S2Kizzy Atoa Msaada kwa Prodyuza Bakteria Aliyepooza Baada ya Kushambuliwa

S2Kizzy Atoa Msaada kwa Prodyuza Bakteria Aliyepooza Baada ya Kushambuliwa

Mtayarishaji wa muziki kutoka Tanzania, S2Kizzy maarufu Zombie, ameonyesha moyo wa utu baada ya kumtembelea na kumpa msaada prodyuza mwenzake aitwaye Bakteria, ambaye kwa miaka miwili sasa amekuwa akikabiliwa na changamoto kubwa ya kiafya. Katika ziara yake, S2Kizzy alimpelekea msaada wa vyakula na mahitaji ya nyumbani, huku akisisitiza kuwa Bakteria alikuwa tegemeo kubwa kwa familia yake kupitia kazi za muziki, lakini sasa hali ngumu imemlazimisha kusimama. Ameongeza kuwa ni muhimu jamii iungane na kusimama pamoja na wale wanaopitia changamoto. Zombie ametoa wito kwa mashabiki na watu wenye nia njema kushirikiana na kusaidia familia hiyo kupitia namba 0714 315 680. Bakteria alipata matatizo ya kupooza na kushindwa kutembea kufuatia shambulio la vibaka karibu na studio yake mjini Tanga, jambo lililosimamisha kabisa ndoto zake za muziki. Kwa sasa, Bakteria anaishi na mama yake mzazi ambaye pia anakabiliwa na matatizo ya kiafya, hali inayoongeza ugumu wa maisha yao.

Read More
 S2kizzy Awahimiza Maprodyuza Kuwa Wajasiri Katika Muziki

S2kizzy Awahimiza Maprodyuza Kuwa Wajasiri Katika Muziki

Prodyuza wa muziki kutoka Tanzania, S2kizzy, amewashauri maprodyuza wenzake kutoogopa kufanya aina yoyote ya muziki kwa kuhofia maneno ya watu. Kwa mujibu wa S2kizzy, muziki ni sanaa ya burudani na furaha, hivyo kila prodyuza ana nafasi ya kujaribu mitindo na miondoko mbalimbali ili kuleta furaha na burudani kwa jamii. S2kizzy, ambaye amehusishwa na kutengeneza hit singles nyingi za wasanii wakubwa Afrika Mashariki, amesisitiza kuwa ubunifu na kujiamini katika kazi ndiyo msingi wa mafanikio katika tasnia ya muziki ambayo imejaa ushindani mkubwa. Ujumbe huu umetafsiriwa kama motisha kwa vijana wengi wanaojitahidi kuingia kwenye muziki lakini hukumbwa na hofu ya mitazamo ya watu

Read More
 S2kizzy Ajiita Profesa wa Muziki, Awahimiza  Beatmakers Kujiamini Zaidi

S2kizzy Ajiita Profesa wa Muziki, Awahimiza Beatmakers Kujiamini Zaidi

Mtayarishaji wa muziki kutoka Tanzania, S2kizzy maarufu Zombie, ameweka wazi mtazamo wake kuhusu nafasi ya beatmaker katika tasnia ya muziki. Akipiga stori na The Throne, Zombie anasema hakuna haja mtu yeyote kujisikia vibaya akiitwa beatmaker kwa sababu hiyo ndiyo nguzo muhimu inayoshikilia mchakato mzima wa utayarishaji muziki. Kwa maelezo yake, kutengeneza beat ndiko kunakoipa ngoma uhai kabla ya hatua nyingine za uzalishaji kuingia. Hata hivyo, anasisitiza kuwa safari yake ya kimuziki imemfikisha mbali zaidi ya hatua hiyo, na sasa anajitazama kama profesa wa muziki kutokana na uwezo wake mpana unaojumuisha kuunda beat, kufanya production, kutoa mwongozo na kupanga mashairi. S2kizzy, ambaye amefanya kazi na wasanii wakubwa wa Afrika Mashariki na kimataifa akiwemo Diamond Platnumz, Rayvanny na Harmonize, amekuwa akihusishwa na mageuzi makubwa kwenye sauti ya Bongofleva na kuisukuma kuvuka mipaka ya kanda. Wachambuzi wa muziki wanasema matamshi yake yanaonyesha namna tasnia inavyoendelea kukua na kuhitaji wataalamu wenye ujuzi mpana zaidi ya kutengeneza beat pekee, kwani muziki wa kisasa unahitaji ubunifu, usimamizi wa kiufundi na mtazamo wa kimataifa.

Read More
 S2kizzy Amporomoshea Matusi Hussen Machozi

S2kizzy Amporomoshea Matusi Hussen Machozi

Mtayarishaji wa muziki wa Bongo Fleva, S2kizzy, ameimtolea maneno makali mwanamuziki Hussen Machozi, akimuita mpumbavu. Akipiga stori na East Africa Radio, mtayarishaji huyo amesema hana sababu ya kushirikiana naye kimuziki ikizingatiwa kuwa nyimbo zake zimepitwa na wakati. S2kizzy anayejulikana kwa jina la utani Zombie amemchana vikali Machozi na kutamka wazi kuwa hamheshimu huku akimshauri msanii huyo kutafuta njia nyingine za kuendeleza muziki wake. Kauli ya S2kizzy imeibuka kufuatia madai ya Hussen Machozi, aliyelalamika kuwa mtayarishaji huyo hajawahi pokea simu zake licha ya kujitambulisha kwake mapema. Hussen alienda mbali zaidi na kuhoji kuwa juhudi zake za kuwasiliana na S2kizzy zimekuwa zikigonga mwamba, jambo lililomfanya kulalamikia kutothaminiwa.

