Rapa Diddy Kusomewa Hukumu Oktoba 3 kwa Kesi ya Ukahaba

Rapa Diddy Kusomewa Hukumu Oktoba 3 kwa Kesi ya Ukahaba

Rapa na mfanyabiashara maarufu wa Marekani, Sean Combs almaarufu Diddy, amepangiwa rasmi tarehe ya kusomewa hukumu yake kuhusiana na makosa ya biashara ya ukahaba. Jaji Arun Subramanian ametangaza kuwa hukumu hiyo itasomwa Oktoba 3 mwaka huu, ikiwa ni siku ile ile aliyopendekeza wiki iliyopita mara baada ya Diddy kupatikana na hatia kwa makosa mawili makuu yanayohusiana na kusafirisha watu kwa lengo la kujihusisha na ngono. Kulingana na vyanzo vya mahakama, Diddy atasalia kizuizini hadi siku hiyo ya hukumu, hali inayomaanisha kuwa atakuwa amekaa gerezani kwa zaidi ya mwaka mmoja kufikia wakati huo. Muda aliokaa rumande unatarajiwa kuzingatiwa katika uamuzi wa mwisho wa kifungo chake. Hii inakuwa hatua nyingine kubwa katika sakata linalomkumba Diddy, ambaye kwa miaka mingi amekuwa mmoja wa majina makubwa katika tasnia ya burudani Marekani. Wadau mbalimbali wa muziki na mashabiki wake wameendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa kesi hii inayotikisa vichwa vya habari kimataifa.

Read More
 Mahakama Yatoa Uamuzi Mpya Kesi ya Diddy, Shtaka Kubwa Linasubiriwa

Mahakama Yatoa Uamuzi Mpya Kesi ya Diddy, Shtaka Kubwa Linasubiriwa

Mwanamuziki na mfanyabiashara maarufu wa Marekani, Sean “Diddy” Combs, amepatikana na hatia ya kosa la ukahaba haramu lakini amesafishwa mashtaka mazito zaidi ya biashara haramu ya ngono (sex-trafficking) na uhalifu wa kupanga (racketeering), ambayo yangemuweka gerezani maisha. Kufuatia hukumu hiyo, mchakato wa kutoa adhabu rasmi umekamilika na sasa unatarajiwa kutangazwa rasmi hivi karibuni. Diddy anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 jela kwa kosa hilo la ukahaba haramu. Wanasheria wake wameshikilia kuwa anapaswa kuachiliwa kwa dhamana akisubiri kusikilizwa kwa hukumu yake rasmi, wakisisitiza kuwa hana historia ya kukimbia kesi. Hata hivyo, upande wa mashtaka unapinga vikali ombi hilo, ukionya kuwa Diddy ana ushawishi mkubwa wa kifedha na kijamii unaoweza kutumiwa kuingilia mchakato wa haki. Kesi hii imeibua mjadala mkubwa duniani kuhusu matumizi mabaya ya mamlaka, ushawishi wa mastaa katika vyombo vya sheria, na mapambano dhidi ya unyanyasaji wa kingono.

Read More
 Ushahidi wa Kid Cudi Dhidi ya Diddy Wamvunja Moyo Kanye West

Ushahidi wa Kid Cudi Dhidi ya Diddy Wamvunja Moyo Kanye West

Rapa maarufu mwenye utata, Kanye West, ametoa hisia zake kuhusu hali inayoendelea kumkumba Sean Diddy Combs, akieleza masikitiko yake juu ya hatua ya Kid Cudi kutoa ushahidi dhidi ya Diddy. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Ye ameonekana kuzungumzia kile anachokiona kama mfumo wa haki unaowakandamiza watu weusi, akisisitiza haja ya jamii ya wasanii na Wamarekani Weusi kwa ujumla kujilinda na kushikamana badala ya kushirikiana na mifumo anayoamini kuwa ya kibaguzi. “I wish Cudi hadn’t testified against Puff. We need to not be locked in white systems. Praying for Puff and his family. Praying for Puff Daddy and the Family.”Aliandika X Kauli hiyo imeibua hisia mseto kutoka kwa mashabiki na wanamuziki wenzake, huku baadhi wakimtetea kwa msimamo wake wa kutaka mshikamano miongoni mwa wasanii wa asili ya Kiafrika, na wengine wakimkosoa kwa kudharau mchakato wa haki. Kid Cudi, ambaye zamani alikuwa rafiki wa karibu wa Ye, anatajwa kuwa miongoni mwa mashahidi waliotoa ushahidi dhidi ya Diddy kufuatia madai mazito yanayomkabili kuhusu vitendo vya unyanyasaji na ukiukaji wa haki.

Read More
 Watu Wanalipwa $50 kwa Saa Kuvaa T-Shirt za “Free Diddy”, Mwanamke Afichua Siri

Watu Wanalipwa $50 kwa Saa Kuvaa T-Shirt za “Free Diddy”, Mwanamke Afichua Siri

Taarifa mpya zimeibuka kuhusu watu waliokuwa wamevaa T-Shirt zenye maandishi “Free Diddy” nje ya mahakama, zikionesha kwamba si wote waliokuja kwa hiari yao. Mwanamke mmoja amefichua kuwa baadhi ya watu waliokuwa wamevalia T-Shirt hizo walikuwa wamelipwa hadi $50 kwa saa ili kushiriki katika kile kinachoonekana kuwa ni kampeni ya kumuunga mkono msanii maarufu, Diddy. Kwa mujibu wa vyanzo vya burudani nchini Marekani, mwanamke huyo alisema kuwa alikaribishwa kushiriki katika shughuli hiyo lakini alikataa kuvaa T-Shirt hizo licha ya kuahidiwa malipo ya $20 kwa saa mwanzoni, ambayo baadaye yaliripotiwa kuongezeka hadi $50 kwa saa kwa baadhi ya watu. “Nilijua siwezi kuvaa hiyo T-shirt. Siwezi kusimama nikimuunga mkono mtu ambaye sijui ukweli wake,” alisema mwanamke huyo. Kampeni ya Free Diddy imezua mjadala mkubwa mtandaoni, huku baadhi ya watu wakihisi kuwa inalenga kuonesha picha ya uungwaji mkono wa umma kwa Diddy wakati mashtaka dhidi yake bado yanaendelea kushughulikiwa mahakamani. Mpaka sasa, haijafahamika wazi ni nani aliyefadhili kampeni hiyo ya mavazi, lakini madai ya watu kulipwa kushiriki yamezua maswali kuhusu uhalisia na dhamira ya maandamano hayo ya kuunga mkono msanii huyo.

Read More