Sosuun Atoa Somo kwa Mabinti Kuhusu Maisha Bila Watoto

Sosuun Atoa Somo kwa Mabinti Kuhusu Maisha Bila Watoto

Msanii maarufu wa Kenya, Sosuun, ameibua mjadala mkubwa baada ya kutoa ujumbe mzito unaolenga mabinti nchini kuhusu uamuzi wa kutokuwa na watoto. Kupitia video yake Instagram, Sosuun alisema kuwa kutokuwa na watoto kunaweza kuonekana kama uamuzi sahihi katika kizazi cha sasa, hasa kwa kuzingatia changamoto za mahusiano yasiyodumu na watoto kukosa malezi ya wazazi wote wawili. Hata hivyo, aliwaonya mabinti kutofanya maamuzi hayo kwa misingi ya mitindo inayotrend mitandaoni bila kujitafakari kwa undani. Sosuun alisisitiza kuwa maisha ya uzee huja na changamoto zake, ikiwemo kupoteza nguvu, maradhi, na kuhitaji msaada wa kihisia na kimwili. Katika wakati kama huo, familia na watoto mara nyingi huwa nguzo muhimu ya msaada. “Fikiria kwa kina kabla ya kuamua, usifanye kwa sababu kila mtu anafanya,” alisema Sosuun. Ujumbe huo umetajwa kama somo kwa mabinti nchini Kenya, wengi wakimpongeza msanii huyo kwa kuzungumza ukweli unaoangazia thamani ya familia na malezi, huku mjadala ukiendelea mitandaoni kuhusu uhuru wa maamuzi ya kibinafsi.

Read More
 Rapa Sossun Awatetea Wasanii wa Kike Dhidi ya Ubaguzi wa Umri

Rapa Sossun Awatetea Wasanii wa Kike Dhidi ya Ubaguzi wa Umri

Rapper Sossun ameibuka kutetea wasanii wa kike nchini Kenya baada ya kuibuka kwa mijadala mitandaoni kufuatia wimbo mpya uliotolewa na Avril pamoja na Kendi. Kupitia Instagramn yake, amesema kuwa vijana wa Gen Z wanapaswa kuacha kuwakosoa wasanii wa kizazi cha Gen X na Millennial kwa kigezo cha umri, akisisitiza kuwa hoja hiyo haina mashiko katika muziki. Hitmaker huyo wa Sura ya Kazi, amebainisha pia kuwa kuna upendeleo katika tasnia ya muziki, kwani wasanii wa kiume kama Nyashinski na Nameless mara chache hukosolewa kuhusu umri wao, ilhali wenzao wa kike hufanyiwa mashambulizi ya maneno mitandaoni. Kwa mtazamo wake, umri haupaswi kuwa kikwazo kwa wasanii wa kike kuendelea kuachia kazi mpya, kwani mashabiki wao pia wanakua pamoja nao na bado wataendelea kuwapa sapoti.

Read More
 SOSUUN NA VIVIAN WASHAMBULIWA MTANDAONI KWA KUTUMIA KIKI KUTANGAZA NGOMA YAO MPYA

SOSUUN NA VIVIAN WASHAMBULIWA MTANDAONI KWA KUTUMIA KIKI KUTANGAZA NGOMA YAO MPYA

Mashabiki wa muziki nchini wamewatolea uvivu wasanii Vivian pamoja na Sosuun baada wasanii hao kuonekana kutumia kiki kutangaza kazi yao mpya ambayo itaingia sokoni hivi karibuni. Kupitia mitandao yao ya kijamii wawataka Vivian na Sosuun waache suala la kuendekeza kiki kwenye muziki wao na badala yake watoe muziki mzuri ambao utajiuza wenyewe. Aidha wameenda mbali zaidi na kusema kwamba wasanii hao hawana ubunifu kwenye masuala ya kutengeneza matukio yatakayowafanya wazungumzie mtandaoni kwani kiki waliyotengeneza haina mashiko yeyote ya kuteka hisia za watu. Kauli hiyo ya wakenya mara baada ya Sosuun kurekodi video akimvamia Vivian akiwa kwenye studio za main switch na kutaka kumshushia kichapo kwa hatua ya kumvunjia heshima mapema wiki aliposema kuwa familia yake ndio imemfanya apotea kwenye game ya muziki nchini licha ya kuwa kipaji. Utakumbuka kwa sasa Vivian pamoja na Sosuun  wameachia ngoma yao mpya inayokwenda kwa jina la “Chachisha.”

Read More
 SOSUUN AMVUA NGUO VIVIAN KWA MADAI YA KUMVUNJIA HESHIMA

SOSUUN AMVUA NGUO VIVIAN KWA MADAI YA KUMVUNJIA HESHIMA

Rapa wa kike nchini Sosuun amemsuta vikali msanii vivian kwa madai ya kuvumnjia heshima aliposema kwenye moja ya post yake kwenye mtandao wa Instagram kuwa familia ya msanii huyo ndio imeua kipaji chake cha muziki. Kwenye post hiyo vivian alitoa rai kwa sosuun arudi tena kwenye muziki kutokana na mashabiki kukosa nyimbo zake kwa muda ambapo alienda mbali zaidi kudai kuwa hatua ya sosuun kupotea kwenye muziki imetokana na yeye kujikita zaidi kwenye masuala ya familia, jambo ambalo amedai limemponza kimuziki. Sasa Kupitia instagram wake Sosuun aliibuka na kutupia maneno mazito vivian kwa kusema kwmbaa aache  kumfuatilia maisha yake na badala yake amzalie mume wake watoto aone kama atabaki kwenye muziki wake ambapo amejitapa kwa kusema kwamba amemzidi kimuziki licha ya ukimya wa miaka 10 kwenye muziki wake. Haikushia hapo Sosuun alienda mbali zadi na kumtaka vivian abadili muonekano wake wa kisanii huku akisema kwamba msanii huyo anajishusha kimuziki kwa  kuvalia mavazi yasioendana na brand yake licha ya kuwa mwiimbaji mzuri. Hata hivyo hatua ya wawili hao kutupiana maneno makali mitandaoni imeonekana kuibua maswali miongoni mwa walimwengu kwenye mitandao ambapo baadhi ya wamemnyoshea kidole cha lawama vivian kwa kumvunjia heshima sosuun kwa kuyaweka mapungufu yake mtandaoni huku wengine wakihoji kuwa huenda wawili hao wanatengeneza mazingira ya kuzungumziwa ili waweze kuachia ngoma ya pamoja.

Read More