Msanii Diamond Afunguka Kuhusu Kipaji Chake cha Kuandika Mashairi

Msanii Diamond Afunguka Kuhusu Kipaji Chake cha Kuandika Mashairi

Msanii nguli wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amefunguka wazi kuhusu kipaji chake cha kipekee katika uandishi wa nyimbo, akieleza kuwa hiyo ndiyo silaha yake kubwa katika mafanikio ya muziki wake. Kupitia mahojiano ya hivi karibuni, Diamond amesema ubora wake unajengwa zaidi na uwezo wake wa kuandika mashairi yenye hisia na ujumbe mzito, jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kupendwa na mashabiki ndani na nje ya Tanzania. “Watu wengi wanajua tu napiga shoo, naimba, lakini ukweli ni kwamba uandishi wa mashairi ndiyo silaha yangu kubwa. Hapo ndipo nguvu yangu ipo,” amesema Diamond. Ameeleza kuwa mbali na nyimbo zake binafsi, amekuwa akiandika pia nyimbo kwa wasanii wengine, hususan wale walioko chini ya lebo yake ya WCB Wasafi, lakini pia amewahi kusaidia wasanii wa nje ya lebo hiyo. Hata hivyo, hakutaja majina ya wasanii au nyimbo alizohusika nazo, lakini amesisitiza kwamba mchango wake katika uandishi wa nyimbo umechangia mafanikio ya wengi kwenye tasnia. Kauli hiyo inazidi kuthibitisha nafasi yake kama mmoja wa wasanii waandamizi na wabunifu zaidi katika muziki wa Afrika Mashariki, huku akiendelea kushika nafasi ya juu kwenye chati mbalimbali za muziki barani Afrika.

Read More
 Mbosso Avunja Ukimya: “Sijarudi Kijijini Kwa Sababu Maisha Yamenishinda”

Mbosso Avunja Ukimya: “Sijarudi Kijijini Kwa Sababu Maisha Yamenishinda”

Staa wa muziki wa Bongo Flava, Mbosso Khan, amejitokeza kufafanua madai yaliyoenea mitandaoni kuwa amerejea kijijini kwao Kibiti, mkoani Pwani, kwa sababu maisha yamekuwa magumu baada ya kuondoka katika lebo ya WCB Wasafi. Kupitia mahojiano na gazeti moja nchini Tanzania, Mbosso amesema kuwa tafsiri iliyotolewa na baadhi ya watu kuhusu picha zake akiwa kijijini ni ya kupotosha na haina ukweli wowote. “Wakati mwingine huwa nayafurahia sana maisha ya mitandaoni, na wakati mwingine yanakera sana. Mimi kwenda nyumbani kwetu Kibiti ndiyo maisha yangu yamekuwa magumu jamani? Inamaana kila anayeenda kwao basi mjini pamemshinda?” alihoji Mbosso kwa msisitizo. Msanii huyo ambaye amewahi kutamba na vibao kama “Amepotea”, na “Umechelewa”, aliongeza kuwa safari yake kwenda Kibiti haikuhusiana kabisa na hali ya maisha bali ilikuwa ni kwa ajili ya kutembelea familia, marafiki, na kushughulikia mambo mengine nje ya muziki.  “Nimeenda kule kwa sababu kuna ndugu, jamaa na shughuli nyingine huwa nazifanya kule mbali na muziki. Hii haimaanishi kuwa nimefilisika au maisha yamenibana,” alisema. Aidha, Mbosso alizungumzia ukimya wake katika tasnia ya muziki tangu aondoke WCB, akieleza kuwa yuko kwenye kipindi cha maandalizi na mipango ya kimuziki kwa umakini zaidi. “Mashabiki wasiwe na shaka. Kazi zipo tayari na zingine bado zinaendelea kutengenezwa. Nimeamua kujipa muda ili nije kwa kishindo,” alieleza kwa kujiamini. Kauli ya Mbosso imepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki mitandaoni, huku wengi wakionesha kuungwa mkono kwa uamuzi wake wa kutetea heshima yake na kufafanua ukweli kuhusu maisha yake baada ya kuondoka Wasafi. Kwa sasa, mashabiki wake wanasubiri kwa hamu kazi mpya kutoka kwake, wakitumaini kuwa atarejea kwenye chati za muziki kwa kishindo kama alivyoahidi.

Read More