Toxic Lyrikali Amwaibisha Wakuu Music kwa Kuanika DM zake Akilizimisha Bifu

Toxic Lyrikali Amwaibisha Wakuu Music kwa Kuanika DM zake Akilizimisha Bifu

Rapa kutoka Kenya, Toxic Lyrikali, amezua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kuanika jumbe za faragha za WhatsApp alizodai kutumiwa na Wakuu Music, akimshinikiza kuingia kwenye bifu naye kwa lengo la kuvuta umakini wa mashabiki. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Toxic ameshare screenshots za mawasiliano hayo zikimuonyesha Wakuu Music akimkabili kuhusu madai kuwa alikuwa amemdiss kwenye nyimbo zake. Hata hivyo, Toxic amekanusha madai hayo na kudai kuwa kinachoendelea ni juhudi za kulazimisha bifu ya kutengeneza headlines. Hitmaker huyo wa Back Bencher, ameonekana kushangazwa na kitendo hicho, akisema kuwa ni jambo la kushangaza kuona mtu mzima bado anamtext akilazimisha ugomvi wa kisanii ili apate kuzungumziwa na mashabiki. Kwa mujibu wa jumbe alizochapisha, Wakuu Music anaonekana kukerwa na madai kwamba amedharauliwa katika baadhi ya mistari ya ngoma za Toxic, jambo ambalo rapa huyo amekanusha na kudai kuwa hana mpango wa kuingia kwenye bifu la bandia kwa ajili ya hype.

Read More
 Toxic Lyrikali Aidharau Diss track ya Fathermoh kwa Kuita Mchongoano

Toxic Lyrikali Aidharau Diss track ya Fathermoh kwa Kuita Mchongoano

Rapa Toxic Lyrikali ameonekana kutochukulia kwa uzito diss track iliyodaiwa kumlenga kutoka kwa msanii wa Gengetone, Fathermoh, akisema kuwa kinachoendelea si chochote zaidi ya mchongoano wa kawaida kwenye muziki. Akizungumza Insta live, Toxic Lyrikali amesema hana muda wa kujibu diss track wala kuingia kwenye mabishano ya kitoto, Akisisitiza kuwa amejikita zaidi katika kazi yake na mafanikio anayopata kwa sasa. Rapa huyo ametoa wito kwa wasanii waliomtangulia kwenye tasnia kuacha wivu unaochochewa na mafanikio ya wasanii chipukizi, akisema badala ya kushambuliana mitandaoni au kwenye nyimbo, ni bora waweke nguvu kwenye kufanya kazi na kuboresha sanaa zao. Toxic Lyrikali ameongeza kuwa anathamini upendo mkubwa anaopata kutoka kwa mashabiki wake, hasa kutoka Kenya, akisema huo ndio unaompa nguvu ya kuendelea kupiga hatua bila kuathiriwa na maneno ya pembeni.

Read More
 Rapa Toxic Lyrikali Amuaibisha Tipsy Gee kwa Kuanika Video ya Kuomba Msamaha

Rapa Toxic Lyrikali Amuaibisha Tipsy Gee kwa Kuanika Video ya Kuomba Msamaha

Rapa Toxic Lyrikali ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kuanika video inayomuonyesha msanii wa gengetone Tipsy Gee akimuomba msamaha, kufuatia mzozo wa muda mrefu uliokuwa ukiendelea kati yao. Katika video hiyo inayosambaa kwa kasi, Tipsy Gee anaonekana akiwa mpole na mnyenyekevu, akizungumza kwa sauti ya chini na kumuomba radhi Toxic Lyrikali, hali ambayo imewafanya baadhi ya mashabiki kudai kuwa alijinyenyekeza kama mtoto baada ya maneno makali aliyokuwa akitoa awali. Kwa mujibu wa Toxic Lyrikali, Tipsy Gee amekuwa akimtukana na kumdhalilisha kupitia mitandao ya kijamii kwa kipindi kirefu, hali iliyozua mvutano na maneno makali baina ya wasanii hao wawili. Hata hivyo, mambo yalichukua mkondo mpya baada ya Toxic kuchapisha video hiyo, akidai ni ushahidi kuwa mpinzani wake alitambua makosa yake na kuamua kuomba msamaha.

