Wema Sepetu Aitwa na Bodi ya Filamu Nchini Tanzania Kisa Mavazi

Wema Sepetu Aitwa na Bodi ya Filamu Nchini Tanzania Kisa Mavazi

Bodi ya Filamu Tanzania imemwita rasmi msanii maarufu wa filamu za Bongo, Wema Sepetu, kufika katika ofisi zao kwa ajili ya mahojiano kufuatia kusambaa kwa picha jongevu (video clips) mitandaoni ambazo zinadaiwa kukiuka maadili ya kazi za sanaa nchini. Katika taarifa iliyotolewa na bodi hiyo, imeelezwa kuwa video hizo zinamuonesha Wema akiwa amevaa mavazi yasiyo na staha, jambo ambalo limeibua mjadala mkubwa mitandaoni na kuibua wasiwasi miongoni mwa wadau wa tasnia ya filamu na jamii kwa ujumla. Bodi hiyo imekumbusha wasanii wote Nchini Tanzania kuzingatia maadili, sheria na kanuni za uendeshaji wa kazi za sanaa, hasa katika enzi hizi ambapo maudhui huenea kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii. Wema Sepetu, ambaye ni mmoja wa waigizaji maarufu na wenye ushawishi mkubwa nchini humo, bado hajatoa kauli rasmi kuhusiana na wito huo wa Bodi. Hata hivyo, mashabiki wake wamekuwa wakitoa maoni tofauti, baadhi wakimtetea na wengine wakihitaji afuate misingi ya maadili ya kazi za sanaa.

Read More
 Wema Sepetu Awajibu Wakosoaji wa Mavazi Yake kwa Kauli ya Kejeli

Wema Sepetu Awajibu Wakosoaji wa Mavazi Yake kwa Kauli ya Kejeli

Msanii nyota wa filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu, ametoa kauli yenye kejeli kufuatia wimbi la ukosoaji aliopewa mtandaoni kuhusu mavazi aliyovaa katika hafla ya hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wema ameonekana kuchoshwa na malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa baadhi ya mashabiki na wafuasi wake, akiamua kuwatolea majibu kwa maneno yenye utani mzito. Katika ujumbe huo ulioandikwa kwa mtindo wa kuchekesha lakini wenye ujumbe mzito, Wema alisema: “Next time navaa Baibui kubwa sana na Ninja… Gloves na Socks nyeusi na Miwani… Msijali wapendwa…” Ujumbe huo umetafsiriwa kama majibu ya wazi kwa wale waliomkosoa kwa madai ya kuvaa mavazi yasiyoendana na maadili au mila za Kitanzania, hasa kwenye maeneo ya hadhara. Wema ameonesha dhahiri kuwa hakubaliani na mtazamo huo, na badala yake, ameonesha kuwa atendelea kujiamini na kuwa huru katika uchaguzi wa mavazi yake. Baada ya kauli hiyo, mjadala umeendelea kushika kasi kwenye mitandao ya kijamii huku mashabiki wakigawanyika. Baadhi wameunga mkono msimamo wa Wema, wakisema kuwa ana haki ya kuvaa anavyotaka, ilimradi hafanyi kosa la kisheria. Wengine, hata hivyo, walisisitiza kuwa kama mtu maarufu, anatakiwa kuwa mfano wa kuigwa, hasa kwa vijana wa kike. Sio mara ya kwanza kwa Wema Sepetu kujikuta kwenye vichwa vya habari kutokana na mavazi yake. Mara kadhaa amekuwa akikosolewa vikali, lakini pia amekuwa akipata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wake waaminifu. Wema, ambaye ni mshindi wa taji la Miss Tanzania 2006 na muigizaji aliyeshiriki katika filamu nyingi, amekuwa kwenye macho ya umma kwa zaidi ya muongo mmoja, hali ambayo imekuwa ikimuweka kwenye darubini ya mitazamo mbalimbali ya kijamii.

Read More
 Whozu na Wema Sepetu mbioni kufunga ndoa

Whozu na Wema Sepetu mbioni kufunga ndoa

Mwanamuziki wa Bongofleva Whozu ameashiria kufunga pingu za maisha na mwigizaji Wema Sepetu mwaka 2023. Whozu alidokeza hayo kwa kuacha comment kwenye Instagram kupitia ukurasa wa Sepetu na kumwita mke wake kisha kuweka ishara ya Pete ya ndoa na emoji ya Bibi harusi. Whozu ameandika; “2023 …. Wifey ” ikiwa ni kiashirio kwamba uhusiano wao kuvuka kwenda hatua nyingine kubwa. Wawili hao ambao mahusiano yao kwa mara ya kwanza waliyaweza wazi kwa mashabiki wao kwenye siku ya kumbukizi ya kuzaliwa ya Wema Sepetu, Septemba 28.

Read More
 WEMA SEPETU ANYOSHA MAELEZO KUFANYA MUZIKI WA BONGOFLEVA

WEMA SEPETU ANYOSHA MAELEZO KUFANYA MUZIKI WA BONGOFLEVA

Muigizaji maarufu Bongo Movie, Wema Sepetu ameweka wazi kuwa hana mpango wa kujitosa kwenye muziki. Mrembo huyo, amebainisha kuwa ana uwezo wa kuingiza sauti yake kwenye nyimbo za wasanii wengine. “Mimi huwa napenda kuingiza zile sauti za nyuma, kuimba siwezi, sitaki kujitia aibu, kama wasanii wanapenda sauti zile za nyuma, mimi niko vizuri Hamna wimbo wowote wa Wema unakuja,” amesema. “Sitegemei kuingia kwenye kuimba kwa kweli. Mtanicheka nikianza kuimba, siko tayari,” alisema Wema akiongea na Wanahabari juzi kati. Hata hivyo amefichua kuwa amewahi kuingiza sauti yake kwenye nyimbo kadhaa za aliyekuwa mpenzi wake, Diamond Platnumz, kama Lala Salama na Chanda Chema

Read More
 WEMA SEPETU AKANUSHA KUITISHA MICHANGO YA KUNUNUA GARI

WEMA SEPETU AKANUSHA KUITISHA MICHANGO YA KUNUNUA GARI

Msanii wa filamu nchini Tanzania Wema Sepetu amesema kuwa hajawahi kuwatuma watu kukusanya michango kwa ajili ya kununua gari. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam , Wema amesema aliona jambo hilo na kuwaambia wasitishe kwa sababu hakuridhika nalo na hakumtuma mtu kufanya hivyo. “Mimi binafsi sikuwahi kumwambia mtu yeyote anichangie pesa, nadhani ilikuwa ni upendo na watu wakaamua wafanye hicho wanachofanya lakini nilishawaambia siko comfortable, na wasitishe na nina imani walishitisja,” amesema. “So, sijui nini kilitokea baada ya hapo na sikutaka kujihusisha toka mwanzo kwa sababu sijawahi kumuomba mtu michango ya gari” amesema Wema Sepetu. Utakumbuka jambo hilo lilibuka mara baada ya Mjasiriamali maarufu mtandaoni, Aristote kumshambulia Wema kwa madai hana gari zuri la kifahari kama ilivyo kwa Irene Uwoya, kauli iliyopokelewa kwa hisia kali na wengi hadi Aristote mwenyewe kuomba radhi

Read More