Weezdom Amkosoa Bahati kwa Kuvaa Mavazi ya Mkewe

Weezdom Amkosoa Bahati kwa Kuvaa Mavazi ya Mkewe

Msanii wa zamani wa muziki wa injili na meneja wa burudani, Weezdom, ameeleza masikitiko yake kuhusu mwenendo wa msanii Bahati, ambaye kwa sasa amegeukia maudhui yenye utata mtandaoni. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram, Weezdom amesema Bahati alikuwa mfano bora wa kuigwa, hasa kwa vijana na familia, na aliwahi kutumia kipaji chake kueneza neno la Mungu kupitia muziki. Lakini sasa anahisi kuwa Bahati amepoteza dira na kusahau msingi wa mafanikio yake. “Sometimes naangalia vitu my mentor, msee mwenye alinifunza Word ya God, vitu anafanya kwa mitandao namhurumia sana. Juu hakuna brand ilishawahi kuwa na influence kubwa kwa wazazi na watoto wadogo zaidi ya huyu jamaa bana!” aliandika Weezdom kwa hisia. Weezdom, ambaye aliwahi kuwa mshirika wa karibu wa Bahati katika huduma ya muziki wa injili, aliongeza kuwa Bahati anapaswa kutafakari upya nafasi yake kama kielelezo kwa vijana na kurejea kwenye msingi wa kiimani uliomuinua kimaisha. Kauli hiyo inakuja baada ya video na picha za Bahati kusambaa mitandaoni zikimwonyesha akiwa amevaa nguo za mkewe, jambo lililoibua maoni mseto kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake. Ujumbe wa Weezdom umechochea mijadala mikubwa mitandaoni, wengi wakijiuliza iwapo Bahati anapaswa kurejea kwenye muziki wa injili au kuendelea na mwelekeo wake wa sasa wa burudani mchanganyiko. Mpaka sasa, Bahati hajatoa tamko lolote rasmi kujibu maoni ya Weezdom, lakini mashabiki wengi wanaendelea kuonyesha maoni yao tofauti kuhusu suala hilo, baadhi wakimtetea na wengine wakimtaka arejee kwenye msingi uliompa umaarufu.

Read More
 Weezdom akiri kupatwa na msongo wa mawazo kisa Bahati

Weezdom akiri kupatwa na msongo wa mawazo kisa Bahati

Msanii Weezdom amefunguka kupatwa na msongo wa mawazo baada ya kuachana na aliyekuwa bosi wake chini ya label ya EMB Records, Bahati. Kwenye mahojiano na Podcast ya EMM, amesema tangu uhusiano wake na Bahati kuingiwa na ukungu, ilikuwa vigumu kwake kujikimu kimaisha jambo lilimpelekea kuchukua maamuzi magumu na kuanza kubugua pombe kupindukia kama njia ya kukimbia changomoto za maisha. Msanii huyo amesema ulevi ulimfanya kupoteza mweelekeo kiasi cha kusahau kufanya muziki. Hata hivyo amesema anamshukuru mwenyezi Mungu kwa kumtoa kwenye tatizo la ulevi baada ya wasamaria wema kujitokeza na kumsaidia kuondokana na matumizi ya pombe.

