Gossip

OSCAR ADAI BRUNO K ALIKIMBIA NA PESA ZOTE WALIZOPOKEA KUTOKA KWA WAHISANI

OSCAR ADAI BRUNO K ALIKIMBIA NA PESA ZOTE WALIZOPOKEA KUTOKA KWA WAHISANI

Siku chache  zilizopita msanii Bruno K alimtoa mwimbaji wa zamani wa Bigtym, Oscar kutoka kwenye lindi la umaskini.

Hitmaker huyo wa Omulwa alimchuka msanii huyo na akaanza kumpa support, huku akiongoza kampeni ya kufufua kipaji  chake cha muziki ambacho kilikuwa kimefifia.

Sasa  baada ya Oscar kupata afueni ameibuka na kumshutumu vikali Bruno K kwa madai ya kutogawa kwa usawa pesa walizopokea kutoka kwa wasamaria wema.

Msanii huyo amehoji ni kwa nini Bruno K mwanzo alikuwa anajifanya anajali sana ilhali alikuwa na ajenda zake za kujinufaisha kupitia jina lake.

Hata hivyo Oscar ametoa changamoto kwa Bruno k kuonyesha namna pesa walizopokea kutoka kwa waganda na makampuni mbalimbali ilivyotumika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *