Spice Diana Aachana Rasmi na Meneja Wake

Spice Diana Aachana Rasmi na Meneja Wake

Mwanamuziki nyota wa Uganda Spice Diana ameripotiwa kuachana rasmi na meneja wake wa muda mrefu Roger Lubega wa kampuni ya Source Management, hatua inayofungua ukurasa mpya katika safari yake ya muziki. Chanzo cha karibu na Spice Diana kimethibitisha habari hizo kupitia mitandao ya kijamii, ikisema kuwa uhusiano wake wa kikazi na Source Management umefika kikomo, na sasa mrembo huyo anaanza rasmi maisha mapya ya kujisimamia chini ya lebo yake mpya ya muziki iitwayo “9 Yard.” Wachambuzi wa masuala ya burudani nchini Uganda wanasema hatua ya Spice Diana kuzindua “9 Yard”, inaonyesha nia yake ya kujitegemea na kuchukua udhibiti kamili wa kazi zake za muziki, chapa yake, na biashara zinazohusiana na sanaa. Kwa kipindi cha miaka 10 chini ya usimamizi wa Roger Lubega, Spice Diana alichipuka hadi kuwa mmoja wa wanamuziki wa kike wanaoheshimika zaidi nchini Uganda, akitoa vibao vingi vilivyotamba na kufanya maonyesho makubwa ndani na nje ya nchi.

Read More
 Willy Paul: Siwezi Kuwa Kwenye Mahusiano na Mwanamke Mlevi

Willy Paul: Siwezi Kuwa Kwenye Mahusiano na Mwanamke Mlevi

Staa wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ameweka wazi msimamo wake kuhusu mahusiano ya kimapenzi, akisema hawezi kamwe kuwa na uhusiano na mwanamke mlevi. Kupitia ujumbe aliouweka mtandaoni, , Willy Paul amesema kuwa anapendelea kubaki single kuliko kujihusisha kimapenzi na mwanamke anayependa pombe kupita kiasi. Mkali huyo wa ngoma ya Ngunga, amesema wanawake wa aina hiyo mara nyingi hawana nidhamu wala mwelekeo wa maisha, jambo analoliona halifai kwa mtu anayemtafuta mwenza wa kweli. Hata hivyo ameongeza kuwa anaomba Mungu amuepushe na wanawake wenye tabia za ulevi, akisisitiza kuwa heri abaki bila mpenzi kuliko kuwa na mwanamke mlevi.

Read More
 Kenya Kuandaa Mashindano ya Kikapu ya Afrika Kanda ya Tano na Mchujo wa BAL Mwezi Ujao

Kenya Kuandaa Mashindano ya Kikapu ya Afrika Kanda ya Tano na Mchujo wa BAL Mwezi Ujao

Kenya imepata heshima ya kuwa mwenyeji wa mashindano ya kikapu ya Afrika kanda ya tano pamoja na mchujo wa kufuzu kwa ligi ya Basketball Africa League (BAL) kwa wanaume, yatakayofanyika mwezi ujao. Kwa mujibu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Nchini (KBF), mashindano ya wanawake yataanza kuchezwa kuanzia tarehe 9 hadi 15 Novemba katika uwanja wa Nyayo Stadium jijini Nairobi. Michuano hiyo itashirikisha vilabu kutoka Kenya, Rwanda, Tanzania, Burundi na Uganda, huku Kenya ikiwakilishwa na KPA na Zetech University. Baada ya hapo, Kenya pia itakuwa mwenyeji wa mashindano ya mchujo ya BAL yatakayowaleta pamoja mabingwa kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika watakaowania nafasi za kufuzu kwenye ligi ya BAL. Michuano hiyo itafanyika tarehe 18 hadi 23 Novemba katika ukumbi wa michezo wa Kasarani. Nchini Kenya, mashindano hayo yataongozwa na Nairobi City Thunder, mabingwa wa ligi kuu ya taifa, ambao watawakilisha nchi katika kipute hicho. Thunder inalenga kuendeleza mafanikio yake baada ya kufuzu kwa awamu ya timu 12 msimu uliopita bila kupoteza mchezo hata mmoja.

