Trey Songz Achunguzwa kwa Madai ya Kumshambulia Mpiga Picha New York

Trey Songz Achunguzwa kwa Madai ya Kumshambulia Mpiga Picha New York

Msanii maarufu wa R&B, Trey Songz, anachunguzwa na polisi kwa madai ya kumshambulia mpiga picha kwenye mgahawa wa The Ivy mjini New York, tukio lililotokea Jumapili asubuhi. Kwa mujibu wa ripoti ya TMZ, mpiga picha aitwaye Isaa Mansoor anadai kuwa alipewa kazi rasmi ya kurekodi matukio ya Trey Songz ikiwemo picha na video ndani ya mgahawa huo. Isaa anasema Trey alifahamu vyema kuwa kulikuwa na kamera mahali hapo, na kwamba kazi hiyo ilikuwa ya maandalizi. Hata hivyo, hali ilibadilika ghafla baada ya mashabiki kuanza kumuomba Trey kupiga nao picha. Inadaiwa kwamba msanii huyo alionekana kukerwa na hali hiyo. Baadaye, wakati mmiliki wa mgahawa alipomwomba apige picha ya mwisho mbele ya nembo ya mgahawa huo, ndipo ghasia zilipozuka. Isaa anadai kuwa Trey alimchapa ngumi kichwani bila tahadhari, akamsukuma ukutani na kuvunja kamera zake mbili za kazi. Tukio hilo limewasilishwa kwa polisi wa New York na uchunguzi rasmi unaendelea. Hadi sasa, Trey Songz bado hajatoa tamko lolote rasmi kuhusiana na madai haya.

Read More
 Trey Songz Aibua Taharuki Mitandaoni Baada ya Kumfokea Shabiki Hadharani

Trey Songz Aibua Taharuki Mitandaoni Baada ya Kumfokea Shabiki Hadharani

Msanii maarufu wa muziki wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, ameibuka tena kwenye vichwa vya habari baada ya video kusambaa mitandaoni ikimuonesha akiwa katika hali ya hasira kali dhidi ya shabiki mmoja. Tukio hilo liliripotiwa kutokea usiku wa Jumanne, Juni 24, 2025, katika eneo lisilotajwa wazi. Katika video hiyo ambayo kwa sasa imeenea kwenye mitandao ya kijamii kama The Shade Room, HotNewHipHop, na The Jasmine Brand, Trey Songz anaonekana akikabiliwa na matusi na dharau kutoka kwa shabiki aliyekataa kumsalimia.  “I’ll beat the sh*t out of you right now!,” Trey, alisikika akisema kwa hasira. Kauli hiyo ilionekana kutolewa mara baada ya shabiki huyo kumwita jina la matusi, huku akimkataa kwa dharau mbele ya umati. Muda mfupi baadaye, walinzi wa msanii huyo waliingilia kati na kuzuia uwezekano wa mzozo mkubwa kutokea. Tukio hili limezua mjadala mkubwa mitandaoni. Mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii wametoa maoni tofauti; baadhi wakimtetea msanii huyo kwa kusema alichokifanya kilikuwa ni kutetea heshima yake, huku wengine wakimlaumu kwa kushindwa kujizuia na kuonyesha ukomavu wa hali ya juu kama mtu maarufu. Hii si mara ya kwanza kwa Trey Songz kujikuta kwenye hali ya utata. Mnamo mwaka 2016, msanii huyo alikamatwa kwa kushambulia afisa wa polisi wakati wa tamasha mjini Detroit. Mwaka 2021, alishtakiwa kwa madai ya unyanyasaji wa kingono – kesi ambayo baadaye ilitupiliwa mbali. Visa vya ukosefu wa nidhamu vimekuwa vikimfuata mara kwa mara, jambo ambalo linazua maswali kuhusu jinsi anavyokabiliana na umaarufu na changamoto za maisha ya hadharani. Mpaka kufikia sasa, Trey Songz hajatoa tamko lolote rasmi kuhusu tukio hilo. Pia, hakuna taarifa yoyote kutoka kwa polisi au vyombo vya sheria vinavyohusiana na tukio hilo. Wakala wake pia hajatoa maelezo yoyote. Tukio hili limezua hisia mseto kuhusu tabia ya wasanii mashuhuri wanapokabiliwa na kejeli au uchokozi kutoka kwa mashabiki. Trey Songz bado anasalia kuwa mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa katika muziki wa R&B, lakini matukio kama haya yanaweza kuathiri taswira yake hadharani ikiwa hayatadhibitiwa kwa hekima.

