Ziza Bafana Akanusha Taarifa za Ugomvi na Kalifah Aganaga

Ziza Bafana Akanusha Taarifa za Ugomvi na Kalifah Aganaga

Msanii wa muziki wa dancehall kutoka Uganda, Ziza Bafana, amefunguka kuhusu uhusiano wake na mwanamuziki mwenzake Kalifah Aganaga, akisema kwamba amekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Aganaga katika tasnia ya muziki. Akizungumza katika mahojiano na Sanyuka Television, Ziza Bafana alikanusha madai kuwa alimshambulia Kalifah kwa maneno au kumdharau, akieleza kuwa alieleweka vibaya. Alisisitiza kuwa hana chuki yoyote dhidi ya Aganaga na hata hawezi kumkosea heshima. “Nilieleweka vibaya kwa sababu mimi binafsi sina ubaya wowote na Kalifah Aganaga. Sina nia mbaya kabisa. Kalifah ni kama ndugu yangu, na mimi ni mmoja wa watu waliomsaidia katika kujenga kazi yake ya muziki. Siwezi kumdharau,” alisema Bafana. Ziza Bafana na Kalifah Aganaga wote ni wasanii wakongwe kwenye muziki wa Uganda na wamewahi kushirikiana kwenye majukwaa mbalimbali. Kauli ya Bafana imekuja wakati ambapo mashabiki wamekuwa wakizungumzia uwezekano wa mgogoro kati yao, hali ambayo sasa inaonekana kufutwa na maelezo hayo ya amani. Mashabiki wamepokea taarifa hiyo kwa hisia tofauti, baadhi wakimtaka Bafana na Aganaga kurejea studio pamoja kama zamani, huku wengine wakisisitiza umuhimu wa umoja miongoni mwa wasanii wa Uganda.

Read More
 Eddy Kenzo Apuzilia Mbali Madai ya Bebe Cool ya Kudhibiti Muziki

Eddy Kenzo Apuzilia Mbali Madai ya Bebe Cool ya Kudhibiti Muziki

Msanii nyota wa Uganda, Eddy Kenzo, ameibuka na kauli kali dhidi ya madai ya Bebe Cool kwamba yeye hudhibiti namna nyimbo zinavyopigwa kwenye redio na runinga nchini humo. Kenzo, ambaye ni miongoni mwa wasanii waliofanikiwa kimataifa kutoka Afrika Mashariki, amesema Bebe Cool hana ushawishi mkubwa kama anavyodai. “Bebe Cool hana uwezo wa kudhibiti airplay kama anavyodhani. Sisi tulipata mafanikio makubwa wakati yeye bado yupo kwenye tasnia, kwa hiyo kauli zake hazina uzito wowote,” alisema Kenzo katika mahojiano na msanii Vampino. Kauli hii ni majibu ya moja kwa moja kwa matamshi ya Bebe Cool aliyotoa mwezi Aprili, ambapo alijisifu kuwa ana ushawishi mkubwa kwenye vituo vya habari na anaweza kuzuia wimbo wowote usipigwe Uganda. “Mimi si rafiki tu wa DJs, bali pia wa wamiliki wa vituo vya redio na TV. Naweza kuamua wimbo gani usipigwe popote nchini,” alisema Bebe Cool awali, akidai wasanii wachanga wanafaa kumheshimu kama mlezi wa tasnia. Lakini kwa Eddy Kenzo, mafanikio hayatokani na upendeleo au vitisho vya watu maarufu bali kutokana na bidii, kipaji na kujituma kwa msanii binafsi. “Wasanii wapya wasihangaike na matamshi kama haya. Wajikite kwenye kazi yao. Mafanikio hayaletiwi na maneno ya mtu bali kazi nzuri,” alisisitiza Kenzo. Bifu hili la kauli kati ya mastaa hawa wawili linaashiria mvutano mkubwa wa ushawishi ndani ya tasnia ya muziki nchini Uganda, huku mashabiki wakigawanyika kati ya kuunga mkono upande wa Kenzo au Bebe Cool. Lakini kwa sasa, Kenzo ameweka wazi msimamo wake kwamba hana muda wa kuendekeza maneno yasiyo na msingi.

Read More
 Spice Diana Afichua Siri Nzito ya Uchawi Miongoni mwa Wasanii Uganda

Spice Diana Afichua Siri Nzito ya Uchawi Miongoni mwa Wasanii Uganda

Msanii maarufu wa Uganda, Spice Diana, ametikisa tasnia ya burudani kwa madai mazito ya kuwepo kwa uchawi miongoni mwa wanamuziki. Katika mahojiano a Galaxy TV, msanii huyo wa “Source Management” alieleza kuwa baadhi ya wasanii hutumia nguvu za giza kwa lengo la kudhoofisha na kuvuruga mafanikio ya wenzao. “Watu wanafanya kazi kwa bidii gizani kuhakikisha wanaharibu kazi za wenzao. Tuwe wakweli – haya mambo yapo,” alisema Spice Diana kwa msisitizo Licha ya kuwa na imani kwamba uchawi upo katika sekta ya muziki, Spice Diana anasema hajawahi kuathirika moja kwa moja na uchawi huo. Anaamini kuwa nguvu ya maombi kutoka kwa mashabiki wake na imani yake kwa Mungu ndiyo ngao yake. “Labda mtu alijaribu kuniroga lakini akashindwa. Mungu amenilinda kupitia maombi ya mashabiki wangu wengi,” alisema. Hata hivyo, msanii huyo aliongeza kuwa si kila changamoto inayompata msanii ina uhusiano na uchawi. Alisisitiza kuwa matatizo ya kawaida ya kibinadamu pia huwapata wasanii kama watu wengine. “Wakati mwingine tunapitia matatizo ya kawaida kama binadamu wengine, lakini tunadhani tumerogwa. Ndio maana sitaki kila tatizo ninalopitia niunganishe na uchawi,” alieleza. Kauli ya Spice Diana imezua mijadala mikali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, huku baadhi wakimsifu kwa ujasiri wake wa kusema ukweli, na wengine wakihofia kuwa madai hayo yanaweza kuongeza hofu na chuki miongoni mwa wasanii. Hili si tukio la kwanza kwa madai ya aina hiyo kusikika. Wasanii wengine kama Zanie Brown na Grace Nakimera pia wamewahi kuelezea masaibu waliyopitia kutokana na kile walichodai kuwa ni hujuma za kishirikina kutoka kwa wenzao katika muziki.

Read More