Bradley Ibs Atwaa Tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi Novemba 2025

Bradley Ibs Atwaa Tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi Novemba 2025

Kocha wa Nairobi City Thunder, Bradley Ibs, ametangazwa rasmi kuwa Kocha Bora wa Mwezi Novemba 2025 baada ya kutwaa tuzo ya Betika/SJAK, tuzo inayotolewa kwa kutambua mchango wa makocha waliobobea katika michezo mbalimbali nchini. Bradley alipata heshima hiyo kufuatia mafanikio makubwa aliyopata akiwaongoza mabingwa wa Ligi Kuu ya Mpira wa Kikapu nchini kufuzu kwa Ligi ya Afrika ya Mpira wa Kikapu (BAL) kwa mara ya pili mfululizo. Mafanikio hayo yalipatikana baada ya Nairobi City Thunder kushinda mechi muhimu za kufuzu na kuonyesha kiwango cha juu cha ushindani katika ukanda. Katika mchakato wa kutwaa tuzo hiyo, Bradley aliwashinda makocha kadhaa waliokuwa wamependekezwa kutokana na mafanikio yao katika michezo tofauti. Miongoni mwao ni Kevin Wambua, kocha wa timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba kila upande (Morans), aliyeiongoza timu hiyo kutwaa ubingwa wa mashindano ya Zambezi 7s. Wengine ni David Vijago, kocha wa Kenya Police Bullets, Simon Odongo wa Kenya Lionesses aliyesaidia timu hiyo kumaliza nafasi ya pili katika mashindano ya wanawake ya bara Afrika, pamoja na Caroline Kola aliyeiongoza timu ya taifa ya Deaflympics katika mashindano yaliyofanyika jijini Tokyo. Pia aliyekuwa kwenye orodha ya waliowania tuzo hiyo ni William Muluya, kocha wa timu ya taifa ya vijana Junior Stars, miongoni mwa makocha wengine waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya michezo nchini.

Read More
 Telegram Yaweka Rasmi Mfumo wa Passkey kwa Watumiaji Wote

Telegram Yaweka Rasmi Mfumo wa Passkey kwa Watumiaji Wote

Telegram imeweka rasmi mfumo mpya wa usalama unaojulikana kama Passkey, hatua inayolenga kuimarisha zaidi usalama wa akaunti za watumiaji wake duniani kote. Mfumo huu sasa unapatikana kwa watumiaji wote wa iOS, Android, macOS na Windows. Mfumo wa Passkey unamwezesha mtumiaji kuingia kwenye akaunti yake bila kutumia neno la siri (password) au PIN za kawaida. Badala yake, mtumiaji hutumia key maalum inayohifadhiwa moja kwa moja kwenye simu au kompyuta yake. Key hiyo hufanya kazi kwa kushirikiana na teknolojia za biometric kama vile Face ID, Fingerprint (alama ya kidole) au njia nyingine za uthibitisho wa kifaa. Kwa mujibu wa Telegram, Passkey ni salama zaidi ikilinganishwa na matumizi ya password za kawaida. Hii ni kwa sababu key hiyo haijirudii, haiwezi kutumika kwenye kifaa kingine bila ruhusa, na ni vigumu sana kudukuliwa. Aidha, hata kama mtu atapata password yako ya zamani, hataweza kuingia kwenye akaunti yako bila kutumia biometric zako binafsi. Hatua hii inalenga kupunguza matukio ya udukuzi wa akaunti, wizi wa taarifa binafsi na udanganyifu wa mtandaoni, ambao umekuwa ukiongezeka siku hadi siku. Kwa mfumo wa Passkey, usalama wa mtumiaji unakuwa umefungamana moja kwa moja na kifaa chake pamoja na utambulisho wake wa kibaiometriki. Telegram inaungana na makampuni makubwa ya teknolojia kama WhatsApp, Facebook, Google, Apple ID, Spotify na mengineyo ambayo tayari yameanza kutumia au kuimarisha matumizi ya Passkey kama njia mbadala ya nenosiri la kawaida.

Read More
 Akothee Ataka Jamii Iache Kuingilia na Kukosoa Mtindo Wake wa Mavazi

Akothee Ataka Jamii Iache Kuingilia na Kukosoa Mtindo Wake wa Mavazi

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, amewataka wakosoaji wake kuacha kuingilia mtindo wake wa mavazi na maisha binafsi, akisema lawama nyingi zinazomkabili zinatoka kwa watu wasioishi kulingana na maadili wanayoyahubiri mitandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee ameweka wazi kuwa hataki kuelekezwa jinsi ya kuvaa na watu anaodai wanaficha maovu yao binafsi nyuma ya pazia la maadili ya kijamii. Ameeleza kuwa kuna watu wanaojifanya walinzi wa maadili ilhali familia zao zinakumbwa na matatizo makubwa kama ulevi, usaliti katika ndoa na kuvunjika kwa familia. Msanii huyo amesisitiza kuwa sanaa ni njia ya kujieleza na kwamba jamii inapaswa kujifunza kuheshimu uhuru wa wasanii badala ya kuwahukumu kwa misingi ya mitazamo binafsi. Aidha, amewataka wanaomkosoa waangalie kwanza mienendo yao kabla ya kumshambulia hadharani. Kauli hiyo ya Akothee imekuja baada ya kukosolewa vikali na baadhi ya wanajamii kufuatia kusambaa kwa vipande vya video ya wimbo wake mpya uitwao Society. Video hiyo inaonyesha mavazi yanayobana na kufichua sehemu nyeti za mwili wake.

Read More
 Magix Enga Atambulisha Mpenzi Mpya Baada ya Kuachana na Baby Mama Wake

Magix Enga Atambulisha Mpenzi Mpya Baada ya Kuachana na Baby Mama Wake

Prodyuza na msanii wa muziki nchini Kenya, Magix Enga, amezua gumzo mitandaoni baada ya kutambulisha mpenzi wake mpya wiki chache tu tangu atangaze kuachana na mama wa mtoto wake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Magix ameshare picha akiwa pamoja na mchumba wake na kueleza kuwa ameingia rasmi kwenye ndoa. Haikuishia hapo, alienda mbali zaidi na kumtaja mwanamke huyo kuwa malkia wake wa moyo na chanzo cha furaha kubwa katika maisha yake. Hatua hiyo imewaacha mashabiki wengi wakiwa na maswali iwapo msanii huyo tayari amefunga ndoa au ni namna ya kuonesha hadharani ukubwa wa penzi lake kwa mwanamke huyo. Tukio hilo linajiri wiki chache baada ya Magix kuthibitisha kuachana na baby mama wake, ambapo alisema uamuzi huo ulifikiwa kwa makubaliano ya pande zote bila migogoro. Msanii huyo alibainisha kuwa licha ya kusitisha uhusiano wao wa kimapenzi, ataendelea kushirikiana kwa karibu na mama huyo katika malezi ya mtoto wao, akisisitiza kuwa ustawi wa mtoto unabaki kuwa kipaumbele chake kikuu.

Read More
 Mwijaku Aumizwa na Kitendo cha Ndoa Yake Kuvunjika

Mwijaku Aumizwa na Kitendo cha Ndoa Yake Kuvunjika

Mtangazaji na mdau wa burudani kutoka Tanzania, Mwijaku, amefunguka kwa uchungu baada ya mke wake kukataa kurudiana naye licha ya kuomba msamaha. Kupitia ukurasa wake wa Instastory, Mwijaku ameeleza kuwa kinachomuumiza zaidi ni mazoea ya muda mrefu, kwani wameishi pamoja kwa zaidi ya miaka 15 na sasa ndoto yao ya kifamilia inavunjika kwa kosa moja. Ameonyesha maumivu makubwa kutokana na hali hiyo, akisisitiza kuwa ni vigumu kukubali kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa kuwa wameishi pamoja kwa miaka mingi. Taarifa zinaeleza kuwa mke wa Mwijaku alikataa miito ya kurudiana, akisema hana tena hisia za kimapenzi kwake. Inadaiwa kuwa chanzo cha mgogoro huo ni madai ya usaliti, ambapo Mwijaku alihusishwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwingine, kitendo kilichomkasirisha mke wake na kuamua kuvunja ndoa yao.

