Sarah Mtalii Afafanua Kuhusu Video Yake na Simon Kabu: “Hatujarudiana, Tulikuwa Kazi Tu”

Sarah Mtalii Afafanua Kuhusu Video Yake na Simon Kabu: “Hatujarudiana, Tulikuwa Kazi Tu”

Mfanyabiashara maarufu Sarah Mtalii ametoa ufafanuzi kuhusu video inayosambaa mitandaoni ikimuonesha akiwa na aliyekuwa mumewe, Simon Kabu, akisema wazi kuwa haikuwa safari ya kimapenzi bali ya kibiashara. Kupitia taarifa aliyotoa kwa vyombo vya habari, Sarah alieleza kuwa video hiyo imechukuliwa visivyo na umma, huku wengi wakidhania kuwa wawili hao wameamua kurejeana kimapenzi. Hata hivyo, Sarah amesisitiza kuwa wao bado hawajarudiana na kwamba mchakato wa talaka yao bado unaendelea mahakamani. “Ilikuwa ni safari ya kibiashara, si kitu kingine. Sisi si wapenzi tena, na talaka yetu inatarajiwa kukamilika rasmi mwezi Julai,” alisema Sarah kwa uwazi. Taarifa hiyo imekuja baada ya mashabiki wengi kueleza mshangao wao kuona wawili hao wakiwa pamoja, huku baadhi wakipeleka tetesi kuwa huenda wametatua tofauti zao. Hata hivyo, Sarah amesema licha ya kutengana kimapenzi, wanaendelea kushirikiana kibiashara kwa sababu ya maslahi ya pamoja na familia. Simon Kabu bado hajatoa tamko lolote kuhusu tukio hilo au kauli ya Sarah, lakini wadadisi wa mitandao wanazidi kufuatilia kwa karibu hatua za wawili hao.

Read More
 CEO WA BONFIRE ADVENTURE AKIRI KUWA MMLIKI WA MATATU ILIYONUNULIWA NA WILLY PAUL

CEO WA BONFIRE ADVENTURE AKIRI KUWA MMLIKI WA MATATU ILIYONUNULIWA NA WILLY PAUL

Sakata la Willy Paul kudaiwa kununua matatu ambayo imetumika imechukua mkondo mpya baada ya bosi wa Bonfire Adventures Simon Kabu kukiri hadharini yeye ndio mmiliki halisi wa matatu hiyo. Kupitia posti ya msanii Willy Paul kwenye mtandao wa Instagram Kabu ameandika ujumbe wa kumpongeza msanii huyo kwa hatua ya kuwekeza kwenye biashara ya matatu ambapo ameenda mbali zaidi na kujinadi kuwa kabla ya Willy Paul kununua matatu hiyo yeye ndio alikuwa anamiliki. Ujumbe huo umezua hisia mseto mitandaoni ambapo baaadhi ya wakenya wameonekana kumkosoa Kabu kwa madai ya kumvunjia heshima Willy Paul huku wengine wakiendelea kumponda msanii huyo wakihoji kuwa walikuwa na fahamu kuwa matatu hiyo ishatumika.

Read More