SPICE DIANA: NITAPATA MTOTO BAADA YA SHEEBAH

SPICE DIANA: NITAPATA MTOTO BAADA YA SHEEBAH

Staa wa muziki nchini Uganda Spice Diana,, alisherehekea kumbukizi yake ya kuzaliwa mwishoni mwa juma lilopita katika hoteli ya Serena kwenye hafla ya iliyohudhuriwa na wanafamilia pamoja na marafiki. Sasa akiwa kwenye moja ya interview hitmaker huyo wa body amedai kwamba hana mpango wa kuaanzisha familia hivi karibuni, ikizingatiwa kuwa hakuna wakati maalum wa kuolewa au kupata watoto. Spice Diana ambaye kwa sasa ametimiza umri wa miaka 27 Amebainisha kuwa bado yuko bize na kazi zake za muziki, hivyo ataanzisha familia pindi tu atakapotimiza ndoto zake kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Mrembo huyo ameenda mbali zaidi na kumtumia msanii mwenzake Sheebah, ambaye ana umri wa miaka 32, kama role model wake kwenye masuala ya ndoa ambapo amewataka watu kutomshinikiza kuingia kwenye ndoa wakati hayuko tayari kisaikolojia.

Read More