UONGOZI WA MEN IN BUSINESS WAMTAMBULISHA STIVO THE SIMPLE BOY KAMA MSANII WAO MPYA

UONGOZI WA MEN IN BUSINESS WAMTAMBULISHA STIVO THE SIMPLE BOY KAMA MSANII WAO MPYA

Lebo ya muziki ya Men in Business imemtambulisha rasmi Stivo The Simple Boy kama msanii wao mpya. Lebo hiyo imesema imesaini msanii huyo kwa mkataba wa miaka miwili ambapo watasimamia shughuli zake za muziki. Uongozi wa Men in Business umewataka wakenya waendelee kufuatilia kazi za Stivo The Simple Boy kwani kuanzia sasa atakuwa na muendelezo mzuru wa kuachia ngoma bila kupoa. Hata hivyo baada ya kutambulishwa kama msanii mpya wa MIB, Stivo The Simple Boy amewashukuru wakenya kwa upendo ambao wamemuonyesha tangu aanze muziki huku akiahidi kuwapa burudani zaidi. Utakumbuka Stivo The Simple Boy alikuwa akisamimiwa na lebo ya muziki ya Made In Kibera ambayo ilimtoa kimuziki lakini msanii huyo aliahamua kuigura uongozi huo baada ya kupora pesa zake alizokuwa anazichuma kupitia muziki wake

Read More
 STIVO THE SIMPLE BOY ATHIBITISHA KUWA MGONJWA, AANDIKA UJUMBE MZITO INSTAGRAM

STIVO THE SIMPLE BOY ATHIBITISHA KUWA MGONJWA, AANDIKA UJUMBE MZITO INSTAGRAM

Msanii wa muziki nchini Stephen Otieno maarufu kama Stivo The Simple Boy amewaacha mashabiki na maswali mengi baada ya kuchapisha ujumbe kwenye akaunti yake mpya ya Instagram akisema kwamba amekuwa mgonjwa kwa muda sasa. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Mihadarati” ameposti picha akiwa kwenye mazingira ya studio yenye caption inayosomeka “Mziki ni dawa yangu, Mafans wangu wish me a quick recovery niwapee ngoma mpya. Au sio.”,  ujumbe unaowataka mashabiki zake wamuombee apate nafuu ili aweze kuwabariki na ngoma mpya. Posti yake hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki zake ambao walishuka kwenye uwanja wa comment ya post kwenye mtandao wa Instagram na kumtakia afueni ya haraka. Stivo The Simple ni miongoni mwa wasanii wachache ambao wamewakosha wapenzi wa muziki mzuri nchini Kenya kutokana na aina ya uimbaji wake lakini pia ni moja kati ya wasanii waliopata umaarufu mkubwa ndani ya kipindi kifupi tofauti na wasanii wengine.

Read More
 PRITTY VISHY ATANGAZA KUVUNJA UHUSIANO WAKE WA KIMAPENZI NA MSANII STIVO THE SIMPLE BOY

PRITTY VISHY ATANGAZA KUVUNJA UHUSIANO WAKE WA KIMAPENZI NA MSANII STIVO THE SIMPLE BOY

Mchumba wa msanii Stivo The Simple Boy ametangaza kuachana na msanii huyo baada ya kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa muda. Akipiga stori na mzuka kibao Pritty Vishy amesema amechukua maamuzi ya kuachana na Stivo the simple baada ya msanii huyo kuonekana kutomdhamini kwani amekuwa akiusikiliza sana uongozi wake wa Made In Kibera. Kauli ya Pritty Vishy inakuja siku chache baada kudai kuwa uongozi wa Made in Kibera umekuwa ukimnyanyasa Stivo the Simple kwa kupora pesa zake ambazo amezitolea jasho kupitia muziki. Hata hivyo Stivo The Simple hajatoa tamko lolote kuhusiana na madai ya Pritty Vishy ila ni jambo la kusubiriwa

Read More
 MCHUMBA WA STIVO THE SIMPLE BOY AANIKA MAOVU AMBAYO MSANII HUYO ANAPITIA CHINI UONGOZI WAKE WA MADE IN KIBERA

MCHUMBA WA STIVO THE SIMPLE BOY AANIKA MAOVU AMBAYO MSANII HUYO ANAPITIA CHINI UONGOZI WAKE WA MADE IN KIBERA

Mpenzi wa msanii Stivo the Simple boy Pritty Vishy ameanika maovu ambayo msanii huyo amekuwa akipitia chini ya uongozi wake wa Made in Kibera. Akipiga stori na SPM Buzz mrembo huyo amesema uongozi wa Stivo umekuwa ukipora miraba ya nyimbo za msanii huyo huku akitoa mfano kuna kipindi stivo alisaini dili la shillingi laki 2 lakini uongozi wake ulimlipa shillingi elfu 4. Pritty Vishy ameenda mbali zaidi na kusema kuwa uongozi wa stivo umekuwa ukidhibiti mitandao yote ya kijamii ya msanii huyo baada ya video akiwa na stivo katika mazingira mabaya kuenea mtandaoni. Hata hivyo amesema stivo amekata mawasiliano nae baada kuhama Kibera huku akiongeza kuwa uamuzi huo umetokana na video iliyosambaa kwenye mtandao wa Tiktok ambayo uongozi wake haukupendezwa nayo. Hii sio mara ya kwanza kwa stivo the simple kudaiwa kuwa anapitia maisha magumu chini uongozi wake wa made in kibera mwaka jana watumiaji wa mitandao ya kijamii waliibua madai hayo jambo lilofanya uongozi wake  kujitokeza na kukana tuhuma hizo.  

Read More