Read More
 BIFU LA WEEZDOM NA MANZI WA TRM LACHUKUA SURA MPYA, WARUSHIANA MATUSI MTANDAONI

BIFU LA WEEZDOM NA MANZI WA TRM LACHUKUA SURA MPYA, WARUSHIANA MATUSI MTANDAONI

Msanii wa muziki Weezdom ameingia tena kwenye Headline kwenye mitandao ya kijamii kwa kumkingia kifua mpenzi wake Mylee Stacy baada ya mrembo aitwaye Manzi wa TRM kumchafua mtandaoni na kashfa za uongo. Kupitia kwenye mtandao wa Instagram Weezdom ameonekana kukasirishwa na kitendo cha Ex wake huyo kumchafua Mylee Stacy na stori za kutunga ambapo amemporomoshea matusi mazito Manzi wa TRM akimtaka akome kumzungumzia vibaya Mylee Stacy mtandaoni. Msanii huyo  amemtaka manzi trm akubali kwamba mahusiano yao yalivunjika kitambo badala ya kumkosesha Mylee Stacy Amani kwa kutumia jina lake kujitafutia umaarufu mtandaoni. Hata hivyo watumiaji wa mitandao ya kijamii wameonekana kutofurahisha na kitendo cha Weezdom kumtolea mambo mazito ex wake Manzi wa TRM ambapo wamemshauri wangetatua tofauti zao nje ya mitandao ya kijamii kwani wanajiahibisha wenyewe. Utakumbuka hatua ya weezdom kumshushia matusi Manzi wa TRM imekuja siku chache baada ya kumuomba msamaha mpenzi wake Mylee Stacy kwa kitendo cha kumporeshea matusi mazito mtandaoni ambapo alienda mbali zaidi na kuahapa kutorudia kitendo cha kuwavunjia wanawake heshima.

Read More
 WEEZDOM AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA MWANADADA CAROL LEEHAVI, ADAI UHUSIANO WAO ULIKUWA KIKI

WEEZDOM AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA MWANADADA CAROL LEEHAVI, ADAI UHUSIANO WAO ULIKUWA KIKI

Msanii wa muziki nchini Weezdom amekiri kutumia kiki kutangaza wimbo uitwao Wazae aliyoshirikishwa na Carol Leehavi Kupitia ukurasa wake wa Instagram Weezdom amesema hata uhusiano wake wa kimapenzi na mrembo huyo ulikuwa batili na ilikuwa ni njia ya kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye tasnia ya muziki nchini kenya. Msanii huyo ametangaza kurejea kwa kishindo kwenye muziki wake atakapoachia wimbo wake mpya  ambao  kwa mujibu wake hatatumia nguvu nyingi kuitangaza kwani ni moto wa kuotea mbali. Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wametilia shaka tamko lake hilo ikizingatiwa kuwa amekuwa mtu wa mzaha sana kwenye muziki wake baada ya kuendekeza sana kiki badala ya kuachia muziki mzuri. Kauli ya Weezdom imekuja siku chache baada ya uhusiaano wake Carol Leehevi kuingiwa na ukungu baada ya wawili hao kurushiana maneno makali mtandaoni, jambo lilomfanya mwanamuziki huyo kurudiana na ex wake wa zamani Mylee Stacy.

Read More
 PENZI LA WEEZDOM NA MYLEE STACY LAFUFUKA TENA, WAOMBANA MSAMAHA HADHARANI

PENZI LA WEEZDOM NA MYLEE STACY LAFUFUKA TENA, WAOMBANA MSAMAHA HADHARANI

Aliyekuwa msanii wa nyimbo za Injili nchini Weezdom ameamua kumuomba msamaha mpenzi wake wa zamani Mylee Stacy ikiwa ni siku chache zimepita tangu amporomoshee mvua ya matusi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Weezdom amekiri kumvunjia heshima mpenzi wake wa zamani Mylee Stacy ambaye kwa mujibu wake wamepitia changamoto nyingi kimaisha kwa kusema kwamba anajutia kitendo cha kumdhalilisha hadharini kwenye mitandao ya kijamii. Msanii huyo ametumia fursa hiyo pia kuwaomba msamaha wanawake wote wote ambao amekuwa nao kwenye mahusiano ya kimapenzi na kuahidi kuwa atawapa heshimu kwa mchango wao kwenye safari yake ya maisha . Hata hivyo Ex wake Mylee Stacy alishuka kwenye uwanja wa comment ya post yake na kuachia ujumbe wa kukubali msamaha wake, jambo lilozua mjadala mzito miongoni mwa walimwengu kwenye mitandao ya Kijamii ambao walionekana kushangazwa na hatua ya Weezdom kurudiana na Ex wake Mylee Stacy, wengi wakihoji huenda wawili hao wamekuwa wakipanga matukio ya kuchafuana mtandaoni ili waweze kuzungumziwa kwenye  majukwaa ya burudani nchini. Ikumbukwe kauli ya Weezdom imekuja siku chache baada ya paparazi mmoja kuvujisha mtandaoni video yake akiwa na Mylee Stacy ambapo walionekana wakielekea nyumbani kwa Weezdom.  