Read More
 Toxic Lyrikali Awapa Vijana Moyo wa Kutia Bidii Baada ya Kushare Picha Yakeya Kazi ya Mjengo

Toxic Lyrikali Awapa Vijana Moyo wa Kutia Bidii Baada ya Kushare Picha Yakeya Kazi ya Mjengo

Msanii wa muziki kutoka Kenya,Toxic Lyrikali, amewagusa wengi mitandaoni baada ya kushare picha ya zamani inayomuonesha akiwa kazini akifanya kazi ya mjengo, miaka kadhaa kabla ya kupata mafanikio kwenye muziki wake. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Toxic Lyrikali ameeleza kuwa picha hiyo ni ukumbusho wa safari yake ya maisha, akisisitiza kuwa mafanikio hayaji kwa njia za mkato bali kwa juhudi, subira na kujituma bila kukata tamaa. Mashabiki wengi wamempongeza hitmaker huyo wa Back Bencher kwa unyenyekevu na ujasiri wa kuonyesha alikotoka, wakisema ni funzo tosha kwa vijana wanaodharau kazi ndogo au kukata tamaa mapema wanapokosa mafanikio ya haraka. Kwa mujibu wa mashabiki hao, simulizi ya Toxic Lyrikali inaonyesha wazi kuwa kila kazi halali ina heshima yake, na kwamba mafanikio ni matokeo ya safari ndefu yenye changamoto nyingi.

Read More
 Rapper Toxic Lyrikali Ashinda Tuzo Mbili Kwenye Unkut HipHop Awards 2025

Rapper Toxic Lyrikali Ashinda Tuzo Mbili Kwenye Unkut HipHop Awards 2025

Msanii wa hip-hop Toxic ameweka rekodi mpya baada ya kutwaa tuzo mbili kubwa katika hafla ya Unkut Hip-Hop Awards 2025, na hivyo kuthibitisha ubabe wake katika game ya rap nchini. Toxic alishinda tuzo ya Msanii Bora wa Kiume, akiwapiku wakali kama Khaligraph Jones, Octopizzo, Breeder LW na Masterpiece, katika kipengele kilichoonekana kuwa na ushindani mkali zaidi mwaka huu. Sanjari na ushindi huo, Toxic pia aliibuka mshindi katika kipengele cha Wimbo Bora wa Mwaka kupitia hit yake “Chinje”, ngoma iliyotamba sana mitandaoni na kwenye vituo vya radio. Wimbo huo uliwashinda vibaya washindani waliokuwa wakipewa nafasi kubwa, akiwemo Wakadinali, Nyashinski, Buruklyn Boyz, na tena Khaligraph Jones. Mashabiki wamepongeza mafanikio yake wakisema Toxic sasa anathibitisha kuwa nguvu mpya kwenye hip-hop imefika na inazidi kuvunja rekodi. Mwenyewe, kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliwashukuru mashabiki kwa kumuamini na kuahidi mwaka wa mafanikio makubwa zaidi.

Read More
 Mashabiki Wapagawa Baada ya Toxic Lyrikali Kuonekana na Mrembo

Mashabiki Wapagawa Baada ya Toxic Lyrikali Kuonekana na Mrembo

Msanii anayetikisa anga la muziki kwa sasa nchini Kenya, Toxic Lyrikali, ameibua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kushiriki kipande cha video kwenye Instagram Story akionekana akiwa kwenye mahaba mazito na mrembo asiyejulikana. Katika video hiyo, Toxic na mrembo huyo wameonekana wakifurahia ukaribu wao bila kujificha, jambo ambalo limezidisha tetesi za kimapenzi. Baadhi ya mashabiki wanasema huenda huyo ndiye mpenzi wake mpya, hasa ikizingatiwa kwamba msanii huyo hana mazoea ya kuweka warembo wala kuonyesha maisha yake ya mapenzi mitandaoni. Hata hivyo, wengine wanahisi inaweza kuwa sehemu ya maandalizi ya kazi yake mpya. Inadaiwa kuwa Toxic Lyrikali anajiandaa kuachia wimbo unaoitwa Hide & Sick akimshirikisha Mjaka Wa Fine, na kwamba tukio hilo linaweza kuwa sehemu ya kuikuza kazi hiyo kabla ya kuachiwa rasmi. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kwa shauku kuona kama video hiyo ilikuwa ishara ya mapenzi mapya au ni mbinu ya kuibua msisimko kuelekea ujio wa kazi yake mpya. Msanii huyo bado hajatoa tamko lolote kuhusu video hiyo.

