Yemi Alade Afichua Aliwahi Kudanganya Umri Wake kwa Miaka Mitatu

Yemi Alade Afichua Aliwahi Kudanganya Umri Wake kwa Miaka Mitatu

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria, Yemi Alade, amefichua kuwa aliwahi kudanganya umri wake kwa miaka mitatu, akidai ana miaka 22 ilhali kwa wakati huo alikuwa na miaka 25. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Yemi Alade ameeleza kuwa aliamua kufanya hivyo kutokana na shinikizo la kijamii na tasnia ya muziki, ambayo mara nyingi huwapa nafasi zaidi wasanii wachanga. Kitendo hicho, amesema, kilimfanya apate msongo wa mawazo kutokana na ugumu wa kuishi na uongo huo na kutokukubali ukweli kuhusu umri wake halisi. Msanii huyo wa wimbo waa Johnny amefafanua kuwa uamuzi huo ulisababisha apoteze kujiamini na kukosa amani kwa muda mrefu, kwani kila mara aliishi kwa hofu ya ukweli wake kufichuka. Hata hivyo, amesema ameweza kujifunza umuhimu wa kukubali umri na safari yake binafsi, akisisitiza kuwa huwezi kudanganya muda wala kujificha nyuma ya umri mwingine. Yemi Alade, ambaye amekuwa mmoja wa nyota wakubwa wa muziki wa Afro-pop barani Afrika, sasa anasema anathamini zaidi ukweli na anawahimiza wasanii wengine kuwa wa kweli kuhusu maisha yao binafsi.

Read More