Read More
 WEEZDOM AMVUA NGUO EX WAKE MYLEE STACY KWA KUMPOROMOSHEA MATUSI MAZITO

WEEZDOM AMVUA NGUO EX WAKE MYLEE STACY KWA KUMPOROMOSHEA MATUSI MAZITO

Aliyekuwa mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Weezdom ameingia tena kwenye Headline kwenye mitandao ya kijamii baada ya kumporomoshea Matusi Ex wake Mylee Stacy kwa hatua ya kuivuruga ndoa yake. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Weezdom ameonekana kukasirishwa na kitendo cha Ex wake huyo kumtumia jumbe za mapenzi nyakati za usiku akiwa na mke wake ambapo ameenda mbali zaidi na kumtaka Mlyee Stacy akome kumpigia mke wake simu kila mara na badala ya akubali kwamba mahusiano yao yalivunja kitambo. Hata hivyo watumiaji wa mitandao ya kijamii wameonekana kutofurahisha na kitendo cha weezdom kumtolea mambo mazito ex wake Mylee Stacy ambapo wamemshauri wangetatua tofauti zao nje ya mitandao ya kijamii kwani wanajiahibisha wenyewe. Utakumbukwa Weezdom na Mylee Stacy wamekuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa muda ambapo wamekuwa wakiachana na kurudiana lakini uhusiano wao uliingiwa na ukungu mwishoni mwaka wa 2020 baada ya Stacy kudaiwa kutoka kimapenzi na dancer wa FBI aitwaye Ezra madai ambayo  mrembo huyo alikuja akakanusha vikali.

Read More
 WEEZDOM AKANUSHA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA BAHATI

WEEZDOM AKANUSHA MADAI YA KUFUTWA KAZI NA BAHATI

Msanii wa muziki nchini Weezdom amenyosha maelezo kufuatia post aliyoweka kwenye mtandao wa Instagram akisema kwamba Bahati akome kufutilia maisha yake. Akipiga stori na mwana youtube Presenter Ali Weezdom amesema alikasirishwa na kauli ya Bahati kwamba alimfuta kazi kama meneja wake baada ya kuzembea katika majukumu yake. Msanii huyo amekanusha madai yaliyoibuliwa na bahati kwamba alifuta kazi kama meneja wake kwa kusema madai hayo sio ya kweli kwani yeye binafsi ndiye aliamua kuacha kazi kama meneja wake. Amesema ameshangazwa na hatua ya Bahati kukosa shukran kwake licha ya kumsaidia mambo mengi kwenye muziki wake ikiwemo kumuandikia wimbo wa barua uliompa mafanikio makubwa kwenye tasnia ya muziki. Weezdom amesema bahati amemfanya aonekane mbaya kwenye jamii kwa kukodisha watu wamtusi kwenye mitandao ya kijamii ambapo amesema hatotishwa na jaribio hilo la kumzima kwani yeye ni moja kati ya watu ambao huwa hajali jinsi watu wanamchukulia. Hata hivyo amemtaka bahati aache kuwafanyia wasanii wengine mabaya hata kama aliwashika kipindi cha nyuma kwani yeye pia mafanikio ambayo ameyapata yametokana na watu waliomtangulia kumuonyesha njia. Kauli ya Weezdom imekuja mara baada ya Bahati kunukuliwa kwenye moja ya interview akisema kwamba watu waache kumuuliza kuhusu habari za weezdom ambaye alishindwa kutekeleza majukumu ya kusimamia kazi zake wakati alimpa wadhfa wa umeneja.

