Spice Diana Amshambulia Sheebah, Adai Analipa Wanablogu Kumchafua

Spice Diana Amshambulia Sheebah, Adai Analipa Wanablogu Kumchafua

Msanii nyota wa muziki nchini Uganda, Spice Diana, ameendeleza mashambulizi ya maneno dhidi ya msanii mwenzake Sheebah Karungi, akimtuhumu kuwalipa wanablogu na baadhi ya watu kutoka kwenye timu yake ili kusambaza taarifa za kumchafua mtandaoni. Akizungumza katika mahojiano na kituo cha runinga nchini Uganda, Spice Diana alisema kuwa Sheebah mara nyingi hujikita kumzungumzia kila anapopata nafasi, jambo ambalo kwa upande wake anadai halimsumbui. Spice Diana amesema kuwa hatua ya kum-unfollow Sheebah kwenye Instagram ilitokana na kile alichokiona kama tabia za kimaslahi binafsi na zisizo za ukweli. Alieleza kuwa badala ya kushughulikia masuala yao binafsi kwa njia ya moja kwa moja, Sheebah alichagua kuchapisha ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, hali iliyomfanya apoteze imani naye. Kwa upande wake, Sheebah Karungi, kupitia mkutano na wanahabari uliofanyika wiki iliyopita, alikanusha madai ya kumshambulia Spice Diana au kulipa wanablogu waandike habari mbaya kumhusu, akieleza kuwa hana sababu yoyote ya kufanya hivyo. Mvutano kati ya wasanii hawa wawili umeendelea kushika kasi kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya mzozo huo

Read More
 Sheebah hakunilipa chochote kutumbuiza kwenye shoo zake – Chozen Blood

Sheebah hakunilipa chochote kutumbuiza kwenye shoo zake – Chozen Blood

Msanii kutoka nchini Uganda Chozen Blood amefunguka madai ya kulipwa na msanii Sheebah Karungi kwenye tamasha lake la siku mbili lilofanyika kwenye hoteli ya Serena na Freedom City mwishoni mwa juma lilopita. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Chozen Blood amesema hakupokea hata senti moja kutoka kwa Sheebah kutumbuiza kwenye matamasha yake mawili ambayo yalipokea upendo mkubwa kutoka kwa mashabiki. “Nilitumbuiza Freedom City na siku mbili  Serena. Hakunilipa chochote,” alisema wakati wa mahojiano yake. Utakumbuka hivi karibuni Mwanamuziki Crysto Panda aliwataka wasanii kutumbuiza bila malipo kwenye shoo za wasanii wenzao huku Rickman Manrick akiwataka wasanii kudai malipo kila mara wanapoalikwa kwenye matamasha za muziki kabla ya kupanda jukwaani.

Read More
 Khalifah Aganaga amshambulia Sheebah Karungi kwa kumvunjia heshima

Khalifah Aganaga amshambulia Sheebah Karungi kwa kumvunjia heshima

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo kutoka nchini Uganda, Khalifah Aganaga amemtolea uvivu msanii Sheebah Karungi akimtaja kuwa na roho mbaya. Aganaga anasema alishtuka baada ya Sheebah kushindwa kumualika kwenye tamasha lake katika Hoteli ya Serena jijini Kampala hivi karibuni licha ya kumkingia kifua alipokimbiwa na meneja wake, Jeff Kiwa. “Ulikuja kwangu kipindi meneja wako alikukimbia, kila mtu alikuwa na shaka na uwezo wako kisanaa lakini nilikupa nyimbo, ukaweza kuteka nyoyo za mashabiki zako kwa mara nyingine. Lakini nimesikitishwa na kitendo cha wewe kunivunjia heshima,” alisema kwa uchungu. Aganaga anasema kilichomuumiza zaidi ni kitendo cha Sheebah Karungi kuondoa nembo ya lebo yake ya Bad Character tabia kwenye wimbo wake wa “Bailamos. Hata hivyo amesisitiza kuwa anataka kuthaminiwa wakati bado yupo hai na sio kufanyiwa figisu figisu kwenye shughuli zake za muziki.

