VIVIAN AWAPA SOMO WASANII WA KIKE NCHINI KENYA
Msanii nyota nchini Vivian amewapa somo mastaa wa kike kwa kuwataka wajitume ili kujiletea maendeleo kwa kuwa muda wa kutumiwa kingono na wanaume umepita. Akizungumza na Mungai Eve, Vivian amesema kuwa baadhi ya wasanii wamekuwa wakijiweka nyuma na wakati mwingine kukubali kutumiwa kingono ili watoke wakati uwezo wanao. Vivian ambaye anafanya vizuri na wimbo wake uitwao Chachisha aliomshirikisha Sosuun amesema dhana ya mwanamke shujaa kwake ni yule anayepambana kufanikisha kila kitu huku akisisitiza kwamba mwanamke anaweza kuwa kiongozi, mwalimu au kufanya kazi yoyote iwapo akidhamiria kupambana. Hata hivyo amewataka wanawake kuondoa dhana ya kuwezeshwa na badala yake wapambane kutunza uanamke wao.
Read More