TYGA NA ROB KARDASHIAN WAMCHANA BLAC CHYNA BAADA YA KUSEMA HAPEWI PESA ZA MATUNZO YA WATOTO

TYGA NA ROB KARDASHIAN WAMCHANA BLAC CHYNA BAADA YA KUSEMA HAPEWI PESA ZA MATUNZO YA WATOTO

Rapa kutoka Marekani Tyga pamoja na Rob Kardashian wameamua kwa pamoja kumtolea uvivu Blac Chyna ambaye ni mama wa watoto wao baada ya kusema hadharani kwamba hapewi pesa za matunzo ya watoto na ameamua kuuza magari yake matatu kwa ajili ya kupata pesa za kujikimu. Tyga ambaye ana mtoto mmoja na Chyna (King Cairo Stevenson) alikuwa wa kwanza kuibuka kwenye comment katika post hiyo ya Blac Chyna ambayo imepostiwa kwenye ukurasa wa The Shaderoom Instagram, kwa kuandika ujumbe unaosomeka  “Nalipa ($40K) zaidi ya shilling million 4.6 kwa mwaka kwa ajili ya Ada ya mtoto wangu shule, na ninaishi naye toka Jumatatu hadi Jumamosi. Kwanini nilipe pesa za matunzo ya mtoto.” aliandika Tyga na kumalizia kwa kicheko. Rob Kardashian ambaye pia wamezaa mtoto mmoja (Dream Renèe Kardashian) alikuja na kuacha comment yake isemayo “Nalipa ($37k) zaidi ya shilling million 4.3 za Kenya kwa mwaka kama Ada ya shule ya binti yangu. Ninasimamia gharama zote za matibabu. Nalipa gharama zote za ziada kwa binti yangu. Ninakuwa naye kuanzia Jumanne hadi Jumamosi. Kwanini nilipe pesa ya matunzo ya mtoto.” aliandika Rob Kardashian.

Read More
 KESI YA TYGA KUMPIGA EX WAKE CAMARYN SWANSON YATUPILIWA MBALI

KESI YA TYGA KUMPIGA EX WAKE CAMARYN SWANSON YATUPILIWA MBALI

Staa wa muziki kutoka nchini Marekani Tyga hatashtakiwa kwa makosa ya jinai katika kesi yake ya unyanyasaji wa nyumbani dhidi ya mpenzi wake wa zamani Camaryn Swanson. Mapema wiki hii TMZ imeripoti kwamba kesi ya Tyga itasikilizwa katika Ofisi ya Mwanasheria wa Jiji la Los Angeles, ambapo atajadili jinsi ya kushughulikia migogoro ya nyumbani. Hapo awali, iliripotiwa kuwa Tyga bado anaweza kushtakiwa kwa kosa la kumpiga makonde mpenzi wake wa zamani Camaryn Swanson kutokana na madai ya ugomvi kati yake na mpenzi wake Huyo uliotokea Oktoba Mwaka Jana.

Read More
 TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

Rapa kutoka nchini Marekani Tyga amefunguka kuhusu taarifa za kufunguliwa mashtaka kwa madai ya kumpiga ex wake Camaryn Swanson, Jumatatu wiki iliyopita. Tyga alijisalimisha kwenye mikono ya polisi mjini Los Angeles Jumanne  wiki iliyopita ambapo Tovuti ya TMZ ilidai kwamba tayari amefunguliwa mashtaka ya unyanyasaji wa nyumbani. Sasa baada ya kimya cha muda mfupi, Tyga ameamua kuweka wazi sakata hilo. Kupitia ukurasa wake wa instagram rapa huyo amekanusha kwa kusema madai hayo hayana ukweli wowote, kwani hakukamatwa na polisi na wala hakufunguliwa mashtaka yoyote bali alifika kituo hapo kujieleza. Kwa mujibu wa nyaraka za polisi wa Los Angeles, zinaonesha Michael Stevenson maarufu Tyga alishtakiwa kwa makosa ya uhalifu mnamo Oktoba 12 mwaka huu na aliachiwa masaa machache baadaye kwa dhamana ya shillingi millioni 5.5 za kenya.

Read More
 TYGA AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUMPIGA EX GIRLFRIEND WAKE

TYGA AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUMPIGA EX GIRLFRIEND WAKE

Staa wa muziki kutoka marekani Tyga amefunguliwa mashtaka kwa kumpiga mpenzi wake wa zamani Camaryn Swanson. Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ, mrembo huyo alifika nyumbani kwa Tyga mishale ya saa 9 usiku Jumatatu wiki ambapo awali aliambiwa asifike nyumbani hapo. Taarifa zinaeleza kwamba Camaryn alikuwa amelewa, lakini Tyga alimruhusu aingie ndani kwa ajili ya kuzungumza naye. Baadaye zilianza kusikika kelele za Camaryn ambaye ameiambia polisi kwamba Tyga alikuwa akimrushia ngumi wakati wa majibizano yao. Mama yake mzazi alifika na kumchukua kisha kuwapigia simu polisi kutoa taarifa. Polisi walifika nyumbani kwa Tyga siku hiyo hiyo kwa ajili ya uchunguzi na Tyga ameripotiwa kuandikisha kutoa maelezo kwa upande wake ikiwa tayari amefunguliwa kesi ya unyanyasaji wa nyumbani. Camaryn ame-share picha zake za majeraha baada ya tukio hilo.

Read More