Tems Aweka Historia kwa Kutumbuiza Katika Fainali ya FIFA Club World Cup

Tems Aweka Historia kwa Kutumbuiza Katika Fainali ya FIFA Club World Cup

Mwanamuziki nyota kutoka Nigeria, Tems, ameandika historia mpya usiku wa kuamkia leo kwa kuwa msanii wa kwanza wa Kiafrika kutumbuiza kwenye fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu (FIFA Club World Cup), hatua inayotajwa kuonyesha wazi ukubwa wa kipaji chake na kuendeleza hadhi ya muziki wa Afrika kwenye jukwaa la kimataifa. Tems alitumbuiza katika burudani ya mapumziko (Halftime Show) sambamba na mastaa wa kimataifa, Doja Cat kutoka Marekani na J Balvin wa Colombia katika tukio lililofanyika kwenye Uwanja wa MetLife, New Jersey, Marekani. Hii ni mara ya kwanza kabisa kwa michuano hiyo ya Club World Cup kuandaa onyesho la burudani katikati ya mchezo (halftime show), hivyo kufanya tukio hilo kuwa la kihistoria katika dunia ya soka na burudani. Burudani hiyo ya kuvutia ilifanyika wakati wa fainali ya michuano hiyo, ambapo klabu ya Chelsea FC kutoka England iliibuka mshindi dhidi ya mabingwa wa Ufaransa, Paris Saint-Germain (PSG), na kutwaa taji la Kombe la Dunia kwa ngazi ya vilabu. Uwepo wa Tems katika jukwaa hilo umepongezwa na mashabiki na wadau wa sanaa kama hatua kubwa kwa wasanii wa Afrika, huku wengi wakisema kwamba anazidi kuvunja mipaka na kupeperusha bendera ya bara la Afrika kwa mafanikio makubwa. Tems, anayefahamika kwa sauti yake ya kipekee na uandishi wa nyimbo wa hali ya juu, amekuwa akivuma kimataifa kwa miaka ya hivi karibuni, na sasa amejiweka kwenye ramani ya wasanii wa dunia wanaotumbuiza kwenye matukio makubwa ya kihistoria.

Read More
 Tems, Doja Cat na J Balvin Kuwasha Jukwaa la Club World Cup Usiku Huu

Tems, Doja Cat na J Balvin Kuwasha Jukwaa la Club World Cup Usiku Huu

Usiku wa leo, majira ya saa nne usiku kwa saa za Afrika Mashariki, macho na masikio ya mashabiki wa soka duniani yatakuwa yameelekezwa kwenye Uwanja wa MetLife, New Jersey, Marekani, ambako fainali ya FIFA Club World Cup itapigwa kati ya mabingwa wa Ulaya, Chelsea FC kutoka England, na mabingwa wa Ufaransa, Paris Saint-Germain (PSG). Mchezo huu unatarajiwa kuwa wa kusisimua na wa kiwango cha juu, ukiwa ndio hitimisho la mashindano hayo ya kimataifa kwa ngazi ya vilabu. Katika kilele cha tukio hilo, kutakuwa na Halftime Show ya aina yake, ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya michuano ya Club World Cup, kutafanyika onesho la burudani kipindi cha mapumziko. Wasanii watatu wakubwa duniani, Doja Cat kutoka Marekani, J Balvin kutoka Colombia, na Tems kutoka Nigeria watatumbuiza mbele ya mashabiki lukuki ndani ya uwanja na wale wanaotazama kupitia runinga duniani kote. Tukio hili la kihistoria linaashiria hatua mpya katika kuunganisha michezo na burudani, na linathibitisha hadhi ya soka kama jukwaa pana la utamaduni wa dunia.

