Shakira aweka rekodi kwenye mtandao wa Youtube

Shakira aweka rekodi kwenye mtandao wa Youtube

Mwimbaji nyota duniani Shakira ameuanza mwaka 2023 kwa kuvunja rekodi ya muda wote ya mtandao wa Youtube hii ni kufuatia wimbo wake mpya uitwao “BZRP MUSIC SESSION 53” kuwa wimbo wa Ki-Latin uliotazamwa kwa muda mfupi zaidi katika mtandao huo tangu video itoke. Inaelezwa kuwa, video ya wimbo huo ilipata views Milioni 63 kwa saa 24 na pia ikapata views Milioni 125 ndani ya siku 4 pekee. Hiyo inatajwa kuwa ni rekodi ya aina yake. Wimbo huo ni Disstrack kwa Baba watoto wake Gerald Pique ambaye ni mchezaji mstaafu wa klabu ya Barcelona, wamebarikiwa watoto wawili nao ni Milan (9) na Shasha (7), na waliachana mwaka jana baada ya kuwa kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka 10.

Read More
 SHAKIRA AKABILIWA NA KESI YA KUKWEPA KULIPA KODI UHISPANIA

SHAKIRA AKABILIWA NA KESI YA KUKWEPA KULIPA KODI UHISPANIA

Mwimbaji kutoka Colombia, Shakira anakabiliwa na kesi nchini Uhispania kwa madai ya ulaghai wa kulipa kodi, kulingana na vyombo vya habari nchini humo. Waendesha mashtaka wa serikali wanadai Shakira alishindwa kulipa ushuru wa mapato ya kibinafsi na mali kati ya 2012-2014, ambayo kwa sasa ina thamani ya takriban dola milioni 15, madai ambayo ameyakanusha. Shakira alitaja mashtaka yake kuwa “uongo” katika mahojiano na jarida la Elle mapema mwezi huu, akisema “Nililipa kila kitu walichosema ninadaiwa, hata kabla ya kufungua kesi. Kwa hivyo hadi leo, nina deni la sifuri kwao.” Mamlaka za Uhispania zinadai nyota huyo aliishi nchini humo kwa muda wa siku 183 kila mwaka kati ya 2011 na 2014, lakini Shakira alikanusha madai hayo pia na kwa mujibu wa mawakili wake, makazi ya msingi ya staa huyo kwa wakati huo yalikuwa nchini Bahamas. Katika hatua nyingine, Jaji wa mahakama moja huko Barcelona inayoshughulika na shauri hilo, ameamuru kesi hiyo isogezwe mbele, licha ya kutoweka wazi tarehe ya kuanza kusikilizwa tena.

Read More
 SHAKIRA AKIRI KUMPENDA GERARD PIQUE LICHA YA NDOA YAO KUVUNJIKA

SHAKIRA AKIRI KUMPENDA GERARD PIQUE LICHA YA NDOA YAO KUVUNJIKA

Mwanamuziki Shakira bado anaumizwa na kuvunjika kwa penzi lake na Gerard Pique, ameripotiwa kukasirika baada ya kuona video ambayo inamuonesha nyota huyo wa Barcelona akidendeka na mpenzi mpya, binti wa miaka 23 anayeitwa Clara Chia Marti. Tovuti mbali mbali nchini Uhispania zinaripoti kwamba Shakira ameshikwa na gadhabu baada ya kumuona Pique ambaye waliachana mwezi June mwaka huu akionesha ushababi huo hadharani kinyume na makubaliano yao kwamba waheshimu faragha mbele ya watoto wao kwa angalau mwaka mmoja baada ya kuachana. Wawili hao waliachana kwa sababu za usaliti ambapo Shakira alidaiwa kumfumania Pique akiwa na mwanamke mwingine. Mrembo Clara Chia Marti anadaiwa kuwa Afisa Mahusiano kwenye kampuni ya Pique na penzi lao lilianza miezi kadhaa nyuma

Read More
 PENZI LA SHAKIRA NA GERALD PIQUE LAVUNJIKA RASMI

PENZI LA SHAKIRA NA GERALD PIQUE LAVUNJIKA RASMI

Mwanamuziki maarufu duniani Shakira amethibitisha kuachana na Gerard Piqué baada ya miaka 11 ya kuwa kwenye mahusiano. Timu yake ya mawasiliano imetoa taarifa rasmi kupitia mtandao wa Twitter ambapo imeandika “Tunasikitika kuthibitisha kwamba tumeachana rasmi. Kwa ustawi wa watoto wetu, ambao ndio kipaumbele chetu kikubwa zaidi, tunakuomba kwamba uheshimu faragha yao. Asante.” Sababu kuu iliyopelekea wawili hawa kuachana ni tuhuma za usaliti ambapo inadaiwa Shakira alimfumania Gerard Piqué akiwa na mwanamke mwingine. Utakumbuka kwa pamoja wamebarikiwa kupata watoto wawili wa Kiume.

Read More
 PENZI LA SHAKIRA NA PIQUE LAINGIWA NA UKUNGU

PENZI LA SHAKIRA NA PIQUE LAINGIWA NA UKUNGU

Mwanamuziki maarufu duniani Shakira anadaiwa kumfumania mumewe mchezaji staa wa Barcelona Gerard Piqué akiwa na mwanamke mwingine, hiyo imepelekea wawili hao kwa sasa kila mmoja kuishi kivyake huku penzi lao likiwa mbioni kuvunjika. Kwa mujibu wa Mwandishi wa Gazeti la El Periodico, Emilio Pérez de Rozas. Shakira na Pique walianza mahusiano mwaka 2011 baada ya kukutana kwenye video ya “Waka Waka (This Time for Africa)” mwaka 2010. Pamoja wana watoto wawili wa Kiume. Jarida la Forbes linawataja Shakira na Pique kwenye orodha yao ya Couples zenye nguvu zaidi duniani.

Read More