Read More
 Sheebah Karungi aweka wazi manyanyaso aliyoyapitia kwenye kundi la Obsession

Sheebah Karungi aweka wazi manyanyaso aliyoyapitia kwenye kundi la Obsession

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Sheebah Karungi amefunguka tusiyoyajua kuhusu uhusiano wake na wasanii wa kundi la Obsessiom ambalo lilimtoa kimuziki. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema wasanii wa kundi hilo walimbana kisanaa kiasi cha kumtenga kwenye baadhi ya shughuli zao za muziki. Hitmaker huyo “Muwomya” amesema kutokana na changamoto alizopitia mikono mwa wasanii wa kundi la Obsession hakukataa tamaa kwenye ndoto yake ya kuwa mwanamuziki mkubwa nchini uganda na ndio maana akajitoa kwenye kundi hilo kuendeleza muziki wake kama msanii wa kujitegemea. Utakumbuka Sheebah Karungi amekuwa kwenye muziki kwa takriban mwongo mmoja uliopita na watu walifahamu kwenye tasnia ya muziki Afrika Mashariki kupitia wimbo wake uitwao Ice  Cream.

Read More
 SHEEBAH KARUNGI MBIONI KUHALALISHA NDOA YAKE KWA NJIA YA HARUSI

SHEEBAH KARUNGI MBIONI KUHALALISHA NDOA YAKE KWA NJIA YA HARUSI

Msaniii kutoka Uganda Sheebah Karungi ametangaza kuhalalisha mahusiano yake kwa kufanya harusi mwezi Disemba mwaka huu kutokana na watu wengi kumshinikiza kuingia kwenye ndoa miaka ya hivi karibuni. Kupitia video aliyo-share kwenye mitandao ya kijamii Hitmaker huyo a “Kansalewo” amesema kuwa hafla ya harusi yake itafanyika Disemba 9 katika hoteli ya Serena Jijini Kampala sambamba na tamasha lake la muziki. Hata hivyo walimwengu wametilia shaka kauli ya Sheebah Karungi kwa kusema kuwa huenda mrembo huyo anatengeneza mazingira ya kuzungumziwa mtandaoni kwa ajili ya kutangaza tamasha lake la muziki. Sheebah Karungi ambaye kipindi cha nyuma alidai kuwa haamini kwenye masuala ya ndoa alikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na meneja wake wa zamani Jeff Kiwa lakini uhusiano wao ulikatishwa na jini mkata kamba baada ya meneja wake huyo kumsaliti kimapenzi.

Read More
 SHEEEBAH KARUNGI AFUNGUA KESI DHIDI YA MWANAUME ALIYEMDHALALISHA KINGONO

SHEEEBAH KARUNGI AFUNGUA KESI DHIDI YA MWANAUME ALIYEMDHALALISHA KINGONO

Hatimaye mwanamuziki Sheebah Karungi  ameandikisha taarifa kwa polisi kuhusu kitendo cha kudhalalishwa kijinsia na mwanaume mmoja wiki kadhaa zilizopita. Msemaji wa polisi nchini Uganda CP Fred Eranga amethibitisha habari hiyo kwa kusema  Sheebah ametoa maelezo yote kuhusu mshukiwa aliyemdhulumu kingono kwenye moja ya onesho lake baada ya kuhojiwa na maafisa wa CID kwa muda, Mei 17 mwaka huu. Eranga aidha amesema Sheebah amekanusha madai ya kunyanyaswa kimapenzi na mwanahabari tajika nchini Uganda Andrew Mwenda licha ya watu wengi kumshuku kuhusika na kitendo cha kumdhalilisha kingono kwenye gari lake kabla ya show yake. Hata hivyo amemshukuru msaniii huyo kwa kushirikiana na vyombo vya usalama kwenye kesi yake hiyo huku akitoa hakikisho kuwa uchunguzi ukikamilika mshukiwa atachukuliwa hatua kali za kisheria iwe funzo kwa wanaume wanaowanyanyasa wanawake kijinsia katika jamiii. Utakumbuka wiki iliyopita Sheebah aligonga vichwa vya habari baada ya kujitokeza na kulaani kitendo cha kunyanyaswa kijinsia na mwanaume mmoja ambaye alidai kuwa anaheshimika katika jamii. Kisa hicho kilizua mjadala mzito miongoni mwa wadau wa muziki  nchini Uganda ambapo wengi walimtaka Sheebah amfungulie kesi mshukiwa huku wengine wakimtaka amuanike hadharani jina la mwanaume huyo jambo ambalo sheebah hakufanya.

