Zari Hassan Atishia Kuwaanika Wanawake Wanaomtaka Mtoto Wake wa Kiume Kimapenzi

Zari Hassan Atishia Kuwaanika Wanawake Wanaomtaka Mtoto Wake wa Kiume Kimapenzi

Socialite maarufu mwenye asili ya Uganda, Zari Hassan, ameonyesha kuchoshwa na wanawake wanaoendelea kumuandikia mwanawe wa kiume jumbe za mahaba wakionyesha nia ya kumtaka kimapenzi. Kupitia kauli yake mitandaoni, Zari amesema amekuwa akipokea DM nyingi kutoka kwa wanawake wanaojitokeza waziwazi kumtongoza mtoto wake, hali anayosema imevuka mipaka na kumkera. Mwanamama huyo, ameweka wazi kuwa mwanawe tayari yuko kwenye mahusiano na binti wa kizungu, huku akiwataka wanawake hao kuacha tabia ya kumtumia jumbe za kumtamani kimapenzi (thirsty messages). Ameonya wakiendelea na tabia hiyo huenda akachukua maamuziki magumu ya kuwaanika mtandaoni. Kauli ya Zari imezua mijadala mitandaoni, baadhi wakimuunga mkono kwa kulinda faragha ya mwanawe, huku wengine wakiona ni athari ya umaarufu unaoambatana na familia za mastaa.

Read More
 Zari Hassan Aibua Mjadala Kuhusu Mvuto wa Mume Wake Shakib Lutaaya

Zari Hassan Aibua Mjadala Kuhusu Mvuto wa Mume Wake Shakib Lutaaya

Sociliate mwenye asili ya Uganda, Zari Hassan, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kusema kuwa mume wake Shakib huvutia idadi kubwa ya wanawake. Kulingana na Zari, kivutio cha Shakib kwa wanawake hakitokani na mvuto wake binafsi, bali kinachochewa zaidi na hadhi yake kama mume wa mtu maarufu. Mwanamama huyo, ambaye ni mmoja wa socialite wenye ushawishi mkubwa barani Afrika, ameongeza kuwa mara nyingi wanawake humfuata Shakib kwa udadisi, wakitaka kufahamu ni nini hasa alichokiona kwake hadi wakafunga ndoa. Kauli hiyo imezua maoni mseto kutoka kwa mashabiki, baadhi wakisema Zari amekuwa akizungumza kwa ujasiri na kwa mtindo wake wa kawaida wa kuchokoza mjadala, huku wengine wakiona maneno yake kama ishara ya kujiamini na kumthamini mume wake. Shakib na Zari wamekuwa katika uhusiano wa hadharani kwa muda, na mara kadhaa wamekuwa wakionekana wakioneshana mapenzi mtandaoni na kwenye vyombo vya habari. Hata hivyo, uhusiano wao umekuwa ukivutia mjadala kutokana na tofauti zao za umri na maisha yao ya hadhara.

Read More
 Zari Hassan Awaonya Wanawake dhidi ya Kuzaa Bila Uhakika wa Kifedha

Zari Hassan Awaonya Wanawake dhidi ya Kuzaa Bila Uhakika wa Kifedha

Socialite mwenye asili ya Uganda, Zari Hassan, ametoa onyo kali kwa wanawake kuhusu kupata watoto bila maandalizi ya kifedha. Zari anasema katika dunia ya sasa, upendo pekee hauwezi kuendesha familia, akisisitiza kwamba wanawake wanapaswa kuwa na uhuru wa kifedha ili kuishi na kulea watoto bila kutegemea wanaume. Mwanamama huyo wa watoto watano, ameeleza kuwa ni muhimu kwa mwanamke kujijengea msingi imara wa kiuchumi kabla ya kuingia kwenye majukumu ya uzazi, kwani mahusiano yanaweza kubadilika ghafla. Kwa mujibu wa Zari, mahusiano yanayojengwa tu kwa mapenzi au mvuto wa kimwili mara nyingi hayadumu, na mwisho wa siku wanawake wengi huishia kulea watoto wao pekee. Hata hivyo amesema kuwa mwanamke ambaye hana uwezo wa kifedha hana sababu ya kupata mtoto hadi atakapokuwa imara kiuchumi.

Read More
 Zari Hassan Afichua Anavyosumbuliwa na Wanaume Wanaomtaka Kimapenzi Mtandaoni

Zari Hassan Afichua Anavyosumbuliwa na Wanaume Wanaomtaka Kimapenzi Mtandaoni

Mjasiriamali na socialite Zari Hassan amefichua kuwa kisanduku chake cha ujumbe mtandaoni kimefurika na jumbe kutoka kwa wanaume wanaomfuata kwa nia ya kimapenzi. Kupitia mitandao yake ya kijamii, mama huyo wa watoto watano ameonyesha kuchoshwa na wingi wa wanaume wanaomwandikia kwa sababu zisizo sahihi, akisema wengi wao hawana nia ya dhati bali wanatafuta njia ya kumpotezea muda. Zari, ambaye kwa sasa ameolewa na bondia na mbunifu wa mitindo kutoka Uganda Shakib Cham, amebainisha kuwa idadi kubwa ya wanaume hao wanamtafuta kwa tamaa na si kwa uhusiano wa maana. Socialite huyo anayejulikana kwa jina la The Boss Lady amewahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii wa muziki kutoka Tanzania Diamond Platnumz pamoja na marehemu mfanyabiashara Ivan Semwanga, ambaye wana watoto pamoja.

