Sam West awataka watu kutoingilia mahusiano yake na Vivian

Sam West awataka watu kutoingilia mahusiano yake na Vivian

Siku moja baada ya Sam West kuthibitisha kuwa mahusiano yake na mwimbaji Vivian yameingiwa na ukungu, sasa mchekeshaji huyo ambaye anasusua kisanaa nchini ameibuka na mpya. Kupitia mitandao ya kijamii Sam West amewataka watu kutoingilia sana sakata la ndoa yake na Vivian kuvunjika kwani huenda wakabaki njia panda ikitokea wamefufua tena penzi lao. “Methali: Mambo ya watu wawili waliopendana usiyaingilie, utaachwa katikati wakirudiana.” Ameandika Instagram. Ujumbe huo umetafsiriwa na walimwengu kuwa huenda ni kiki ya ujio mpya wa Vivian kimuziki ambapo amewataka wawili hao kuachia wimbo huo mara moja badala ya kudanganya umma kuwa jini mkata kamba ameingilia mahusiano yao. Sam West na mke wake Vivian wamekuwa gumzo mtandaoni baada ya taarifa kuibuka kuwa wawili hao wamebwaga manyanga. Utakumbuka Vivian ndiye alikuwa wa kwanza kuweka wazi kuwa anapitia wakati mgumu akitaka mashabiki wamweke kwa maombi baada ya mume wake kumkimbia licha ya kujaribu kutatua tofauti zao. Haikushia hapo Sam West pia alitumia mitandao yake kijamii kudokeza kuwa ndoa yake imefikia mwisho kwa kile alichokitaja kutoelewana kati yake na mke wake Vivian.

Read More
 Sam West athibitisha kuvunja kwa ndoa yake na Vivian

Sam West athibitisha kuvunja kwa ndoa yake na Vivian

Sam West amethibitisha kuvunjika kwa mahusiano yake na mwimbaji Vivian baada ya kudumu kwenye ndoa kwa muda wa takriban miaka sita. Kupitia ujumbe wa mafumbo aliouchapisha kwenye mtandao wa Instagram Sam West aamesema ameamua kuachana na mwimbaji huyo kwa sababu ambazo zipo nje ya uwezo wake kwani angendelea kubaki kwenye mahusiano hayo huenda angepoteza maisha yake kutokana na msongo wa mawazo. Kauli ya Sam West inakuja baada ya Vivian kuweka wazi kuwa anapitia kipindi kigumu katika maisha kufuatia mume wake kumkimbia ambapo alienda mbali zaidi na kuwataka mashabiki wamweke kwa maombi kutokana na jini mkata kamba kuingilia mahusiano yake. Hata hivyo mashabiki walitilia shaka taarifa za mrembo huyo kuachana na mume wake Sam West wengi wakihoji kuwa huenda anatafuta njia ya kuteka hisia zao kwa ajili ya ujio wa ngoma yake mpya. Utakumbuka wawili hao wamekuwa pamoja tangu mwaka wa 2016 baada ya Sam West kumvisha pete ya uchumba Vivian mubashara kwenye kipindi cha runinga ambapo mwaka wa 2018 walihalalisha mahusiano yao kwa njia ya harusi ya kitamaduni.

Read More