Trey Songz Akamatwa kwa Kumpiga Mfanyikazi wa Klabu ya Usiku New York
Msanii wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa usalama kufuatia tukio la vurugu lililotokea katika klabu moja ya usiku jijini New York City. Kwa mujibu wa taarifa zilizowasilishwa katika mahakama ya jinai ya Manhattan, tukio hilo lilitokea Desemba 4 katika Dramma Night Club, eneo la Times Square. Trey Songz na kundi lake walikuwa wakifurahia burudani hadi pale mfanyakazi wa klabu alipowaarifu kuwa klabu ilikuwa ikifungwa majira ya saa kumi alfajiri. Waendesha mashtaka wanadai kuwa msanii huyo mwenye umri wa miaka 41 na watu wake walionekana kukerwa kupita kiasi bila sababu ya msingi, hali iliyosababisha mvutano. Inadaiwa kuwa Trey Songz alimpiga mfanyakazi huyo ngumi za usoni, tukio lililomsababisha kuvimba na kupata maumivu makali mwilini. Baada ya tukio hilo, Trey Songz alifikishwa mahakamani Jumapili, akikabiliwa na kesi ya shambulio kuhusiana na tukio la klabu hiyo ambapo kesi yake itatajwa tena mwezi Februari 2026. Ikumbukwe, Trey Songz anakabiliwa pia na kosa la uharibifu wa mali (second-degree mischief) linalohusishwa na tukio jingine ambalo maelezo yake bado hayajawekwa wazi.
Read More