Read More
 Huddah Monroe Ashukuru Wakili Aliyemsaidia Kurekebisha Meno Yake

Huddah Monroe Ashukuru Wakili Aliyemsaidia Kurekebisha Meno Yake

Mrembo maarufu katika mitandao ya kijamii, Huddah Monroe, ameonyesha shukrani zake kwa wakili mmoja wa Kenya aliyemsaidia kurejesha tabasamu lake kwa kumsaidia kifedha. Kupitia Instastory, Huddah amefichua kuwa wakili huyo alimpatia shilingi milioni 2, fedha zilizotumika kurekebisha meno yake yaliyokuwa yameharibika baada ya kuhusika kwenye ajali akiwa bado msichana mdogo. Akizungumza kuhusu safari yake ya maisha, Huddah amesema alikulia katika mazingira ya umaskini, hali iliyowafanya wazazi wake kushindwa kumhudumia kwa matibabu ya meno. Upungufu huo ulimfanya kukumbwa na changamoto kubwa shuleni, ambapo wenzake walimchekelea kwa kukosa meno ya juu (front teeth).. Kwa sasa, Huddah anasema msaada huo umempa nguvu mpya na kuondoa majeraha ya kisaikolojia aliyobeba kwa miaka mingi. Amepongeza wakili huyo kwa moyo wa kujitolea na kuonyesha kuwa msaada wa kijamii unaweza kubadilisha maisha ya mtu kwa kiwango kikubwa.

Read More
 Trey Songz Akamatwa kwa Kumpiga Mfanyikazi wa Klabu ya Usiku New York

Trey Songz Akamatwa kwa Kumpiga Mfanyikazi wa Klabu ya Usiku New York

Msanii wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, ameripotiwa kukamatwa na maafisa wa usalama kufuatia tukio la vurugu lililotokea katika klabu moja ya usiku jijini New York City. Kwa mujibu wa taarifa zilizowasilishwa katika mahakama ya jinai ya Manhattan, tukio hilo lilitokea Desemba 4 katika Dramma Night Club, eneo la Times Square. Trey Songz na kundi lake walikuwa wakifurahia burudani hadi pale mfanyakazi wa klabu alipowaarifu kuwa klabu ilikuwa ikifungwa majira ya saa kumi alfajiri. Waendesha mashtaka wanadai kuwa msanii huyo mwenye umri wa miaka 41 na watu wake walionekana kukerwa kupita kiasi bila sababu ya msingi, hali iliyosababisha mvutano. Inadaiwa kuwa Trey Songz alimpiga mfanyakazi huyo ngumi za usoni, tukio lililomsababisha kuvimba na kupata maumivu makali mwilini. Baada ya tukio hilo, Trey Songz alifikishwa mahakamani Jumapili, akikabiliwa na kesi ya shambulio kuhusiana na tukio la klabu hiyo ambapo kesi yake itatajwa tena mwezi Februari 2026. Ikumbukwe, Trey Songz anakabiliwa pia na kosa la uharibifu wa mali (second-degree mischief) linalohusishwa na tukio jingine ambalo maelezo yake bado hayajawekwa wazi.