Read More
 Zari Amshauri Mumewe Shakib Aachane na Masumbwi Baada ya Kipigo

Zari Amshauri Mumewe Shakib Aachane na Masumbwi Baada ya Kipigo

Socialite maarufu wa Uganda, Zari Hassan, ameripotiwa kumshauri mumewe Shakib Cham kuachana na mchezo wa masumbwi na kuelekeza nguvu zake katika shughuli nyingine za kibinafsi zinazoweza kumuingizia kipato. Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na wawili hao, Zari amekuwa mstari wa mbele kushauri mumewe kutokana na hali iliyoonekana baada ya pambano la hivi karibuni lililomshirikisha Shakib na msanii Rickman Manrick. Katika pambano hilo, Shakib alipokea makonde mazito ya kichwa yaliyopelekea kuanguka chini na kupoteza fahamu, hali iliyomlazimu muamuzi kusitisha pambano hilo mara moja. Tukio hilo lilimuumiza mno Zari ambaye alishuhudia mumewe akizirai ulingoni na kulia machozi ya uchungu. Chanzo hicho kimeeleza kuwa, licha ya juhudi za Shakib kujaribu kujiweka kwenye tasnia ya masumbwi ya burudani, mchezo huo haujaweza kuleta mapato yaliyotarajiwa na badala yake umekuwa chanzo cha hofu na maumivu kwa familia.

Read More
 Zari Hassan Aangua Kilio Baada ya Shakib Kupigwa Knockout na Rickman

Zari Hassan Aangua Kilio Baada ya Shakib Kupigwa Knockout na Rickman

Mfanyibiashara na sosholaiti maarufu, Zari Hassan, alijikuta akibubujikwa na machozi baada ya mumewe, Shakib Cham, kupigwa knockout vibaya na msanii Rickman Manrick katika pambano la masupastaa lililoshuhudiwa usiku wa Jumamosi, 30 Agosti 2025, ndani ya MTN Arena, Lugogo. Pambano hilo lililokuwa limevuta maelfu ya mashabiki lilimalizika mapema katika raundi ya pili, baada ya Rickman kumshushia Shakib ngumi nzito pande zote za kichwa na kumwangusha chini akipoteza fahamu. Umati ulilipuka kwa shangwe, lakini macho yote yalihamia moja kwa moja kwa Zari, aliyekuwa safu ya mbele, akishuhudia mume wake akizimwa ringini. Awali, Zari alionekana akishangilia kwa nguvu akimhimizia mumewe kupambana, lakini alibadilika ghafla na kuangua kilio mara tu Shakib alipoanguka chini bila msaada. Alimkimbilia ulingoni, akimshika na kumfariji huku akibubujikwa na machozi, jambo lililoacha taswira ya aibu mbele ya umati na kamera zilizokuwa zikirekodi kila tukio. Mitandaoni, mashabiki hawakuchelewa kumrushia vijembe, wakimuita “First Lady wa Knockout”, huku wengine wakisema “hata machozi ya Zari hayawezi kufuta aibu ya kipigo cha Shakib.” Wengine walimkejeli kuwa safari hii si biashara zake wala mitindo yake ya kifahari iliyokuwa gumzo, bali machozi yake ringini. Rickman kwa upande wake aliendeleza rekodi yake ya ushindi, akipata ushindi wa pili katika michezo ya masupastaa baada ya kumbwaga pia msanii Grenade Official mnamo Desemba 2024. Kwa Shakib na Zari, pambano hili limeacha kumbukumbu chungu, knockout kwa ulingo, na machozi kwa jukwaa la mbele.

Read More
 Zari Hassan akatisha mkataba na hoteli moja nchini Uganda kwa kuvujisha picha zake za faraghani

Zari Hassan akatisha mkataba na hoteli moja nchini Uganda kwa kuvujisha picha zake za faraghani

Soshalaiti’ na mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki, Zari Hassan amekatisha mkataba wake na hoteli moja ya kifahari nchini Uganda ambapo alikuwa mapumzikoni na mpenzi wake Shakib Cham. Zari ametangaza kuvunja mkataba wake na Divine Resort & Spa baada ya mpiga picha mmoja wa hoteli hiyo kukiuka kifungu cha mkataba wao kilichosema kwamba picha na video zote zinapaswa kuidhinishwa na Zari kabla ya kuachiwa. “Mpiga picha huyo ameweka picha za Zari kabla ya kuidhinishwa. Kuanzia sasa, Zari hatabanwa tena na mkataba huo na hata-tag Divine Resort AndS pa kwenye chapisho zake zozote za mitandao ya kijamii,” sehemu ya barua ya kusitishwa kwa Mkataba huo imeeleza. Katika barua hiyo, Zari ambaye ni zamani wa staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz alitoa agizo kwa mpiga picha mhusika kufuta picha zake zote alizochapisha kwenye kurasa zake na zile ambazo alituma kwa wanablogu. Pia, aliizuia hoteli hiyo dhidi ya kutumia picha zake na mpenzi wake kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii au tovuti yao. “Kukosa kuzingatia yaliyo hapo juu kutahitaji timu kuendelea na hatua za kisheria na fidia,” barua hiyo ilieleza. Katika video aliyopakia kwenye Snapchat na Insta Story yake, Zari alidai kuwa mpiga picha huyo alivujisha picha hizo kwa sababu alitaka kuwa wa kwanza kutangaza habari za likizo yake na mpenzi wake kwenye blogu yake. Alilalamikia hatua hiyo na kusema kuwa mhusika alikosa weledi katika kazi yake na kukiuka makubaliano kati yake na hoteli. “Baadhi ya picha hizo ni nzuri na zingine kidogo ni PG 13,” alisema Zari.

Read More