Size 8 na DJ Mo Wathibitisha Ndoa Yao Imerejea Imara Baada ya Misukosuko

Size 8 na DJ Mo Wathibitisha Ndoa Yao Imerejea Imara Baada ya Misukosuko

Wanandoa maarufu kwenye tasnia ya muziki wa injili, DJ Mo na Size 8, wamefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu kipindi kigumu cha ndoa yao, ambapo walitengana kwa muda wa miezi saba kabla ya kurudiana. Kwenye mahojiano na runinga ya TV 47, DJ Mo  alielezea kuwa licha ya kutengana, walidumisha mawasiliano kwa sababu ya watoto wao na upendo uliobaki kati yao.  “Ni kweli tulitengana kwa miezi saba. Lakini hatukuwahi kufungiana nje kabisa. Nikienda kuwaona watoto nilimwambia ‘nakumiss’, na nikaanza kumkatia tena kama mwanzo,” alisema DJ Mo kwa ucheshi. Size 8 naye alikiri kuwa kipindi hicho kilikuwa kigumu, lakini kilikuwa muhimu kwa ajili ya kutafakari, kusamehe, na kukua kiroho na kihisia. Alieleza kuwa maombi, ushauri wa ndoa, na nia ya dhati ya kulinda familia yao vilichangia sana kwenye maridhiano yao. “Tulihitaji hiyo nafasi. Tulikuwa tumechoka, lakini sasa tunatembea pamoja tena, tukijifunza kila siku,” alisema Size 8. Wawili hao walisisitiza kuwa ndoa si rahisi, lakini kwa mawasiliano, uvumilivu na imani, kila changamoto inaweza kushughulikiwa. Waliwatia moyo wanandoa wengine kuzungumza wazi wanapopitia migogoro badala ya kuficha au kukata tamaa. Wanandoa hao, ambao pia ni watangazaji wa kipindi cha Dine With The Murayas, wamekuwa mfano wa ndoa ya kisasa yenye changamoto lakini pia inayoweza kujengwa upya kwa msingi wa upendo na imani. Mashabiki wao wengi wamepongeza uamuzi wao wa kusimulia safari yao ya ndoa kwa uwazi, wakisema inaleta matumaini kwa wapenzi na wanandoa wengine wanaopitia changamoto kama hizo.

Read More
 SIZE 8 AFUNGUKA KUHUSU MADAI YA KUIKIMBIA NDOA YAKE

SIZE 8 AFUNGUKA KUHUSU MADAI YA KUIKIMBIA NDOA YAKE

Msanii wa nyimbo za injili Size 8 Reborn amethibitisha kwamba ni kweli aliondoka nyumbani kwake baada ya kuingia kwenye ugomvi na mume wake DJ MO. Akizungumza na mashabiki zake mapema leo kupitia channel yake ya Youtube amesema alikuwa amemkasirikia mume wake ambaye alikuwa amemkosoa hivyo alihitaji nafasi ya kukaa pekee yake na kujifikiria. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Mateke” amesema anashukuru Mungu wamerudiana pamoja baada kumaliza tofauti zao walipopatanishwa na marafiki pamoja na viongozi wa dini. Katika hatua nyingine msanii huyo ambaye pia ni kasisi ametoa angalizo kwa mashabiki zake kutoharibu ndoa zao kisa migogoro isiyokuwa na msingi huku akiwataka kutafuta ushauri nasaha mahusiano yao yanapoingiwa na ukungu. Utakumbuka wikiendi hii iliyopita taarifa za Size 8 kuikimbia ndoa yake ziligonga vichwa vya habari ambapo alidaiwa kuondoka nyumbani kwake akiwa na watoto wake wawili baada ya mume wake DJ MO kumsaliti.

Read More
 NDOA YA SIZE 8 NA DJ MO YAVUNJIKA

NDOA YA SIZE 8 NA DJ MO YAVUNJIKA

Mitandao mbali mbali ya burudani nchini imeripoti kuwa Mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Size 8 Reborn ameikimbia ndoa yake mara baada ya kuingia kwenye ugomvi mkali na mume wake DJ Mo. Vyanzo vya karibu na wawili hao vimesema Size 8 aliondoka nyumbani kwake wiki iliyopita pamoja na watoto wake wawili kutokana na vitendo vya usaliti. Hata hivyo juhudi za marafiki na wanafamilia kuwalewata pamoja wawili hao hazikuzaa matunda kufutia hatua ya Size 8 kuwataka wampe muda wa kufikiria kuhusu hatma ya ndoa yake. Kwa sasa hitmaker huyo wa ngoma ya “Mateke” hamfuati mume wake DJ MO kwenye mitandao ya kijamii huku chanzo cha ndoa yao kuingiwa na ukungu ikiwa haijulikana.

