COUNTRY BOY ADAI LEBO YA KONDE GANG IMEIPA HADHI MUZIKI WAKE

COUNTRY BOY ADAI LEBO YA KONDE GANG IMEIPA HADHI MUZIKI WAKE

Rapper mkali kwa michano kutoka Tanzania country boy amefunguka namna lebo ya muziki ya Konde Gang ilivyobadilisha maisha yake na kuupa hadhi mziki wa Hip Hop nchini tanzania. Kwenye mahojiano yake ya hivi karibuni, rapa huyo amesema kuwa chini ya lebo hiyo imemuongezea thamani kama msanii na hata imepelekea hadhi ya muziki wa hiphop tanzania kupanda kwani mara nyingi wasanii wa Hip-hop huwa wanakosa nafasi ya kujiunga na lebo kubwa. Kwenye lebo ya Konde Gang, Country boy ndiye msanii pekee anayefanya muziki wa Hip-hop na Kabla ya kuingia kwenye lebo hiyo, Rapa huyo alipita kwenye lebo kadhaa za muziki ikiwemo Rooftop Entertainment.

Read More
 KANYE WEST MBIONI KUZINDUA KAMPUNI INAYOJIHUSISHA NA VIFAA VYA KITEKNOLOJIA

KANYE WEST MBIONI KUZINDUA KAMPUNI INAYOJIHUSISHA NA VIFAA VYA KITEKNOLOJIA

Baada ya kukuvalisha viatu na mavazi ya aina yake kupitia chapa ya Yeezy, Kanye West yupo tayari kukuletea vifaa vya kiteknolojia. Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ, Kanye ameripotiwa kulisajili kibiashara jina la ‘DONDA’ mnano Septemba 21 mwaka huu ambapo dhumuni ni kutengeneza vifaa kama Simu, (laptop), Tablets, Headphones na Bluetooth speakers. Akiwa muumini mkubwa wa vifaa vya kampuni ya Apple, sasa Kanye West amedhamiria kuwa mshindani mkuu wa kampuni hiyo kubwa ya vifaa vya kiteknolojia duniani. Kwenye DONDA, Kanye West amepanga pia kutengeneza Saa za mkononi pamoja na miwani za kisasa, vifaa vingine kama earbuds na wireless headset ambavyo vitakuwa sehemu ya bidhaa za DONDA. DONDA ni jina la mama mzazi wa Kanye West ambaye alifariki dunia Novemba mwaka wa 2007 na amelitumia jina hilo kwenye album yake ya 10 ambayo ilitoka Agosti 29 mwaka huu

Read More
 ALI KIBA AWEKA HADHARANI TRACKLIST YA ALBUM YAKE MPYA “ONLY ONE KING”

ALI KIBA AWEKA HADHARANI TRACKLIST YA ALBUM YAKE MPYA “ONLY ONE KING”

Hatimaye orodha ya nyimbo ambazo zinaunda Album ya Mfalme wa muziki wa Bongo Fleva ali kiba iitwayo Only One King imeachiwa rasmi. Album hiyo ina jumla ya nyimbo kumi na sita na kwa sasa unaweza kui-pre order kupitia mtandao wa kusambaza muziki duniani wa Apple Music. Kwenye Album hiyo wasanii mbalimbali kama patoranking, black diamond, sauti sol, nyashinski, khaligraph jones, sarkodie, Mayorkun, tommy flavour, k2ga na abdu kiba ndio watasikika Nyimbo 12 kwenye album hiyo ndio geni haujawahi kuzisikia masikioni mwako na nyimbo 4 tu ndizo ambazo Ali kiba ameshaziachia tayari. Only one king Album kutoka kwa mtu mzima Ali kiba inatoka Oktoba 7, mwaka wa 2021 kwenye mitandao ya kusambaza muziki duniani.

Read More
 GOOGLE YAWEKA UWEZO WA SIMU KUREKODI VIDEO WAKATI WA DHARURA.

