Spice Diana Aachana Rasmi na Meneja Wake
Mwanamuziki nyota wa Uganda Spice Diana ameripotiwa kuachana rasmi na meneja wake wa muda mrefu Roger Lubega wa kampuni ya Source Management, hatua inayofungua ukurasa mpya katika safari yake ya muziki. Chanzo cha karibu na Spice Diana kimethibitisha habari hizo kupitia mitandao ya kijamii, ikisema kuwa uhusiano wake wa kikazi na Source Management umefika kikomo, na sasa mrembo huyo anaanza rasmi maisha mapya ya kujisimamia chini ya lebo yake mpya ya muziki iitwayo “9 Yard.” Wachambuzi wa masuala ya burudani nchini Uganda wanasema hatua ya Spice Diana kuzindua “9 Yard”, inaonyesha nia yake ya kujitegemea na kuchukua udhibiti kamili wa kazi zake za muziki, chapa yake, na biashara zinazohusiana na sanaa. Kwa kipindi cha miaka 10 chini ya usimamizi wa Roger Lubega, Spice Diana alichipuka hadi kuwa mmoja wa wanamuziki wa kike wanaoheshimika zaidi nchini Uganda, akitoa vibao vingi vilivyotamba na kufanya maonyesho makubwa ndani na nje ya nchi.
Read More 
								 
			 
			 
			 
			 
			 
			 
			 
			 
			 
			 
			