Read More
 SIZE 8 AWAPA SOMO MASHABIKI ZAKE

SIZE 8 AWAPA SOMO MASHABIKI ZAKE

Msanii wa nyimbo za injili nchini Size 8 amewapa somo mashabiki zake kuwa maisha ni zaidi ya pesa, utajiri na umaarufu kwenye mitandao ya kijamii. Kupitia instastory yake Size 8 amesema mali ya dunia sio ufunnguo wa furaha maishani bali ni utumwa ambao umewakosesha wengi amani ambapo ameenda mbali zaidi na kudai kuwa watu wanapaswa kuukimbilia ufalme wa mungu kwani ndio njia pekee ya kupata furaha milele. Post hiyo ya Size 8 imezua gumzo mtandaoni miongoni mwa mashabiki wengi wakionekana kumuunga mkono kwa kauli yake hiyo huku wengi wakimsuta vikali kwa kuwa nabii wa uongo ilhali anajihusisha na mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya kikristo. Utakumbuka tangu Size 8 atawazwe kuwa kasisi watu wengi wamekuwa wakitilia uwezo wake wa kueneza injili wengi wakihoji kuwa msanii huyo hajatosha kuwa mhubiri kamili kwa kuwa amekuwa akiigiza kuponya wagonjwa na kutoa watu mapepo ilhali ana nyota ya kufanya hivyo.

Read More
 SIZE 8 AWAJIBU KITAALAM WANAOMKOSOA MTANDAONI

SIZE 8 AWAJIBU KITAALAM WANAOMKOSOA MTANDAONI

Msanii wa Nyimbo za Injili nchini Size 8 amewajibu kisomi waliomkosoa baada ya video kusambaa mtandaoni ikimuonyesha akitoa mapepo  kutoka kwa waumini wa kanisa moja jijini Nairobi. Katika mahojiano yake na Presenter Ali, Size 8 amesema hana muda wa kuwaaminisha watu kazi anayomfanyia mungu kwani kuna kipindi watakuja kuamini harakati zake za kusambaza injili. Size 8 ambaye ni kasisi amesema watu wanaomkejeli mtandaoni hawatamkatisha tamaa ya kumtumikia mungu kwa kuwa baadhi yao shetani anawatumia kusambaratisha injili. Hitmaker huyo wa “Mateke” amesema hayo alipolamba dili nono ya kuwa balozi wa bidhaa za urembo za RD Beauty. Ikumbukwe tangu Size 8 aachane na muziki wa kidunia mwaka wa 2013 na kuhamia kwenye muziki wa injili watu wamekuwa wakikosoa kwa kwenda kinyume na maandiko matakatifu ya kikristo kutoka mienendo yake ya kimaisha.

Read More
 SIZE 8 AFUNGUKA KUHUSU AFYA YAKE

SIZE 8 AFUNGUKA KUHUSU AFYA YAKE

Msanii aliyegeukia ukasisi  Linet Minyaki maarufu Size 8 amefunguka kuhusu afya yake na kudai kuwa hayuko tayari kupata mtoto. Katika mahojiano na Nicholas Kioko, kasisi huyo alimtakia Wahu heri katika safari yake ya uja uzito na kudai kuwa hayuko tayari kupata mtoto ila  anataka kumfanyia mungu kazi. Size 8 amefunguka kwa kusema shinikizo ya damu imekuwa ikimsumbua kwa muda jambo ambalo lilimpelekea karibu apotezee uja uzito wake. Ameenda mbali zaidi na kusema kwamba karibu apoteze maisha yake alipojifungua mtoto wake kwani alipooza upande mmoja wa mabega yake. Kasisi huyo amesema anapenda watoto na anatamani angeweza kupata watoto kumi lakini kwa sababu ya matatizo ya Afya yanayomsibu ameshauriwa achukue mapumziko.

Read More
 SIZE 8 AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LAKE NA RINGTONE

SIZE 8 AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LAKE NA RINGTONE

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Size 8 amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya Ringtone kudai kuwa alifukuzwa kwenye uzinduzi wa album yake wikiendi iliyopita. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Size 8 amesema amemsamehe ringtone kwa kitendo cha kuvuruga shughuli ya uzinduzi wa album yake huku akipuzilia mbali madai ya kumfukuza msanii huyo kwenye hafla ya kuibariki album yake hiyo kwa kusema kwamba haikuwa kiki kama inavyotafsiriwa kwenye mitandao ya kijamii. Hata hivyo Ringtone kupitia mitandao yake ya kijamii amesisitiza kuwa Size 8 ni mnafiki na mubaguzi kwenye shughuli zake na kitendo chake cha kumfukuza kwenye uzinduzi wa album yake inaonyesha ni jinsi gani size 8 anawadharau wasanii wa nyimbo za injili.

Read More
 RINGTONE AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA YA KUTAKA KUZICHAPA NA MUME WA SIZE 8, DJ MO.

RINGTONE AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA YA KUTAKA KUZICHAPA NA MUME WA SIZE 8, DJ MO.