Read More
 Mulamwah na Carol Sonnie Wazidisha Tetesi za Kurudiana

Mulamwah na Carol Sonnie Wazidisha Tetesi za Kurudiana

Mchekeshaji na mbunifu wa maudhui nchini Kenya, Mulamwah, pamoja na baby mama wake Carol Sonnie, wamezua gumzo mitandaoni baada ya wawili hao kushare picha wakionekana kuwa kwenye date maalum ya kifamilia wakiwa pamoja na mtoto wao. Kupitia picha na video zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Mulamwah na Carol Sonnie walionekana wakifurahia muda pamoja, jambo lililowafanya mashabiki wengi kuanza kuhisi huenda wawili hao wameamua kurejesha uhusiano wao kwa siri. Hata hivyo, wawili hao wamesisitiza kuwa kukutana kwao kulilenga kumpa mtoto wao upendo wa baba na mama, wakieleza kuwa walifanya hivyo kwa maslahi ya mtoto wao na si kwa nia ya kurudiana kimapenzi. Licha ya ufafanuzi huo, mashabiki wameendelea kuhoji ukweli wa kauli hiyo, wakidai ukaribu na mazingira ya date hiyo yanaashiria zaidi ya malezi ya mtoto pekee. Tetesi hizi zimezidi kupata uzito hasa ikizingatiwa kuwa Mulamwah aliachana na baby mama wake mwingine, Ruth K, miezi kadhaa iliyopita.

Read More
 Parroty Vunulu Alalamikia Redio za Kenya Kupendelea Wasanii wa Tanzania

Parroty Vunulu Alalamikia Redio za Kenya Kupendelea Wasanii wa Tanzania

Msanii wa muziki wa Gengetone Parroty Vunulu ameibuka na malalamiko makali dhidi ya baadhi ya vituo vya redio nchini Kenya, akidai vinapendelea wasanii wa Tanzania huku vikisahau kabisa kukuza na kuunga mkono wasanii wa ndani. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Parroty Vunulu amesema redio nyingi za Kenya zimekuwa zikijikita zaidi katika kuzungumzia na kupiga muziki wa wasanii wa nje, hasa kutoka Tanzania, huku zikiongelea matukio na mafanikio yao mara kwa mara kwenye vipindi mbalimbali. Kwa mujibu wake, hali hiyo inawanyima nafasi wasanii wa Kenya ambao pia wanajitahidi kuandaa kazi na matukio yenye mvuto mkubwa. Msanii huyo ameeleza kuwa licha ya wasanii wa ndani kuendelea kutengeneza matukio, kuachia nyimbo mpya na kufanya juhudi za kuinua tasnia ya muziki wa Kenya, watangazaji wengi wamekuwa wakipuuza juhudi hizo kwa kutozizungumzia wala kuzipa nafasi inayostahili hewani. Parroty Vunulu ametoa onyo kali kwa redio hizo akizitaka zibadilishe mwelekeo wao na kuanza kudhamini, kupigia debe na kuzungumzia muziki wa Kenya pamoja na wasanii wake. Ameonya kuwa endapo hali hiyo itaendelea, basi Wakenya wanafaa kufikiria kususia kusikiliza redio ambazo hazithamini na kuunga mkono muziki wa ndani.

Read More
 Yammi Atikisa Mitandao kwa Dokezo la Kolabo na Diamond Platnumz

Yammi Atikisa Mitandao kwa Dokezo la Kolabo na Diamond Platnumz

Msanii wa Bongo Fleva Yammi amezua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kudokeza uwezekano wa kolabo yake na staa wa kimataifa Diamond Platnumz. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Yammi ameposti picha ya pamoja na Diamond Platnumz, hatua iliyochochea hisia na mijadala miongoni mwa mashabiki wao. Kilichozidi kuwasha moto wa gumzo hilo ni ujumbe aliouambatanisha na picha hiyo akiwauliza mashabiki wake endapo angefanya wimbo na kaka yake Diamond Platnumz, wanadhani jina la wimbo huo lingekuwa lipi. Ujumbe huo umewafanya mashabiki wengi kuamini kuwa kolabo hiyo iko njiani, huku wengine wakianza kupendekeza majina mbalimbali ya wimbo huo, wakieleza matumaini yao kuwa kazi hiyo itakuwa kubwa ndani na nje ya Afrika Mashariki. Hata hivyo, hakuna uthibitisho rasmi kutoka kwa Yammi wala Diamond Platnumz kuhusu lini kolabo hiyo itafanyika au kama tayari imerekodiwa. Licha ya hilo, wengi wanaona kuwa endapo wawili hao wataungana, basi muziki wa Bongo Fleva utafaidika pakubwa kutokana na nguvu na ushawishi wao katika tasnia.

