Mashabiki Wapagawa Baada ya Toxic Lyrikali Kuonekana na Mrembo
Msanii anayetikisa anga la muziki kwa sasa nchini Kenya, Toxic Lyrikali, ameibua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kushiriki kipande cha video kwenye Instagram Story akionekana akiwa kwenye mahaba mazito na mrembo asiyejulikana. Katika video hiyo, Toxic na mrembo huyo wameonekana wakifurahia ukaribu wao bila kujificha, jambo ambalo limezidisha tetesi za kimapenzi. Baadhi ya mashabiki wanasema huenda huyo ndiye mpenzi wake mpya, hasa ikizingatiwa kwamba msanii huyo hana mazoea ya kuweka warembo wala kuonyesha maisha yake ya mapenzi mitandaoni. Hata hivyo, wengine wanahisi inaweza kuwa sehemu ya maandalizi ya kazi yake mpya. Inadaiwa kuwa Toxic Lyrikali anajiandaa kuachia wimbo unaoitwa Hide & Sick akimshirikisha Mjaka Wa Fine, na kwamba tukio hilo linaweza kuwa sehemu ya kuikuza kazi hiyo kabla ya kuachiwa rasmi. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kwa shauku kuona kama video hiyo ilikuwa ishara ya mapenzi mapya au ni mbinu ya kuibua msisimko kuelekea ujio wa kazi yake mpya. Msanii huyo bado hajatoa tamko lolote kuhusu video hiyo.
Read More