GOOGLE YAWEKA UWEZO WA SIMU KUREKODI VIDEO WAKATI WA DHARURA.

Google imeweka uwezo wa simu kurekodi video katika wakati wa dharura kwenye Android 12. Imeweka uwezo wa kurekodi video automatic endapo mtu akibonyeza power button zaidi ya mara 5 au unapokwepo katika hali ya hatari.   Katika sehemu ya Emergency SOS, mtumiaji anaweza kuwasha option ya “Record emergency Video” ambapo endapo ukibonyeza Power Button mara 5 na kuendelea, moja kwa moja simu itakuwa katika SOS Mode, itakuwa inarekodi video huku ikipiga simu ya Emergency Services.   Video za dharura inaweza kuwa na urefu wa dakika 45 na ikubwa wa 10MB kwa dakika moja ili kusaidia storage na kufanya backup. Hii itasaidia mtu akipata matatizo, anaweza kutumia simu yake kurekodi ushahidi kwa Video.   Google imesema ukirekodi video, kama upo unatumia huduma ya internet; video hiyo inakuwa inajisevu ili endapo simu yako ikifa au kuibiwa ile video itabaki katika Cloud Storage yako.    

Read More
 FACEBOOK YAANZA KUWEKA REELS KATIKA APP YAKE

FACEBOOK YAANZA KUWEKA REELS KATIKA APP YAKE

Facebook iliweka videos fupi katika mtandao wa Instagram zilizopewa jina la Reels, mbinu ambayo inasemekana ni kushindana na soko la TikTok na YouTube Shorts kwa sababu imeonekana kuna watu wengi wanapendelea short videos.   Sasa habari njema ni kwamba Facebook imeanza kuweka rasmi Reels katika app yake ya Facebook kwa watumiaji wa Marekani na imesema itaweka katika nchi zote zilizobaki. Watumiaji wa Facebook wataweza kuweka Reels na kushare katika mtandao wa Instagram na Facebook.   Reels za Instagram pia zitaweza kuonekana katika mtandao wa Facebook na mpangilio na muonekano unaonekana kama Instagram Reels na TikTok. Reels za Facebook zitakuwa na Audio, AR Effects, Timer/Countdown/Speeds na sehemu ya Multi Clips ambayo itawezesha watumiaji kumix videos.   Watumiaji wa Facebook wataona tab mpya ya “Reels” katika app ya Facebook na hivi karibuni itaanza kupatikana kwa watumiaji wa nchi zote duni kwani ni update ambayo imeanza rasmi leo.         Facebook iliweka videos fupi katika mtandao wa Instagram zilizopewa jina la Reels, mbinu ambayo inasemekana ni kushindana na soko la TikTok na YouTube Shorts kwa sababu imeonekana kuna watu wengi wanapendelea short videos.   Sasa habari njema ni kwamba Facebook imeanza kuweka rasmi Reels katika app yake ya Facebook kwa watumiaji wa Marekani na imesema itaweka katika nchi zote zilizobaki. Watumiaji wa Facebook wataweza kuweka Reels na kushare katika mtandao wa Instagram na Facebook.   Reels za Instagram pia zitaweza kuonekana katika mtandao wa Facebook na mpangilio na muonekano unaonekana kama Instagram Reels na TikTok. Reels za Facebook zitakuwa na Audio, AR Effects, Timer/Countdown/Speeds na sehemu ya Multi Clips ambayo itawezesha watumiaji kumix videos.   Watumiaji wa Facebook wataona tab mpya ya “Reels” katika app ya Facebook na hivi karibuni itaanza kupatikana kwa watumiaji wa nchi zote duni kwani ni update ambayo imeanza rasmi leo.        