Read More
 Jux Atoa EP Maalum Kuelezea Safari Yake ya Mapenzi na Mkewe Priscy

Jux Atoa EP Maalum Kuelezea Safari Yake ya Mapenzi na Mkewe Priscy

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Juma Jux, ameachia rasmi kazi yake mpya ya muziki, EP iitwayo “A Day To Remember”, kama kumbukizi maalum ya ndoa yake na mkewe mpendwa, Priscy. Kupitia mitandao ya kijamii, Jux ameeleza kuwa mradi huu si kazi ya kawaida, bali ni simulizi ya maisha yao ya upendo, kuanzia mwanzo wa safari yao ya mahaba hadi furaha waliyonayo sasa kama wanandoa. EP hiyo imejaa hisia, utamaduni na usanii wa hali ya juu, ikiwa imeshirikisha mastaa wawili wakubwa: Phyno kutoka Nigeria na D Voice kutoka Tanzania. Jux ameamua kuunganisha ladha ya Afrika Mashariki na Magharibi ili kuwasilisha ujumbe wa upendo unaovuka mipaka ya lugha na mataifa. Kati ya watayarishaji walioweka mikono yao kwenye kazi hii ni S2kizzy, Foxx Made It, na Aykbeats, huku kazi ya mixing na mastering ikifanywa na Lizer Classic, jina kubwa katika ubora wa sauti Afrika. Katika ujumbe wake, Jux hakusita kumshukuru mkewe Priscy kwa kuwa chanzo cha msukumo wa EP hii, pamoja na familia yake, timu nzima ya wasanii na wahusika waliounga mkono kazi hiyo, na mashabiki waliomfuatilia kwa miaka mingi. Amesisitiza kuwa baada ya harusi yao rasmi, atatoa wimbo wa kipekee kama zawadi ya kufunga sura hii mpya ya maisha. EP “A Day To Remember” itapatikana kuanzia usiku wa leo kwenye majukwaa yote ya kidijitali ya kusikiliza muziki. Mashabiki tayari wameonyesha hamasa kubwa, wakisubiri kwa shauku kusikia mchanganyiko wa upendo na sanaa katika kazi hii ya kipekee.

Read More
 Prodyuza kutoka Tanzania S2kizzy ashirikishwa kwenye Album ya Black Eyed Peas “Elevation”

Prodyuza kutoka Tanzania S2kizzy ashirikishwa kwenye Album ya Black Eyed Peas “Elevation”

Mtayarishaji wa Tanzania S2kizzy ameshiriki kwenye kuitayarisha Album mpya ya Kundi maarufu la Muziki duniani Black Eyed Peas “Elevation” ambayo imetoka rasmi wiki hii. Zombie ameshiriki kutayarisha wimbo namba 9 kwenye Album hiyo uitwao “Filipina Queen” ambao ameshirikishwa mwanadada Bella Poarch. Kwenye Album hiyo yenye vyuma 15, Black Eyed Peas wamewapa mashavu wakali wa dunia kama Shakira, Ozuna, David Guetta, Daddy Yankee na wengine. Kundi hilo linaundwa na wasanii wanne akiwemo William James Adams Jr, Allan Pineda Lindo (apl.de.ap), Jaime Luis Gomez (Taboo) na J. Rey Soul. Kundi hilo lilifanikiwa kuitikisa dunia na Hit single yao “Where Is The Love” mwaka 2003.

Read More
 MAPRODYUZA WA BONGOFLEVA S2KIZZY NA BLACQ WATOFAUTIA KIMAWAZO KUHUSU SUALA LA MIRAHABA

MAPRODYUZA WA BONGOFLEVA S2KIZZY NA BLACQ WATOFAUTIA KIMAWAZO KUHUSU SUALA LA MIRAHABA

Watayarishaji wawili wa muziki kutoka nchini Tanzania Blacq Beatz na S2kizzy wameonekana kutofautiana katika mtazamo wa maprodyuza kutohusika katika mgao wa mirabaha ya muziki iliyotolewa usiku wa kuamkia Januari 29. Hili limekuja baada ya Chama cha Hakimiliki Tanzania COSOTA kwa kushirikiana na wizara ya sanaa kutoa sehemu ya fedha zilizopatikana kwenye kazi za wanamuziki {mirabaha} huku watayarishaji wa muziki wa Bongofleva wakisahaulika kwenye orodha hiyo. S2kizzy ameonekana kutofurahishwa na jambo hilo huku Blacq akijibu kuwa jambo hilo limetokana na wao kama maprodyuza kutojua thamani na haki yao, ambapo amesema maprodyuza wa Bongofleva waendelee kusubiri kusaidiwa na wasanii.

Read More