Entertainment

YOUNG DEE AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA

YOUNG DEE AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA

Rapa kutoka nchini Tanzania Young Dee ameachia rasmi album yake mpya inayokwenda kwa Nyanguva.

Young D ambaye ni CEO wa Kampuni ya The Dream City, inayojihusisha na usimamizi wa kazi zake,  amesema  album hiyo imebeba jumla ya mikwaju 10 ya moto huku ikiwa na kolabo 5 pekee.

Young D amewashirikisha wasanii mbali mbali kama rapa Rosa Ree, Rapcha, Mrisho Mpoto, Linex na wengine kibao.

Album ya Nyanguva  ni album ya kwanza  kwa mtu mzima Young Dee na inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya  kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile Boomplay

Ikumbukwe album ya Nyanguva ilipaswa kuachiwa rasmi mwezi Julai mwaka huu lakini kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wa Young Dee uongozi wake uliahirisha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *