Msanii Ykee Benda mbioni kufanya show yake mwakani
Nyota wa muziki kutoka nchini Uganda Ykee Benda ametangaza tarehe ambayo atafanya show yake ijayo. Kupitia mitandao yake ya kijamii Bosi huyo wa Mpaka Records amesema ana mpango wa kuindaa show yake Mei 13 mwaka 2023 ingawa hajaweka wazi eneo ambalo atafanyia show hiyo. Kwa mwaka huu,Ykee Benda ametoa nyimbo zaidi 8 ambazo zimepokelewa kwa ukubwa na mashabiki zake. Mwimbaji huyo anajiunga na wasanii kama Jose Chameleone, Spice Diana, King Saha na Karole Kasita ambao tayari wametangaza tarehe ambayo watafanya shows zao mwaka 2023. Utakumbuka 2019 Ykee Benda alipata mapokezi mazuri kwenye show yake iitwayo Singa ambayo ilifanyika Serena Hotel, jijini Kampala.
Read More