Telegram Yazindua Cocoon AI Isiyokusanya Data za Watumiaji

Telegram Yazindua Cocoon AI Isiyokusanya Data za Watumiaji

Kampuni ya Telegram imeamua kuingia kwenye ushindani mkali na Meta AI kwa kuzindua mfumo mpya wa akili bandia unaolenga kulinda faragha ya watumiaji. Hatua hii inalenga kuwavutia watumiaji ambao hawapendezwi na bidhaa za Meta, zinazokosolewa kwa kukusanya data binafsi za watumiaji. Telegram imeanzisha kipengele kipya kinachoitwa AI Summaries, kinachoendeshwa na akili bandia mpya iitwayo Cocoon. Kupitia Cocoon, watumiaji sasa wanaweza kufupisha ujumbe mrefu kwenye channels na kupata muhtasari kwa haraka na kwa urahisi zaidi. Kwa mujibu wa Telegram, Cocoon ni AI iliyojengwa kwa misingi ya faragha na usalama wa data. Kila ombi la mtumiaji hufichwa kwa mfumo wa encryption, na data hazionekani wala kuhifadhiwa na Telegram au wasimamizi wa Cocoon. Aidha, hakuna uhusiano kati ya maombi ya AI na utambulisho wa mtumiaji. Hatua hii inaonesha mwelekeo mpya wa Telegram wa kuimarisha ulinzi wa taarifa binafsi, huku ikizidi kuleta ushindani katika sekta ya akili bandia duniani.

Read More
 Telegram Yaweka Rasmi Mfumo wa Passkey kwa Watumiaji Wote

Telegram Yaweka Rasmi Mfumo wa Passkey kwa Watumiaji Wote

Telegram imeweka rasmi mfumo mpya wa usalama unaojulikana kama Passkey, hatua inayolenga kuimarisha zaidi usalama wa akaunti za watumiaji wake duniani kote. Mfumo huu sasa unapatikana kwa watumiaji wote wa iOS, Android, macOS na Windows. Mfumo wa Passkey unamwezesha mtumiaji kuingia kwenye akaunti yake bila kutumia neno la siri (password) au PIN za kawaida. Badala yake, mtumiaji hutumia key maalum inayohifadhiwa moja kwa moja kwenye simu au kompyuta yake. Key hiyo hufanya kazi kwa kushirikiana na teknolojia za biometric kama vile Face ID, Fingerprint (alama ya kidole) au njia nyingine za uthibitisho wa kifaa. Kwa mujibu wa Telegram, Passkey ni salama zaidi ikilinganishwa na matumizi ya password za kawaida. Hii ni kwa sababu key hiyo haijirudii, haiwezi kutumika kwenye kifaa kingine bila ruhusa, na ni vigumu sana kudukuliwa. Aidha, hata kama mtu atapata password yako ya zamani, hataweza kuingia kwenye akaunti yako bila kutumia biometric zako binafsi. Hatua hii inalenga kupunguza matukio ya udukuzi wa akaunti, wizi wa taarifa binafsi na udanganyifu wa mtandaoni, ambao umekuwa ukiongezeka siku hadi siku. Kwa mfumo wa Passkey, usalama wa mtumiaji unakuwa umefungamana moja kwa moja na kifaa chake pamoja na utambulisho wake wa kibaiometriki. Telegram inaungana na makampuni makubwa ya teknolojia kama WhatsApp, Facebook, Google, Apple ID, Spotify na mengineyo ambayo tayari yameanza kutumia au kuimarisha matumizi ya Passkey kama njia mbadala ya nenosiri la kawaida.

Read More