Thee Pluto Akana Madai ya Kudate Mwanamke wa Kisomali
YouTuber maarufu wa Kenya, Thee Pluto, amejitokeza kufafanua madai yaliyosambaa mitandaoni kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali. Akizungumza kupitia mitandao yake ya kijamii, Thee Pluto amesema kuwa si kila mtu anayepigwa naye picha au kuonekana naye hadharani ni mpenzi wake. Amesisitiza kuwa uvumi wa aina hiyo ni wa kupotosha na umekuwa ukiwaweka watu katika hali ya mkanganyiko kuhusu maisha yake ya kibinafsi. Thee Pluto, ambaye ni maarufu kwa majaribio yake ya uaminifu (loyalty tests) mitandaoni, ameomba mashabiki na wafuasi wake kutofautisha kati ya mahusiano ya kirafiki na kimapenzi, akiongeza kwamba si kila anayeonekana naye ana uhusiano wa kindoa naye.
Read More