Read More
 Toxic Lyrikali Afunguka Kuhusu Bifu ya Eastlands na Nairobi West

Toxic Lyrikali Afunguka Kuhusu Bifu ya Eastlands na Nairobi West

Msanii na rapper Toxic Lyrikali amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu bifu inayodaiwa kuendelea kati ya vijana wa Nairobi West na Eastlands, akitaka tofauti hizo kukomeshwa na vijana waelekeze nguvu kwenye shughuli za kujijenga kimaisha. Katika ujumbe wake kwa mashabiki kwenye moja ya show yake, Toxic Lyrikali ameweka wazi kuwa mvutano wa maeneo hautoi faida yoyote kwa vijana, na badala yake unawazuia kuona fursa muhimu zinazoweza kubadili maisha yao. Mkali huyo wa ngoma ya Euphoria, amesisitiza kuwa vijana wanapaswa kufikiria zaidi kuhusu kutafuta kipato, kubuni miradi na kujenga mustakabali imara badala ya kuendeleza bifu zisizo na tija. Kauli yake imepokelewa kwa msisimko kwenye mitandao ya kijamii, ambapo wadau wa muziki na mashabiki wamempongeza kwa kuonyesha uongozi na kutoa wito wa umoja. Wengi wamesema kuwa ujumbe huo unawatia moyo vijana kuachana na tofauti za maeneo ambazo mara nyingi huibua migogoro ya kijamii.

Read More
 Rapa Toxic Lyrikali Adharau Diss Track ya Wakuu Music

Rapa Toxic Lyrikali Adharau Diss Track ya Wakuu Music

Rapa anayeongoza katika chati za muziki nchini Kenya, Toxic Lyrikali, amepuuza kwa dharau ‘diss track’ iliyomlenga iliyotolewa na kundi la Wakuu Music, akieleza kuwa hana muda wa kujibu migogoro inayoendeshwa na wivu na chuki kutokana na mafanikio yake. Kupitia Instagram Live, Toxic Lyrikali amesema wazi kuwa hawezi kamwe kujibu diss track kutoka kwa wasanii ambao “hata hawana blue tick,” akimaanisha hawathibitishwi au kutambulika rasmi kwenye mitandao ya kijamii. Akieleza sababu ya kutojibu kwa wimbo, Lyrikali amesema hatua yake haitokani na kushindwa, bali ni kutokana na ukweli kwamba ‘diss track’ ya Wakuu Music haikidhi viwango vya rap. Rapa huyo ametoa wito kwa wasanii wote wanaotaka kumkosoa kwa nyimbo kutafuta mashairi yenye uzito na pointi za maana badala ya kujidhalilisha na diss tracks ambazo hazina uzito. Hata hivyo amewashukuru mashabiki wake kwa sapoti kubwa anayoipata, akiwahakikishia kuwa kutojibu kwake hakuleti shaka yoyote kuhusu uwezo wake kwani kazi yake ndiyo jibu lake kuu. Wakuu Music walikuwa wameachia diss track hiyo maalum wakimtaka Toxic Lyrikali ajibu kwa mashairi, lakini amekataa kabisa kuingia kwenye vita ya maneno akisema hajishughulishi na wasanii wanaotafuta kiki kupitia jina lake.

Read More
 Bifu Kati ya VJ Patelo na Toxic Lyrikali Yapamba Moto Mtandaoni

Bifu Kati ya VJ Patelo na Toxic Lyrikali Yapamba Moto Mtandaoni

Vita vya maneno kati ya VJ Patelo na rapa Toxic Lyrikali vimechacha tena mtandaoni, safari hii vikihusisha majigambo ya fedha na vito vya thamani. Toxic Lyrikali ndiye alianza mashambulizi kupitia Instagram Live kwa kudai kuwa Patelo anaishi kwa kutegemea pesa za mke wake, Dee, jambo lililozua mjadala mkali kati ya mashabiki wao. Hata hivyo, Patelo hakusita kujibu. Kupitia mitandao ya kijamii, ameonyesha maisha yake ya kifahari na misururu ya minyororo ya thamani, huku akimkejeli Toxic kwa kusema kuwa minyororo yake ni “miyoo” (bandia). Mashabiki wa pande zote mbili wameendelea kutoa maoni tofauti, wengine wakimtetea Patelo kwa kudai anajitegemea, huku wengine wakisema Toxic Lyrikali alikuwa anasema ukweli kuhusu maisha ya VJ huyo. Vita hivyo vya maneno vinaonekana kuendelea, huku kila upande ukijaribu kuthibitisha nani ni “boss” halisi katika maisha ya kifahari.