Read More
 KRG The Don Adokeza Kugombea Useneta Nairobi 2027 Kupitia Wimbo Mpya ‘Leo’

KRG The Don Adokeza Kugombea Useneta Nairobi 2027 Kupitia Wimbo Mpya ‘Leo’

Msanii wa muziki wa Kenya, KRG The Don, amedokeza uwezekano wa kuwania kiti cha useneta wa Kaunti ya Nairobi mwaka 2027 kupitia wimbo wake mpya uitwao “Leo.” Katika video ya wimbo huo, mashabiki wamegundua bango linalosomeka “Hon. Stephen Kiruga Kimani – Senator Nairobi County. Vote!” jambo lililotafsiriwa kama ishara ya wazi kwamba msanii huyo ana mipango ya kuingia kwenye ulingo wa siasa. Iwapo ataamua kuingia rasmi katika siasa, KRG The Don ataungana na orodha ya wasanii wa Kenya waliowahi kujaribu bahati yao kwenye uongozi wa kisiasa, akiwemo Jaguar, Bahati, na Prezzo. Ikumbukwe kuwa awali KRG The Don alishawahi kutangaza hadharani nia ya kuingia kwenye siasa, ingawa hakutaja ni wadhifa upi atakaowania wala eneo gani atalisimamia kwenye uchaguzi ujao wa mwaka 2027.

Read More
 Msanii Alien Skin Anusurika Kifo Baada ya Kushambuliwa Jinja

Msanii Alien Skin Anusurika Kifo Baada ya Kushambuliwa Jinja

Msanii mwenye utata kutoka Uganda, Alien Skin, amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na kundi la vijana wakorofi wakati wa ziara yake katika mji wa Jinja siku ya Alhamisi. Mkali huyo wa ngoma ya Sitya Danger alikuwa amesafiri hadi mji huo kwa ajili ya kutumbuiza katika mkutano wa kisiasa wa chama cha NRM, lakini hali ilibadilika ghafla na vurugu kuzuka muda mfupi baada ya onyesho lake kumalizika. Mashuhuda wanasema kuwa baadhi ya vijana waliokuwa kwenye umati waligeuka wenye fujo, jambo lililowalazimu polisi na waandaaji wa hafla hiyo kuingilia kati haraka kumwokoa msanii huyo. Alien Skin aliondolewa kwa dharura na kikosi chake cha usalama hadi sehemu salama. Duru za kuaminika zinasema kuwa huenda tukio hilo lilichochewa na mivutano ya kisiasa, ikizingatiwa kuwa msanii huyo amewahi kutofautiana na wafuasi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) kinachoongozwa na Bobi Wine, ambaye ana ushawishi mkubwa katika eneo hilo. Hii si mara ya kwanza kwa Alien Skin kukumbwa na vurugu katika eneo la mashariki mwa Uganda, mapema mwaka huu aliripotiwa kushambuliwa mjini Iganga baada ya onyesho jingine.

Read More
 Mchekeshaji Terence Creative Aomba Radhi Jamii ya Kisii kwa Matamshi ya Chuki 

Mchekeshaji Terence Creative Aomba Radhi Jamii ya Kisii kwa Matamshi ya Chuki 

Mchekeshaji kutoka Kenya Terence Creative amelazimika kuomba radhi jamii ya Kisii baada ya kutoa matamshi yaliyotafsiriwa kuwa ya chuki na kikabila kupitia ukurasa wake wa Facebook. Terence alizua mjadala mkali mtandaoni baada ya kuchapisha ujumbe unaodaiwa kumlenga aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i, akionekana kufanya utani kuhusu uwezekano wa kiongozi huyo kushinda urais mwaka 2027. Chapisho hilo liliwakasirisha baadhi ya wananchi, hususan kutoka jamii ya Kisii, waliolitafsiri kama kejeli na isiyoonyesha heshima kwa jamii nzima pamoja na viongozi wake. Baada ya wimbi la ukosoaji kuongezeka, mchekeshaji huyo alilazimika kufuta chapisho hilo na kuomba msamaha hadharani kwa jamii ya Kisii, akieleza hakuwa na nia mbaya wala dhamira ya kuudhi jamii ya Kisii. Terrence amesema kuwa ujumbe huo ulikuwa sehemu ya utani wa kawaida, lakini ukachukuliwa vibaya, akisisitiza kwamba anaipenda na kuithamini jamii hiyo pamoja na viongozi wake.