Read More
 SHEEBAH ALAANI KITENDO CHA KUDHALALISHWA KINGONO KWENYE MOJA YA ONESHO LAKE

SHEEBAH ALAANI KITENDO CHA KUDHALALISHWA KINGONO KWENYE MOJA YA ONESHO LAKE

Aliyekuwa mwimbaji wa Team No Sleep Sheebah Karungi amemtolea uvivu mwanamume mmoja ambaye alimdhalilisha kijinsia akiwa jukwaani kwenye onyesho lake lilofanyika wikendi hii iliyopita. Kupitia video aliyoshare kwenye instagram yake Sheebah Karungi amesimulia jinsi mwanamume huyo alimvunjia heshima mbele ya timu yake kabla ya kupanda jukwaani wakati wa onyesho lake na kisha kuanza kumshika shika bila idhii yake. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Pim Pim” amesema kitendo cha mwanamume huyo kumdhalilisha kilimkasirisha kiasi cha kutaka kususia shoo yake lakini ilibidi aheshimu kazi yake kwa kuendelea na onesho lake. Sheebah amehoji ni kwa nini wanaume wamekuwa wakiwachukulia wanawake kama vyombo vya starehe kabla ya kuwashauri wawaheshimu wanawake kama wanavyotaka binti zao waheshimiwe. Hata hivyo mashabiki wa sheebah wameonekana kukemea kitendo hicho, wakibainisha namna unyanyasaji wa kijinsia umekuwa ukiendelea kwa muda mrefu huku Wengine wakimtaka amwanike hadharani mwanaume aliyemnyanyasa kijinsia.

Read More
 SHEEBAH KARUNGI AMKANA HADHARANI CINDY SANYU

SHEEBAH KARUNGI AMKANA HADHARANI CINDY SANYU

Staa wa muziki kutoka nchini Uganda Sheebah Karungi amemkana hadharani msanii mwenzake Cindy Sanyu ambaye ni rais wa Muungano wa wanamuziki nchini humo. Kupitia video aliyoishare kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram Sheebah amesikika akisema kuwa hamfahamu kabisa rais wa sasa wa muungano huo huku akimpigia upatu King Saha ambaye pia ametia nia ya kugombea wadhfa wa urais katika muungano wa wanamuziki nchini Uganda. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Nkwata Bulungi” amemwagia sifa King Saha akidai kwamba ndiye mkombozi wa tasnia ya muziki nchini Uganda ikizingatiwa kuwa ana ndoto ya kupigania suala la hakimiliki ambalo kwa muda mrefu limewaathiri wasanii wengi kwenye shughuli zao za kisanaa. Hata hivyo amewataka mashabiki zake kuunga mkono azma ya King Saha kuwa rais wa muungano wa wasanii kwenye uchaguzi ambao utafanyika hivi karibuni. Kwenye uchaguzi huo King Saha atachuana na Daddy Andrea pamoja na Cindy Sanyu ambaye kwa sasa ni rais wa Muungano wa wanamuziki nchini Uganda.