Read More
 MEEK MILL AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA “EXPENSIVE PAIN”

MEEK MILL AACHIA RASMI ALBUM YAKE MPYA “EXPENSIVE PAIN”

Hatimaye Rapa kutoka nchini marekani meek mill Ameikata Kiu Ya Mashabaki Zake Baada Ya Kuiachia Album Yake Mpya inayokwenda kwa jina la EXPENSIVE PAIN Meek Mill Amethibitisha Hilo Kupitia Ukurasa Wake Wa Instagram kwa kuandika ujumbe unaosomeka “My new album Expensive Pain out now ” akimaanisha kwamba album yake mpya sasa inapatikana kwenye digital platform zote. Expensive Pain inakuwa album ya 5 kwa mtu mzima Meek Mill, lakini pia inavunja ukimya wake wa miaka 3 tangu alipoachia yake ya Championships

Read More
 ZULITUMS ATOA CHANGAMOTO KWA WASANII WA UGANDA KUTUMIA KIINGEREZA KWENYE NYIMBO ZAO

ZULITUMS ATOA CHANGAMOTO KWA WASANII WA UGANDA KUTUMIA KIINGEREZA KWENYE NYIMBO ZAO

Mwanamuziki kutoka nchini uganda Zulitums ametoa changamoto kwa wasanii nchini humo kuanza kutumia lugha ya kiingereza kwenye nyimbo zao ili muziki wa uganda uweze kufika mbali zaidi. Zulitums amesema licha ya wasanii wa uganda kutoa muziki mzuri wengi wao wamekuwa wakitumia lugha ya luganda kwenye nyimbo zao jambo analosema limewafanya wasanii kushindwa kutanua wigo wa muziki wao kwenye nchini zingine. Zulitums ni mmoja wa wasanii nchini uganda walioshindwa kuupeleka muziki wao kimataifa hadi pale alipojiunga na lebo ya muziki ya Black Avie iliyoko nchini Nigeria ambayo imebadilisha aina ya muziki wake.

Read More
 RINGTONE APOTEZA MILLIONI 3 ZA KENYA BAADA YA WIMBO WA YESU ANG’ARE KUFUTWA YOUTUBE

RINGTONE APOTEZA MILLIONI 3 ZA KENYA BAADA YA WIMBO WA YESU ANG’ARE KUFUTWA YOUTUBE

Msanii wa nyimbo za injili nchini Ringtone ameumizwa na kitendo cha wimbo wake uitwao Yesu Ang’are aliyomshirikisha Rose Muhando kufutwa kwenye mtandao wa youtube kwa madai ya haki miliki.   Kupitia ukurasa wake wa instagram Ringtone amesema  anakadiria hasara ya shillingi millioni tatu alizotumia kutayarisha audio na video ya wimbo huo jambo ambalo amesema limempelekea kupata na msongo wa mawazo.   Ikumbukwe wimbo wa yesu Ang’are kutoka kwa mtu mzima Ringtone ulifutwa kwenye mtandao wa youtube baada ya ringtone kushindwa kumaliza tofauti zake na lucy ndanu aliyewasilisha lalama kwenye mtandao wa youtube kuwa rose muhando alitumia mashairi ya wimbo wake kwenye wimbo wa ringtone.          

Read More
 “BLACK CHILD ALBUM” YA MR. SEED YAFIKISHA STREAMS 500,000 BOOMPLAY

“BLACK CHILD ALBUM” YA MR. SEED YAFIKISHA STREAMS 500,000 BOOMPLAY

Nyota wa muziki nchini Mr. Seed anazidi kufanya vizuri kupitia mauzo ya mtandaoni na Albamu yake “Black Child” ambayo tayari ina takriban wiki tatu tangu itoke rasmi.   Album ya “Black Child” ambayo ndio albamu ya kwanza ya  Mr. Seed tangu aanze muziki imefanikiwa kufikisha  zaidi ya Streams laki tano kwenye mtandao wa kusikiliza na kupakua muziki wa Boomplay.   Ikumbukwe album ya Black Child kutoka kwa mtu mzima iliachiwa rasmi Septemba 13 mwaka huu wa 2021 ikiwa na jumla ya mikwaju 10 ya moto huku  ikiwa na kolabo 9 pekee.    

Read More