Read More
 Bifu Laibuka Kati ya Toxic Lyrikali na Tipsy Gee Mtandaoni

Bifu Laibuka Kati ya Toxic Lyrikali na Tipsy Gee Mtandaoni

Rapa kutoka Kenya, Toxic Lyrikali, ameonyesha kutoridhishwa na skit iliyosambaa mtandaoni ikimuonesha mwenzake Tipsy Gee akijifananisha kuwa na mafanikio makubwa zaidi. Katika skit hiyo, Tipsy anaonekana akiendesha gari huku waigizaji waliobandikwa majina ya Toxic na Fathermoh wakiendesha bodaboda, jambo lililotafsiriwa kama kejeli kwao. Kupitia Instagram Toxic amechukizwa na kejeli hiyo na kumtaka Tipsy kuacha mbwembwe na kurudi studio kutoa muziki. Amesema wazi kuwa Tipsy amekuwa akiendesha maigizo mtandaoni badala ya kufanya kazi ya muziki, akimtupia lawama kuwa amegeuka kuwa TikToker anayejali kiki kuliko kutoa ngoma mpya. Kauli ya Toxic imekuja mara baada ya Tipsy Gee, kumtolea uvivu, akidai kwamba licha ya Toxic kumpuuza, yeye ndiye msanii aliye na mafanikio zaidi japo amekaa kwenye tasnia kwa mwaka mmoja pekee.

Read More
 Mashabiki Wamshinikiza Toxic Lyrikali Kuachana na Nyimbo za Mahaba

Mashabiki Wamshinikiza Toxic Lyrikali Kuachana na Nyimbo za Mahaba

Msanii wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Toxic Lyrikali, yuko chini ya shinikizo kutoka kwa mashabiki wake baada ya kuachia nyimbo mbili za mahaba, “Bud Flowers” na “Mpenzi” aliyomshirikisha mwanamuziki Bridget Blue. Mashabiki wengi wamejitokeza kwenye mitandao ya kijamii wakimtaka arejee kwenye mtindo wake wa zamani wa hardcore gangster rap uliomtambulisha kwenye muziki wa hip hop. Wanaeleza kuwa Toxic Lyrikali alijijengea jina kutokana na mistari mikali yenye simulizi za maisha ya mtaani, hivyo kuingia kwenye muziki wa mapenzi kunahatarisha utambulisho wake wa kisanii. Baadhi ya mashabiki wameeleza hisia zao kwa kusema kuwa nyimbo za mahaba hazimpendezi msanii huyo, na kwamba anafuata mkumbo wa soko badala ya kudumisha uhalisia wake. Wengine, hata hivyo, wamesema ni kawaida kwa msanii kubadilika na kupanua wigo wa muziki wake ili kufikia hadhira pana zaidi. Wachambuzi wa tasnia ya muziki wanaona mwelekeo huu unaweza kuwa ni mkakati wa kibiashara, lakini shinikizo la mashabiki linaweza kumlazimisha Toxic Lyrikali kurudi kwenye midundo ya rap kali aliyozoeleka nayo. Kwa sasa, macho na masikio ya mashabiki yapo kwa Toxic Lyrikali ili kubaini iwapo ataendelea kusimama na mwelekeo wa nyimbo za mahaba, au atasikiliza wito wa mashabiki wake na kurudi kwenye muziki wa mitaani uliomtambulisha.

Read More
 Wimbo wa “Chinje” wa Toxic Lyrikali Waweka Historia Youtube

Wimbo wa “Chinje” wa Toxic Lyrikali Waweka Historia Youtube

Rapa anayekuja kwa kasi nchini Kenya, Toxic Lyrikali, ameandika historia baada ya wimbo wake “Chinje” kufikisha views milioni 10 kwenye mtandao wa YouTube ndani ya kipindi cha miezi tisa tangu uachiwe rasmi. Takwimu hizi zimempa nafasi kubwa katika muziki wa Afrika Mashariki, zikimuweka kwenye ramani kama moja ya vipaji vipya vinavyoibuka kwa nguvu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Toxic Lyrikali ametoa shukrani kwa mashabiki wake wote waliomuunga mkono, akisisitiza kuwa mafanikio hayo yasingewezekana bila upendo na uaminifu wao. Aidha, ameahidi kuendelea kuwapa mashabiki wake ngoma kali zaidi katika siku zijazo. Wimbo “Chinje” umekuwa gumzo kwa mashabiki kutokana na midundo yake ya kipekee na ujumbe unaoendana na ladha ya muziki wa kizazi kipya. Wachambuzi wa muziki wanaona mafanikio haya kama kielelezo cha jinsi wasanii wapya wanavyoweza kufika mbali kwa kutumia mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali.

Read More