Read More
 Ringtone Apoko Awataka Wasanii Wakongwe wa Injili Kenya Kustaafu

Ringtone Apoko Awataka Wasanii Wakongwe wa Injili Kenya Kustaafu

Msanii wa muziki wa injili Ringtone Apoko ameibua mjadala mkubwa baada ya kutoa kauli nzito akiwataka wasanii wakongwe wa injili kuachia nafasi vijana, akidai kuwa wameshindwa kuendeleza na kuupa mwelekeo mpya muziki wa injili, hali iliyosababisha kuporomoka kwa umaarufu wa muziki huo. Akizungumza kupitia mitandao ya kijamii, Ringtone amesema kuwa tasnia ya muziki wa injili kwa sasa inahitaji damu changa ili kuleta ubunifu, mvuto na sauti mpya zitakazowavutia vijana wa kizazi cha sasa. Kwa mujibu wa kauli yake, wasanii wakongwe wamekuwa wakitawala tasnia hiyo kwa muda mrefu bila mabadiliko makubwa, jambo ambalo limefanya muziki wa injili kupoteza mwelekeo na ushindani wake kwenye majukwaa ya kidijitali. Msanii huyo amesisitiza kuwa ukimya wake wa muda mrefu ulikuwa ni ishara ya kutoridhishwa na hali ya muziki wa injili, akidai kuwa kwa sasa muziki huo hauonekani wala kusikika kwa kiwango kinachostahili. Ameongeza kuwa kizazi cha Gen Z kiko tayari kujitokeza, kuanza upya na kutoa nyimbo mpya zitakazoleta uhai na mvuto mpya katika tasnia hiyo.

Read More
 Iyanii Akataa Ofa ya Millioni 3 Kutoka kwa Mwanamke Aliyetaka Kuvunja Ubikra Wake

Iyanii Akataa Ofa ya Millioni 3 Kutoka kwa Mwanamke Aliyetaka Kuvunja Ubikra Wake

Msanii wa muziki nchini Kenya, Iyanii, amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa alikataa ofa nono ya shilingi milioni 3 kutoka kwa mwanamke aliyekuwa akitaka kuvunja ubikra wake. Akizungumza kwenye Mic Check Podcast, Iyanii amesema tukio hilo lilianza mwanamke huyo alipomfuata kwa ofa ya awali ya shilingi laki tano. Hata hivyo, baada ya yeye kukataa, mwanamke huyo aliongeza dau hilo hatua kwa hatua hadi kufikia shilingi milioni 3, akijaribu kumbadilisha msimamo wake. Hitmaker huyo wa Donjo Maber, ameeleza kuwa licha ya kiwango kikubwa cha pesa kilichotolewa, alisimama kidete na kushikilia uamuzi wake wa kuchunga ubikra wake, akisema misingi na maamuzi yake binafsi ni muhimu zaidi kuliko tamaa ya mali. Iyanii pia amekiri kuwa madai yake yamekuwa yakizua mshangao kwa wengi, huku baadhi ya watu wakionyesha kutokuamini. Hata hivyo, amesema yeye binafsi anajijua vyema, akisisitiza kuwa hajawahi kushiriki mapenzi na mwanamke yeyote katika miaka yote 27 ya maisha yake.

Read More