Read More
 SHEEBAH KARUNGI MBIONI KUJA NA RECORD LABEL YAKE YA MUZIKI

SHEEBAH KARUNGI MBIONI KUJA NA RECORD LABEL YAKE YA MUZIKI

Staa wa muziki nchini Uganda Sheebah Karungi ameripotiwa kuwa yupo mbioni kuja na lebo yake ya muziki. Kulingana na chanzo cha karibu na msanii huyo sheebah ana mpango wa kuanzisha na lebo ya muziki ambayo itawasajili wasanii wa kike. Chanzo hicho kimeenda mbali zaidi na kusema kuwa kuanzisha lebo hiyo ilikuwa moja kati ya ndoto ya sheebah Karungi kukukuza vipaji vya watoto wa kike nchini Uganda. Hata hivyo juhudi za vyombo vya habari nchini Uganda kumtafuta Sheebah athibitishe suala hilo halikuzaa matunda ila tutakufahamisha katika taarifa zetu za baadae kama mrembo huyo anakuja na lebo au la. Utakumbuka Sheebah na aliyekuwa meneja wake Jeff Kiwa waliingia ugomvi  mbaya mwishoni mwa mwaka wa 2021 jambo lilompelekea mrembo huyo kuvunja mkataba wake na lebo ya Team No Sleep na kuanza kufanya muziki kama msanii wa kujitegemea.

Read More
 SHEEBAH KARUNGI AWAPA SOMO MASHABIKI ZAKE

SHEEBAH KARUNGI AWAPA SOMO MASHABIKI ZAKE

Nyota wa muziki nchini Uganda Sheebah Karungi amewaonya mashabiki zake dhidi ya kuendeshwa na shinikizo za jamii inayowazunguka. Kupitia mitandao yake kijamii Sheebah amewataka mashabiki zake kufanya vitu ambavyo vitawapa furaha na amani kwa ajili ya kuleta matokeo chanya kwenye jamii badala ya kuwa watumwa wakufuata mkumbo ambao jamii inataka. Hitmaker huyo wa  “Yamba Mukama” ameenda mbali na kusema kwamba mtu anaweza kuwa mfano mwema kwenye jamii yake akitumia uhuru wake kutoa hamsa kwa watu wengine kukuza na kuwekeza kwenye shughuli zao ili kuleta mabadiliko katika jamii. Licha ya kwamba Sheebah amekuwa akiwashauri na kutia moyo vijana wenzake watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakimkosoa  mrembo huyo wakihoji kuwa ni balozi asiye na maadili kwa vijana wachanga nchini Uganda.

Read More
 MSANII MPYA WA TNS RAHMAH PINKY AAPA KUVUNJA REKODI YA SHEEBAH KARUNGI

MSANII MPYA WA TNS RAHMAH PINKY AAPA KUVUNJA REKODI YA SHEEBAH KARUNGI

Baada ya kuachia singo yake ya kwanza iitwayo “Superstar”, msanii mpya aliyechukua nafasi ya Sheebah Karungi kwenye lebo ya muziki ya Team No Sleep, Rahmah Pinky ameibuka na kujinasibu kuwa anaenda kuvunja rekodi ya Sheebah kwenye kiwanda cha muziki nchini Uganda kwa kuachia hits kali bila kupoa. Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 17 amesema atafanikisha hilo kupitia kipaji chake cha uandishi wa nyimbo na ukubwa wa uongozi wake. “Sina ushindani na Sheebah, lakini nataka kufanikiwa zaidi kimuziki kuliko yeye. Nitatumia ujuzi wangu wa kuandika nyimbo kufanikisha hilo,” alisema katika mahojiano na runinga moja  nchini Uganda. Kadhalika, amesema atafanya kazi kwa bidii kama njia ya kumjengea msingi wa mashabiki ambao watamsaidia kupenya kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Hata hivyo Rahmah Pinky amesema kuwa anamheshimu sana Sheebah kama mtu ambaye alifungua milango kwa wasanii wengi wa kike nchini Uganda. Utakumbuka mwishoni mwa mwaka wa 2021 Sheebah Karungi aliigura lebo ya muziki ya Team No Sleep hii ni baada ya kuingia kwenye ugomvi wa mali na meneja wa Jeff Kiwa. Baada ya Sheebah kuondoka Jeff Kiwa alienda mbali zaidi na kumtambulisha Rahmah Pinky kama msanii mpya wa TNS kujaza pengo liloachwa na Hitmaker huyo wa Boy fire.

Read More