Read More
 Diamond Platnumz Aondoa Video na Machapisho ya Kuunga Mkono Rais Samia

Diamond Platnumz Aondoa Video na Machapisho ya Kuunga Mkono Rais Samia

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, ameondoa video na machapisho yote ya hivi karibuni kwenye mitandao yake ya kijamii yaliyomuonyesha akimuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan na chama tawala cha CCM. Video hizo, ambazo zilikuwa zimeenea sana mtandaoni, zilionyesha Diamond akitumbuiza katika kampeni na ziara za kisiasa za Rais Samia na chama cha CCM, akionesha wazi uungwaji mkono wake kwa serikali na juhudi za rais huyo kutafuta muhula mwingine wa uongozi. Hatua hii imekuja wakati ambapo Tanzania inakabiliwa na mzozo wa kisiasa na maandamano ya kumpinga Rais Samia, yaliyosambaa katika miji kadhaa ikiwemo Dar es Salaam, Arusha, na Mwanza. Maandamano hayo yamechochewa na madai ya kukandamizwa kwa viongozi wa upinzani na kukamatwa kwa wanaharakati. Hadi sasa, Diamond hajatoa kauli rasmi kuhusu hatua yake, lakini wachambuzi wanasema anaweza kuwa anajitenga na lawama kutokana na mvutano wa kisiasa unaoendelea nchini humo.

Read More
 MozzartBet Yadhamini Shirikisho la Mpira wa Wavu kwa KSh 15 Milioni

MozzartBet Yadhamini Shirikisho la Mpira wa Wavu kwa KSh 15 Milioni

Shirikisho la mchezo wa mpira wa wavu nchini Kenya (KVF) limepokea udhamini wa shilingi milioni 15 kutoka kampuni ya michezo ya kubashiri ya MozzartBet, katika hafla fupi iliyofanyika jijini Nairobi. Hafla hiyo ilihudhuriwa na kinara wa Shirikisho la Mpira wa Wavu Barani Afrika (CAVB), Bouchra Hajij, ambaye yuko nchini kwa ziara rasmi ya kikazi. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa udhamini huo, mwenyekiti wa KVF Charles Nyaberi ameishukuru MozzartBet kwa kuendelea kuwa mdau muhimu katika maendeleo ya mpira wa wavu nchini. Amesema kampuni hiyo imekuwa ikitoa mchango mkubwa kwa timu za taifa Malkia Strikers (wanawake) na Wafalme (wanaume) ambazo zimeweka Kenya kwenye ramani ya michezo ya kimataifa. Kwa upande wake, Rais wa CAVB Bouchra Hajij ameipongeza Kenya kwa juhudi zake katika kukuza mchezo wa mpira wa wavu na akatoa mwito kwa mashirikisho ya kitaifa barani Afrika kuwekeza zaidi katika maendeleo ya wachezaji wa ngazi za chini. Udhamini huo wa KSh 15 milioni unatarajiwa kupunguza mzigo wa kifedha kwa KVF na kusaidia maandalizi ya timu za taifa kushiriki kikamilifu kwenye michuano ijayo ya kimataifa, huku ukichangia pia katika kukuza na kuimarisha mchezo wa mpira wa wavu nchini.