Read More
 Trey Songz ajisalimisha kwa polisi New York

Trey Songz ajisalimisha kwa polisi New York

Nyota wa R&B kutoka Marekani Trey Songz amejikabidhi mwenyewe mikononi mwa polisi wa mjini New York kwa ajili ya kukabiliana na madai ya kuwapiga watu wawili. Ripoti za awali zinasema kwamba Trey Songz alitembeza kipigo kwa mwanamke mmoja huku akimburuza kwa kuvuta nywele zake huko mjini new york, marekani lakini sasa mamlaka zinadai kwamba kulikuwa na mhanga mwingine ambaye alifikiwa na ngumi ya mwimbaji huyo na hivyo kuwa wawili. Hivyo Trey Songz ametakiwa kwenda kusimama kizimbani kwenye mahakama kufuatia madai hayo. Mwanasheria wake aitwaye “mitch schuster” ameweka kifua mbele kwa kusema kwamba yeye yupo tayari kwa lolote lile.

Read More
 TREY SONGZ AZIDI KUANDAMWA NA TUHUMA ZA UDHALILISHAJI

TREY SONGZ AZIDI KUANDAMWA NA TUHUMA ZA UDHALILISHAJI

Mwanamuziki kutoka Marekani Trey Songz anazidi kuandamwa na tuhuma za udhalilishaji baada ya tuhuma ya ubakaji pamoja na unyanyasaji wa kingono zilizotoka Februari mwaka huu, sasa limeibuka shtaka lingine jipya dhidi yake. Kwa mujibu wa TMZ, mwimbaji huyo maarufu duniani kwasasa anadaiwa fidia kwa tukio alilolifanya mwaka 2013 baada ya video ya tukio hilo kusambaa hivi karibuni. Trey Songz kwenye video hiyo anaonekana kulitoa nje titi la mwanamke mmoja aliyehudhuria party ambayo yeye (Trey Songz) ndiye alikuwa host wa party hiyo iliyofanyika kwenye casino la Foxwoods Resort huko Ledyard. Mwanamke huyo alietambulika kwa jina la Megan Johnson sasa anataka fidia ya mamilioni ya pesa, anadai fidia ya $5 Milioni. Barua kutoka kwa mawakili wa Megan Johnson, Trey Songz anatuhumiwa kwa unyanyasaji wa kijinsia na kupuuza usalama wake bila kujali. Kwenye maelezo yake Megan Johnson amedai kuwa alikuwa amemuomba rafiki yake ampige picha Trey Songz alipokuwa nyuma yake ndipo Trey alipomshika na kufanya kitendo hicho cha udhalilishaji.

Read More
 TREY SONGZ KWENYE TUHUMA NYINGINE YA UBAKAJI, ADAIWA KUMUINGILIA KINYUME NA MAUMBILE MWANAMKE MMOJA

TREY SONGZ KWENYE TUHUMA NYINGINE YA UBAKAJI, ADAIWA KUMUINGILIA KINYUME NA MAUMBILE MWANAMKE MMOJA

Staa wa muziki kutoka nchini Marekani Trey Songz anazidi kuandamwa na tuhuma za ubakaji pamoja na unyanyasaji wa kingono, mwanamke wa tatu amejitokeza na kudai fidia ya shilling billion 2.3 za Kenya  kwa madai ya kubakwa na kuingiliwa kinyume na maumbile. Kwa mujibu wa TMZ, shauri hilo lilifunguliwa Februari 15 mwaka huu ambapo mwanamke huyo alisema Trey Songz alimwalika kwenye party katika nyumba moja mjini Los Angeles, baadaye alimpeleka chumbani wakiwa na makubaliano ya kufanya mapenzi kawaida. Walipofika chumbani, Trey Songz alimsukuma chini na kuanza kumlazimisha kumuingilia kinyume na maumbile, baada ya kupambana kujioka kwenye mikono ya mkali huyo wa R&B, mwanamke huyo anasema alizidiwa nguvu na Trey songz na hivyo akamuingilia kinyume na maumbile kwa nguvu.

Read More