA YA KUMVUNJIA HESHIMA 2021

Mwanamuziki wa injili aliyegeukia ukasisi kutoka nchini Kenya Mr. T amekiri kumuomba msamaha msanii wa nyimbo za injili nchini Tanzania Rose Muhando baada ya kumvunjia heshima mwaka wa 2021. Kwenye mahojiano na mpasho Mr. T  amesema alichukua maamuzi hayo baada ya watu kumshambulia kwenye mitandao ya kijamii ambapo amedai kwamba hakuwa na nia ya kumharibia jina Rose Muhando ila alikuwa anatoa mfano kwa wakristo. Hitmaker huyo wa ngoma ya Finje Finje amesema hana ugomvi wowote na  Rose Muhando akizingatiwa kuwa amekuwa akimtakia mema kwenye harakati za kuupeleka muziki wake kwenye hatua nyingine. Mr. T aligonga vichwa vya habari nchini Kenya mara baada ya kumtolea uvivu Rose Muhando kwenye moja ya ibada yake ya kanisani kwa kusema kwamba anguko la Rose Muhando kimuziki lilikuja kufuatia hatua yake kujiunga na lebo ya muziki Sony Music. Hata hivyo mashabiki wengi wa muziki wa injili Afrika Mashariki  hawakufurahishwa na matamashi ya Mr. T jambo ambalo lilimlazimu Rose Muhando kujitokeza na kumsuta  vikali kasisi huyo kwa kumharibia chapa yake ya muziki ambayo ameitengeneza kwa miaka nyingi.      

Read More
 ROSE MUHANDO ATUHUMIWA KUTOKA KIMAPENZI NA MWANABLOGU MAARUFU NCHINI KENYA LORD MUTAI

ROSE MUHANDO ATUHUMIWA KUTOKA KIMAPENZI NA MWANABLOGU MAARUFU NCHINI KENYA LORD MUTAI

Msanii mashuhuri wa nyimbo za injili nchini Tanzania rose Muhando ameusimamisha mtandao wa Twitter kwa Jina lake kukaa kwenye orodha ya ‘Topics’ ambazo zinazungumzwa zaidi kwenye mtandao huo nchini Kenya. Hii ni baada ya mtumiaji mmoja wa mtandao wa Twitter kwa jina la bookten kudai hitmaker huyo wa ngoma ya  “Nibebe” aliwahi kutoka kimapenzi na mwanablogu maarufu wa Twitter Lord Mutai. Kulingana na Bookten aliwahi kufanya kazi kama mpokea wageni katika eneo la burudani liitwalo Club Image mjini Thika na alimuona Lord mutai akimsindikiza rose muhando hadi kwenye chumba cha hoteli katika klabu hiyo. Booktena alienda mbali zaidi na kudai kuwa bwana mutai alilala na rose muhando kwenye chumba hicho hadi asubuhi akihoji kuwa walishiriki tendo la ndoa. Hata hivyo bwana mutai amejitenga na madai hayo akisema kuwa hajawahi kutoka kimapenzi  na rose Muhando katika hoteli yoyote mjini Thika. Mutai amesema mawakili wake kwa sasa wako kwenye harakati ya kufuatilia shutuma zilizoibuliwa dhidi yake na Bookten.

Read More