Mwanamuziki wa nyimbo za injili ringtone ameshika vichwa vya habari wikiendi hii iliyopita mara baada ya kutaka kuzichapa na DJ Mo ambaye mume wa msaniii mwenzake Size 8. Purukushani  kati ya wawili hao ilianza baada ya ringtone kuzua vurugu kwenye hafla ya uzinduzi wa album ya msanii size 8 ambayo imefanyika Februari 13 mwaka huu kwa kutaka kujiunga na wahubiri waliopewa nafasi ya kuibariki album ya size 8, Christ Revealed kabla ya kuingia sokoni. Sasa suala hilo lilimlazimu mume size 8, DJ MO kutumia nguvu kumuondoa ringtone kwenye eneo la tukio kutokana na msanii huyo kutaka kuaharibu hafla ya uzinduzi wa album size 8 kwa kusisitiza kujiunga na wachungaji kwa lazima. Akizungumza nje ya hafla ya uzinduzi wa album size 8 ringtone amesema ameshangazwa na hatua ya DJ Mo kumkataza kujiunga na wahubiri wenzake stejini kuiombea album huku akimsuta vikali kwa hatua ya kumvunjia heshima mbele ya umma licha ya kuwa msanii mkongwe kwenye tasnia ya muziki wa injili nchini. Kwa upande wake DJ MO amepuzilia mbali madai ya ringtone kwa kusema kwamba hayana msingi wowote kwani msanii huyo anapenda kuleta mzaha kwenye shughuli za watu hivyo hangemruhusu kuaharibu hafla ya uzinduzi wa album ya mke wake Size 8. Hata hivyo  jambo hilo limezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii kwani walimwengu wameonekana kumshambulia  ringtone kwa hatua kuvuruga shughuli ya yenyewe huku wengine wakihoji kuwa huenda msanii huyo anatengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwa ajili ya wimbo wake na size 8 ambao unapatikana kwenye Christ Revealed album

Read More
 SIZE 8 MBIONI KUWABARIKI MASHABIKI NA CHRIST REVEALED ALBUM

SIZE 8 MBIONI KUWABARIKI MASHABIKI NA CHRIST REVEALED ALBUM

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Size 8 ametupasha habari njema kuhusu ujio wa album yake mpya iitwayo Christ Revealed ambayo ana mpango wa kuiachia wikiendi hii. Kupitia ukurasa wake wa instagram amesema album yake hiyo itaingia sokoni februari 13 mwaka huu ingawa hajaweka wazi wasanii aliowashirikisha na idadi ya nyimbo zitakazopatikana kwenye album yake mpya. Hata hivyo amesema anamshukuru mungu kwa kumwezesha kukamilisha album hiyo ikizingatiwa kuwa safari ya kuandaa album yake hiyo hajakuwa rahisi kutokana na changamoto nyingi alizokutana nazo. Christ Revealed inakuwa album ya kwanza kwa mtu mzima Size 8 tangu akumbutie ukristo miaka tisa aliyopita baada ya kuachana na muziki wa kidunia.

Read More
 IYANII ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE MPYA NA SIZE 8

IYANII ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE MPYA NA SIZE 8

Hitmaker wa “Pombe” msanii Iyanii ametangaza ujio wa ngoma yake mpya ambayo amemshirisha mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Size 8. Iyanii amethibitisha hilo kupitia instastory ysake kwenyemtandao wa instagram kwa video clip fupi akiwa na Size 8 kwenye mazingira ya studio yenye caption inayoashiria kuwa kuna uwezekano wa Iyanii kufanya wimbo wa pamoja na himaker huyo wa Mateke. Hajafahamika kama wimbvo huo utakuwa wa injili au wa kidunia ila itakuwa ni kazi ya kwanza kwa Iyanii na Size 8 ikiziingatiwa kuwa wawili hao hawajahi fanya wimbo wa pamoja. Huu ni muendelezo mzuri kwa  Iyanii ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa akiachia nyimbo mfululizo bila kupoa.

Read More
 SIZE 8 ATAWAZWA RASMI KUWA KASISI

SIZE 8 ATAWAZWA RASMI KUWA KASISI

Sasa ni rasmi msanii nyimbo za injili nchini Size 8 ametawazwa kuwa mhubiri baada ya kukabidhiwa cheti rasmi ya kuhudumu kama mtumishi wa Mungu. Taarifa hiyo imethibitisha na Size 8 mwenyewe kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kushare baadhi ya picha ya kutawazwa kwake kuwa mhubiri,  hafla ambayo iliongozwa na kasisi Kelvin Ephraim na Jackie Kelvin katika kanisa la JCC, Nairobi. Hitmaker huyo wa “Mateke” ameelezea namna watu walitilia shaka imani yake kipindi anatangaza kukumbatia ukristo lakini mwisho wa siku anashukuru Mungu amefanikisha ndoto aliyokuwa nayo maishani. Size 8 amewashukuru wanafamilia na marafiki kwa kusimama nae kwa safari yake ya kutaka kuwa mhubiri wa neno la Mungu kwa kusema kwamba hajakuwa rahisi. Hata hivyo mashabiki na baadhi ya mastaa wamempongeza kwa hatua hiyo kubwa ambayo amepiga maisha wakimtaka kila la heri kwenye harakati zake za kusambaza injili.

Read More