B Classic akiri kutamani penzi la mwanasholaiti maarufu mtandaoni Shakilla

B Classic akiri kutamani penzi la mwanasholaiti maarufu mtandaoni Shakilla

Msanii B Classic ameweka wazi matamanio ya kumchumbia mrembo maarufu mtandaoni nchini Kenya Shakilla kwa kigezo kuwa lazima awe mlokole. Kupitia instastoy yake amesema yuko tayari kuingia kwenye mahusiano na Shakilla huku akidai kuwa atafanya kila awezalo kuhakikisha kuwa mrembo huyo anafurahia maisha yake ya ndoa. “Shakila ! I have seen unataka kutoka soko – Niko soko pia and I can take you in. Na nikupe maisha poa Tu. Ila are you willing to change? I’ll cater for everything. Bora tu nione unakua church girl. Haijalishi it will take how long,” Aliandika Instastory. Kauli ya B Classic imekuja mara baada ya Shakilla kukiri hadharani kuwa hakuna shabiki yake anayetaka kuingia naye kwenye mahusiano ambayo yataishia kuwa ndoa. β€œSo outta all of my followers, no one wants to enter into a serious relationship with me. Was I meant to be in the streets for life?” aliandika Instastory. Ikumbukwe mwezi mmoja uliopita Shakilla alidai kuwa hatokuja kuchumbiana na wanaume wa Kenya ambapo alienda mbali zaidi na kuhoji kuwa heri atoke kimapenzi na wanaume wa Nigeria kutokana na ukarimu wao.

Read More
 Mchekeshaji Eric Omondi akanusha madai ya kutomlipa Shakilla

Mchekeshaji Eric Omondi akanusha madai ya kutomlipa Shakilla

Mchekeshaji Eric Omondi amekanusha madai ya kumtolipa Shoshalaiti maarufu mtandaoni Shakilla kwa kumshirikisha kwenye kipindi cha wife material. Kwenye mahojiano na Ankali Ray amesema wanawake wote walioshirikishwa kwenye kipindi hicho walilipwa shillingi Ksh. 18,000 kila mmoja akiwemo Shakilla pamoja na Cartoon Comedian. “Nililipa , I swear I paid her . Alilipwa 18 thousand …Shakilla alikua na tabia mbaya sana , alikua ananifuata kwa kila room ,… sijalala na mtu yote.”, Alisema. Kauli ya Omondi imekuja mara baada ya mrembo huyo kumshutumu kuwa alimtumia vibaya kwenye shughuli zake kwa manufaa yake binafsi bila kumlipa chochote. β€œEric amenitumia vibaya kwa njia nyingi sana. Hakunilipa wala mtu yeyote aliyeshiriki kipindi cha wife material,” Alisema.

Read More