Read More
 Bahati Alalamikia Chuki na Wivu Kutoka kwa Wasanii wa Nyimbo za Injili

Bahati Alalamikia Chuki na Wivu Kutoka kwa Wasanii wa Nyimbo za Injili

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Bahati, ameshindwa kuvumilia ukosoaji anaoupata mtandaoni baada ya kuonekana akilia hadharani akielezea machungu anayopitia kutokana na chuki na wivu kutoka kwa baadhi ya wasanii wenzake, hasa wale wa muziki wa Injili. Kupitia video aliyoshiriki kwenye mitandao ya kijamii, Bahati ameonekana mwenye majonzi akisema kwamba kama Mungu angekuwa binadamu, huenda maisha yake yasingekuwa salama kutokana na chuki na husuda za watu. Ameeleza kuwa mara nyingi amekuwa akihukumiwa kwa maamuzi yake ya kisanii na maisha yake binafsi, huku wengi wakisahau kwamba yeye ni binadamu wa kawaida anayekosea kama wengine. Bahati ambaye amepata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki, ameongeza kuwa kila anapojaribu kuinuka, baadhi ya watu wamekuwa wakitamani ashindwe, jambo ambalo limekuwa likimuumiza zaidi akiona baadhi ya wasanii wa Injili wakiendelea kumuombea mabaya badala ya kumtakia heri. Hata hivyo ameahidi kuachia wimbo wake mpya wa kumshukuru Mungu kwa mafanikio aliyoyapata, akisema ni ushuhuda wa jinsi Mungu amemuinua licha ya changamoto na maneno ya watu. Bahati ameeleza kuwa hajawahi kujiona mkamilifu, lakini anaamini baraka zake zinatoka kwa Mungu. Amesema watu wengi hawajui machozi na maumivu aliyopitia ili kufika alipo sasa, na ndiyo sababu ameamua kutumia muziki wake mpya kama sala ya shukrani. Kauli ya Bahati inakuja muda mfupi baada ya kuomba mashabiki zake msamaha kutokana na miendo yake inayokwenda kinyume na maadili ya jamii kwa kujihusisha na maudhui yanayohamasisha ngono.

Read More
 Willy Paul Awakosoa Wasanii Anaodai Kula Pesa za Wamama

Willy Paul Awakosoa Wasanii Anaodai Kula Pesa za Wamama

Msanii nyota wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ametoa kauli tata akijisifia kuwa yeye pekee ndiye msanii ambaye hajawahi kula pesa za wamama, huku akiwakosoa wasanii wenzake kwa kutumia wanawake kama chanzo cha kipato na kiki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul amejipongeza kwa kusema kuwa yeye ndiye msanii pekee ambaye hajawahi kuishi kwa kutegemea wanawake, akiwashauri wasanii wenzake kuacha tabia hiyo na kujitafutia mafanikio kwa kazi zao. Ameongeza kuwa kuna baadhi ya wasanii waliokuwa wakitegemea wanawake matajiri lakini kwa sasa wameachwa na wako kwenye msongo wa mawazo. Katika ujumbe huo huo, Willy Paul amewageukia wasanii wanaovaa mavazi ya kike, akionekana kumtupia dongo Bahati, ambaye hivi karibuni alionekana kwenye video akiwa amevalia chupi ya kike. Mkali huyo wa ngoma ya Ngunga, amesema kwamba tabia kama hizo ni mfano mbaya kwa watoto na jamii kwa ujumla, akisisitiza kuwa wasanii wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa. Kauli ya Willy Paul imetafsiriwa na mashabiki kama dongo kwa Bahati ambaye wiki hii amezua gumzo mtandaoni kutokana vitendo vyake vya kuvalia chupi ya kike na kunywa kinywa alichotumia kuosha miguu ya mke wake Diana Marua