Read More
 Tems Azindua Programu ya Kuwawezesha Wanawake Katika Muziki

Tems Azindua Programu ya Kuwawezesha Wanawake Katika Muziki

Mwanamuziki nyota kutoka Nigeria, Tems, amezindua rasmi programu mpya ya kuwawezesha wanawake vijana kwenye tasnia ya muziki, iitwayo The Leading Vibe Initiative. Programu hiyo inalenga kuwapatia wanawake mafunzo na nyenzo muhimu za kufanikisha kazi zao katika sekta ya muziki. Warsha ya kwanza chini ya mpango huu imepangwa kufanyika kwa siku mbili, kuanzia Agosti 8 hadi 9 jijini Lagos, Nigeria, ambapo washiriki watajifunza kuhusu uandishi wa nyimbo, uzalishaji wa muziki, pamoja na kushiriki midahalo na wataalam wa muziki. Pia kutakuwa na vikao vya studio kwa ajili ya kukuza ubunifu wa washiriki. Mpango huu unawalenga wanawake 15 hadi 20 wenye nia na vipaji katika muziki, huku tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ikiwa Julai 13. Washiriki watapewa vifaa vya kisasa vya uzalishaji na rasilimali nyingine muhimu zitakazowawezesha kuendeleza kazi zao kwa ufanisi. Tems amesema kuwa kupitia The Leading Vibe Initiative, anataka kuhakikisha kuwa wanawake barani Afrika wanapata nafasi ya kujiamini, kupata maarifa sahihi, na kuchangia katika maendeleo ya muziki ndani na nje ya bara. “Ni wakati wa wanawake kuwa sauti kubwa katika muziki wa Afrika. Ninaamini wakipewa nafasi na zana sahihi, wanaweza kuvuka mipaka,” alisema Tems. Tems, ambaye tayari ameweka historia kwa kushinda tuzo mbili za Grammy na kushika nafasi za juu kwenye chati za Billboard, anatarajia kupanua programu hii hadi miji mingine barani Afrika katika siku za uso

Read More
 Rihanna na Tems watajwa kwa mara ya kwanza kuwania tuzo ya Oscar

Rihanna na Tems watajwa kwa mara ya kwanza kuwania tuzo ya Oscar

Mwimbaji Temilade Openiyi a.k.a Tems kutoka Nigeria, ameweka Historia ya kuwa Msanii mwenye muda mfupi kwenye Muziki na kufanikiwa kutajwa kuwania Tuzo ya Oscar kupitia wimbo wa LiftMeUp alioshiriki kuuandika pamoja na Rihanna Licha ya Ukubwa wake kwenye tasnia ya Muziki, kwa mara ya kwanza Mwimbaji Rihanna naye amefanikiwa kuingia kwenye kipengele cha ‘Best Original Song’ kupitia wimbo wa Lift Me Up uliotumika kama Soundtrack ya Filamu ya Black Panther: WakandaForever Tems amefanikiwa kushinda Tuzo zaidi 30 na ametajwa kuwania zaidi ya Tuzo 80 hadi sasa. Rihanna amekuwa kwenye Muziki kwa takribani Miaka 18 na hadi sasa ana Tuzo 235 na kutajwa kuwania zaidi ya Tuzo 630. Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa Machi 12, mwaka 2023 huko Jijini Los Angeles nchini Marekani.

Read More
 Wizkid amu-unfollow Tems kwenye mtandao wa Instagram

Wizkid amu-unfollow Tems kwenye mtandao wa Instagram

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria Wizkid amu-unfollow msanii mwenzake Tems kwenye mtandao wa Instagram. Wawili hao ambao wmefanikiwa kutengeneza Hit Song ya Dunia “Essence” wameonekana kuwa mbalimbali kwa muda jambo ambalo mashabiki walianza kujiuliza maswali juu ya mahusiano yao. Hatua hiyo ya Wizkid kumpunguza Tems kwenye orodha ya wafuasi wake kwenye mtandao wa instagram imekuja ikiwa ni wiki chache toka Wizkid aachie kolabo yake na Ayra Star “SUGAR” Pamoja na Wikzid kumpunguza Tems lakini bado Tems ame mfollow Wizkid kwenye mtandao huo wa instagram

Read More
 Wasanii wa Nigeria Tems na Burna Boy watajwa kuwania Grammy 2023

Wasanii wa Nigeria Tems na Burna Boy watajwa kuwania Grammy 2023

Wasanii wa muziki kutokea nchini Nigeria, Burna Boy na Tems wametajwa kuwania vipengele viwili kila mmoja katika Tuzo za Grammy 2022. Burna Boy ametajwa kwenye vipengele viwili, “Best Global Music Performance” kwa ngoma yake ya “Last Last” na kingine ni “Best Global Music Album” – Love Damini. Naye Tems ametajwa kwenye vipengele viwili kama “Best Melodic Rap Performance” kupitia ngoma aliyoshirikishwa na future Ft Drake – Wait For You na pia “Best Rap Song” – Wait For You.