Read More
 WEEZDOM AMJIBU DIANA MARUA BAADA YA KUDAI UBALOZI WAKE NA LIMAVEST NI BANDIA

WEEZDOM AMJIBU DIANA MARUA BAADA YA KUDAI UBALOZI WAKE NA LIMAVEST NI BANDIA

Msanii wa muziki nchini Weezdom amemtolea uvivu mke wa Bahati, Diana Marua baada ya mrembo huyo kupuzilia mbali ubalozi wake na kampuni ya Limavest. Akipiga stori na mwana youtube presenter Ali, Weezdom amesema kwamba ameshangazwa na kauli ya chuki ambayo diana aliitoa dhidi ya dili alilopewa na kampuni ya Limavest akisisitiza kwamba mrembo huyo ana wivu na mafanikio yake kwani kipindi cha nyuma alinyang’anywa ubalozi wa kampuni hiyo baada ya kukiuka mkataba wa maelewano. Lakini pia ameeleza kwamba Diana ameiponda dili lake la ubalozi kutokana na hatua yake ya kumkingia kifua Willy Paul kwa tuhuma za uongo alizoziibua dhidi ya msanii huyo. Hata hivyo amesema ubalozi wake na kampuni ya Limavest ni halali na sio feki kama jinsi ambavyo Diana Marua amewaaminisha watu kwenye mitandao ya kijamii. Kauli ya Weezdom imekuja mara baada ya Diana Marua kudai kuwa taarifa za Weezdom kulamba dili la ubalozi  wa kampuni ya Limavest ni za uongo kwani msanii huyo anatumia jina la kampuni hiyo kutengeneza kiki ili azungumziwe.

Read More
 WEEZDOM ALAMBA SHAVU LA KUWA BALOZI WA KAMPUNI YA UWEKEZAJI YA LIMAVEST

WEEZDOM ALAMBA SHAVU LA KUWA BALOZI WA KAMPUNI YA UWEKEZAJI YA LIMAVEST

Msanii wa muziki nchini Weezdom amelamba dili nono la kuwa balozi wa kampuni ya uwekezaji ya Limavest. Weezdom ametengaza habari hiyo njema kwa mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa instagram huku akieleza kuwa ana furaha kujiunga na familia ya LimaVest “Najivunia Kukutangazia Kuwa Mimi ndiye Balozi Mpya wa limavest Na tuna Bidhaa mpya yenye bei nafuu Ulizowahi Kufikiria.. Kwa shillingi laki 350 tu…unaweza kushtua kijiji chako kwa kuwapa kitu cha dhamani ambacho kitabadilisha maisha yao na kukutengenezea pesa” aliandika Weezdom kupitia Instagram yake. Weezdom sasa atatakiwa kutangaza bidhaa za  Limavest kwa mashabiki zake kupitia mitandao ya kijamii kwa lengo la kuongezea kampuni hiyo wateja. Limavest ni kampuni ya uwekezaji ambayo huwapa wateja wake fursa sio tu ya kumiliki mali, lakini pia kutumia mali hiyo kuchuma riziki.

Read More
 PENZI LA WEEZDOM NA MYLEE STAICEY LAVUNJIKA RASMI

PENZI LA WEEZDOM NA MYLEE STAICEY LAVUNJIKA RASMI

Msanii Weezdom  hatimaye amethibitisha kuwa yeye na  mpenzi wake wa siku nyingi Mylee Staicey sio wapenzi tena. Katika kikao cha Maswali na Majibu kwenye mtandao wa Instagram, shabiki mmoja alimuuliza msanii huyo kama bado ni wapenzi na  Mylee Staicey na ndipo  alipoweka wazi kuwa waliachana zamani. Kutokana na hilo kama ulikuwa unadhani penzi la weezdom na Stacey lilikuwa limefufuka miezi miwili iliyopita nikuambie tu pole kwani ni wazi kuwa penzi lao limeingiwa na ukungu. Hata  hivyo, bado haijebainika kama kuna ukweli wowote kuhusu stori za wawili hao kuachana ila jambo la kusubiriwa. Itakumbukwa taarifa za wawili hao kuachana zilianza kusambaa mitandaoni mwaka wa 2020 ambapo ilidaiwa kuwa weezdom na mchumba wake stacey wamevunja  penzi lao kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutoaminiana

Read More