Read More
 Wasanii wa Tanzania Wapata Hasara Kubwa Baada ya Maandamano

Wasanii wa Tanzania Wapata Hasara Kubwa Baada ya Maandamano

Maandamano makubwa yaliyolenga kupinga kile kinachoelezwa kuwa udhalimu wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, yamegeuka kuwa janga kwa baadhi ya wasanii wa Bongofleva, baada ya biashara zao kuripotiwa kushambuliwa, kuvunjwa na kuchomwa moto na waandamanaji wenye hasira. Jijini Dar es Salaam, mgahawa maarufu wa Shishi Food, unaomilikiwa na msanii wa muziki Shilole, umeungua moto vibaya usiku wa kuamkia leo. Tukio hilo linadaiwa kufanywa na kundi la waandamanaji waliokuwa wakilenga biashara na mali zinazohusishwa na mastaa wanaoonekana kuunga mkono kuchaguliwa tena kwa Rais Samia Suluhu Hassan. Shilole, ambaye kwa muda mrefu amekuwa akionyesha uhusiano wa karibu na serikali, amekumbwa na hasara kubwa kutokana na tukio hilo. Mashuhuda wanasema moto ulianza ghafla baada ya kundi la vijana kuvamia mgahawa huo, wakipiga kelele za kuipinga serikali. Hasara hiyo pia imewapata wasanii wengine akiwemo Billnass, ambaye duka lake limechomwa moto, na Jux, ambaye duka lake limevunjwa na kuporwa mali ikiwemo nguo na vifaa vya thamani. Wakati huo huo, Makjuice Sinza, biashara inayomilikiwa na watu wa karibu na tasnia ya burudani, imeripotiwa kuharibiwa na kuporwa.

Read More
 Bahati Aomba Msamaha Hadharani Baada ya Ukosoaji Mkubwa wa Mashabiki

Bahati Aomba Msamaha Hadharani Baada ya Ukosoaji Mkubwa wa Mashabiki

Msanii wa muziki mwenye utata kutoka Kenya, Bahati, amelazimika kuomba msamaha hadharani kufuatia wimbi la ukosoaji alilopokea kutokana na maudhui yake mapya tangu arejee kwenye muziki. Kupitia video aliyoipakia kwenye mitandao ya kijamii, Bahati ameeleza kuwa amepokea simu na jumbe nyingi kutoka kwa marafiki wa karibu, mashabiki, wachungaji, na hata watu wasiowajua, wakionesha kutoridhishwa na mwelekeo wa kazi zake za hivi karibuni. Amesema hakutaka kujibu kwa hasira au hisia kwa kuwa anawaheshimu wote, na badala yake aliamua kuzungumza nao moja kwa moja kutoka moyoni. Bahati amesema kuwa anatambua amewaudhi baadhi ya watu kutokana na mienendo na maudhui ya muziki wake wa sasa, hasa baada ya kurejea na wimbo wake mpya Set It. Ameeleza kuwa lengo lake halikuwa kuwakera, bali kuonyesha ubunifu wake kama msanii anayekua na kubadilika. Msanii huyo ameongeza kuwa anatambua umuhimu wa mashabiki wake, familia, na washirika wake wa karibu, akiwashukuru kwa kumuunga mkono kwa kipindi cha miaka 10 kwenye muziki. Kwa mujibu wake, mafanikio yake yamechangiwa zaidi na upendo na uvumilivu wa mashabiki wake kuliko uwezo binafsi wa uimbaji. Bahati pia ametumia nafasi hiyo kuomba radhi kwa wote aliowakera, akisema yeye ni binadamu anayejifunza kila siku. Amesisitiza kuwa anakubali kurekebishwa lakini pia anahitaji maombi na msaada wa wale wanaomuamini. Aidha, ameahidi kutorudia makosa ya kutayarisha maudhui yanayokwenda kinyume na maadili ya jamii, akisema anajitathmini upya ili kuhakikisha kazi zake za baadaye zinabeba ujumbe chanya na wenye manufaa kwa mashabiki wake. Kauli yake inakuja mara baada ya kuachia wimbo wenye utata uitwao Set It, ambao umeonekana kuhamasisha ngono na kuibua mjadala mkali mitandaoni. Mbali na hilo, Bahati pia alichapisha misururu ya video zinazomuonyesha akiwa amevalia chupi na nyingine akinywa mvinyo alioshea miguu ya mkewe, Diana Marua, jambo lililowakera mashabiki wengi waliomkosoa kwa kupoteza maadili aliyojulikana nayo awali.

Read More