Read More
 Tems ashindwa kutumbuiza Kenya

Tems ashindwa kutumbuiza Kenya

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria Tems ametangaza kuwa hatoweza kutumbuiza kwenye Tamasha la Tukutane Festival kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake. Tems amelithibitisha hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kutoa ahadi kwa Wakenya kuwa siku za mbeleni atatua nchini kwa ajili ya kutoa burudani. “Kusema kweli, inasikitisha sana kusema haya lakini sitaweza kutumbuiza kwenye Tamasha la Tukutane kutokana na mazingira yaliyo nje ya uwezo wangu.” “Nimekatishwa tamaa kama ninyi nyote lakini ninatazamia kuja na kuwapa onyesho ambalo mnastahili. Nawapenda nyote.” Ameandika Twitter. Hata hivyo maelezo hayo ya Tems yanapishana na yale yaliyotolewa na waandaji wa tamasha la “Tukutane” (SIC) ambao wao kupitia taarifa yao waliyoitoa wameeleza kwamba, nyota huyo alishalipwa gharama zake zote siku 15 zilizopita, na tamasha lilikuwa lifanyike Oktoba 15. Lakini ghafla meneja wa Tems akawaambia Tems hatoweza kuja kwenye onesho hilo, hajisikii kuja Kenya. Waandaaji wa “Tukutane”, (SIC) wameeleza walishtushwa na taarifa hiyo iliyowavunja moyo. Aidha, wameomba radhi kwa mashabiki kufuatia kadhia hiyo na wanatazamia kupanga tarehe nyingine mpya kwa ajili ya tamasha hilo.

Read More
 Kendrick Lamar ashinda Tuzo ya Msanii Bora wa  Hiphop kwenye BET Hip-Hop Awards 2022

Kendrick Lamar ashinda Tuzo ya Msanii Bora wa Hiphop kwenye BET Hip-Hop Awards 2022

Rapa Kendrick Lamar ameibuka mshindi wa kipengele cha Hip-Hop Artist Of The Year kwenye Tuzo za BET Hip-Hop 2022 ambazo zinatolewa usiku wa kuamki leo nchini Marekani. Kendrick Lamar pia ameondoka na ushindi kwenye vipengele vya Lyricist Of The Year, Best Hip Hop Video “Family Ties”, Best Live Performer na Hip Hop Album Of The Year (Mr. Morale & The Big Steppers) Kwa upande mwingine Rapa 50 Cent ameibuka mshindi wa Tuzo ya ‘Hustler Of The Year’ akiwaangusha DJ Khaled, Drake, Cardi B, Jay-Z, Kanye West na Megan Thee Stallion. Kolabo ya Future, Tems na Drake “Wait For You” imeshinda Tuzo ya Best Collaboration kwenye Tuzo za BET Hip Hop 2022.

Read More
 TEMS APATWA NA TATIZO LA KOO

TEMS APATWA NA TATIZO LA KOO

Mwimbaji nyota wa muziki kutoka Nigeria tems ambaye anafanya vizuri Kimataifa ameweka wazi kukutwa na tatizo la koo ambalo limepelekea kutotokwa na sauti. TEMS ametangaza hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo kwenye taarifa yake ameeleza kwasasa hayupo sawa kufuatia kupata tatizo hilo. Hivyo inamlazimu kusimama kufanya muziki kwa muda, pamoja na kusitisha matamasha yake mawili aliyokuwa akitarajia kuyafanya huko Birmngham na London nchini Uingereza. Itakumbukwa tatizo hilo la sauti pia liliwahi kumkuta mwimbaji na mtayarishaji wa muziki nchini nigeria Tekno mwaka 2018, ambaye yeye alipumzika kwa takribani mwaka mmoja na nusu hadi kuwa sawa.

Read More
 TEMS AKUMBUKA MAGUMU ALIYOPITIA GEREZANI UGANDA

TEMS AKUMBUKA MAGUMU ALIYOPITIA GEREZANI UGANDA

Mwanamuziki wa kike kutoka nchini Nigeria Tems amekumbuka kipindi ambacho aliwekwa gerezani mwishoni mwa mwaka 2020 nchini Uganda. Kupitia akaunti yake ya Twitter Terms ameandika “ Nyakati kama hizi mwaka jana nilikua gerezani na watoto na kina mama nchini Uganda. Sitaki kuamini vitu nilivyo viona” Ikumbukwe Terms pamoja na mwanamuziki omahlay walitiwa mbaroni nchini Uganda baada ya kukiuka masharti ya COVID-19 na kufanya onyesho ambalo lilipelekea wawili hao kupelekwa gerezani

Read More