“Sihitaji Pesa, Nahitaji Fursa” – Msanii Visita Aomba Msaada wa Vifaa

“Sihitaji Pesa, Nahitaji Fursa” – Msanii Visita Aomba Msaada wa Vifaa

Msanii maarufu Visita, ambaye amewahi kung’ara kwenye tasnia ya muziki nchini Kenya, ameacha wengi wakiwa na huzuni na mshangao baada ya kufichua changamoto kali za maisha alizopitia, ambazo zilimsukuma hadi katika hali ya msongo wa mawazo na kuishi maisha ya uraiani kwa muda. Akizungumza katika mahojiano ya kipekee na Obinna TV, Visita alisema maisha yalibadilika ghafla na kuanza kumlemea, hali iliyomfanya ajikute akilala nje, akiwa na njaa na kufungiwa nyumba kwa miezi mitatu. “Nilifikia hatua mbaya sana kimaisha. Nilikua na njaa, nimefungiwa nyumba kwa miezi mitatu, sina pa kwenda. Nilihisi nimevunjika kabisa, lakini ndani yangu nilijua siwezi kubaki hapo nilikua napambana na nafsi yangu kila siku,” Visita alieleza kwa uchungu. Akiwa na uso wa matumaini lakini uliobeba maumivu ya ndani, Visita alisema alipitia hali ya kukosa chakula kwa siku kadhaa hadi majirani walipoanza kumsaidia chakula na mahitaji ya msingi. Hali hiyo iliendelea hadi msamaria mwema mmoja alipojitokeza na kumpatia chumba kidogo cha kujishikilia, si biashara, bali sehemu ya kujisitiri kwa muda huku akijaribu kujijenga upya. “Yule msamaria aliniona nimeishiwa, akanipa chumba kidogo cha kutumia kama makazi. Ndicho ninachoishi sasa, na ndicho kimenisaidia nisiangamie kabisa,” alisema kwa sauti ya shukrani. Visita, ambaye hapo awali alikuwa mmoja wa wasanii waliotoa burudani kwa nguvu katika majukwaa ya muziki, anasema ikiwa angepata vifaa vya muziki kama spika, laptop au mixer hata vya bei nafuu au vilivyotumika (second-hand), anaweza kuanza kufanya kazi ya muziki tena na kujipatia kipato cha kulipa kodi, kula, na hata kujiendeleza. “Naamini nikisaidiwa hata na vifaa vya second-hand, naweza kujimudu, kujilipa kodi na kupata chakula. Sitaki kurudi tena kule nilikotoka,” aliongeza kwa matumaini. Kwa sasa, Visita anaendelea kuishi kwa neema ya watu wachache wanaomuunga mkono, huku akitoa wito kwa wasamaria wema na mashirika ya sanaa kumsaidia arudi kwenye miguu yake. Ameeleza kuwa bado ana kipaji na ndoto za kubadilisha maisha yake na hata kuwatia moyo vijana wengine wanaokumbana na changamoto kama zake. Iwapo ungependa kumsaidia Visita, unaweza kuwasiliana naye kupitia maelezo ya mawasiliano aliyoyatoa kwa Obinna TV au kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Read More
 HITMAKER WA “MAPEPO” VISITA AFILISIKA KIUCHUMI, AOMBA MSAADA KWA WAHISANI.

HITMAKER WA “MAPEPO” VISITA AFILISIKA KIUCHUMI, AOMBA MSAADA KWA WAHISANI.

Msanii tajika nchini Visita ametoa wito kwa wahisani kumsaidia kifedha kwani amefilisika kiuchumi na hana mahala pakuishi. Akiwa kwenye moja ya interview visita amesema kwa sasa anaishi kwenye studio ya kurekodia muziki inayomilikiwa na rafiki yake mmoja. Hitmaker huyo wa Mapepo amesema alifurushwa kwenye  nyumba aliyokuwa akiishi kutokana na malimbikizi ya kodi aliyokuwa akidaiwa. Mwezi Mei mwaka huu rapa huyo alichangiwa pesa na wasanii wenzake pamoja na marafiki mara  baada ya kushindwa kulipa gharama ya matibabu alipokuwa amelezwa hospitalini. Visita ni moja kati ya wasanii walioacha alama kwenye tasnia ya muziki nchini na anafahamika na hits kama Mapepo,Dawa ya moto, Dumbala Remix, Hivo ndio Kunaendanga, Fimbo na nyingine kibao. Ikumbukwe tangu ujio wa msala wa corona wasanii wengi  nchini wameathirika kiuchumi na kimawazo baada ya kufungiwa matamasha ya muziki ambayo wamekuwa wakitegemea kuchuma riziki.

Read More