Yammi Atuhumiwa Kumuiba Mume wa Mtu
Msanii wa Bongo Fleva Yammi amejikuta katikati ya mjadala mkali mitandaoni kufuatia madai yanayomhusisha na kuvunjika kwa uhusiano wa rafiki yake, Gachi. Mjadala huo umeibuka baada ya Gachi kuchapisha ujumbe wenye hisia kali kupitia InstaStory yake, akielezea maumivu ya kuumizwa na rafiki wa karibu. Ingawa hakumtaja mtu yeyote moja kwa moja, mashabiki wengi wamehusisha ujumbe huo na Yammi kutokana na tetesi zilizokuwa tayari zikisambaa mitandaoni. Katika ujumbe huo, Gachi ameonesha kusikitishwa na kitendo alichodai kufanyiwa na rafiki yake, akieleza kuwa alimtambulisha kwa mume wake lakini akatumia mapungufu yake kukimbia na mpenzi wake Sakata hilo limekuja mara baada ya Yammi kutrend kwenye mitandao ya kijamii kufuatia kusambaa kwa video inayomuonesha akiwa na mpenzi wake, ambaye inadaiwa alimzawadia kiasi kikubwa cha fedha katika siku ya Wapendanao (Valentine’s Day).
Read More