Shaniqua Tompkins Amshutumu 50 Cent kwa Unyanyasaji Wakati wa Ujauzito

Shaniqua Tompkins Amshutumu 50 Cent kwa Unyanyasaji Wakati wa Ujauzito

Shaniqua Tompkins, mama wa mtoto wa kwanza wa rapa maarufu 50 Cent, amemshutumu msanii huyo kwa unyanyasaji wa kimwili na kihisia. Akiwa kwenye Instagram Live, Shaniqua alidai kuwa 50 Cent alimshambulia alipokuwa mjamzito wa mtoto wao, Marquise Jackson, akieleza kuwa licha ya ujauzito wake kufikia hatua ya mwisho, bado alikumbwa na vipigo kutoka kwa msanii huyo. Aidha, Shaniqua alidai kuwa rapa huyo pia alimfanyia ukatili Daphne Joy, mama wa mtoto wake wa pili, na kusema tabia hizo za kikatili ndizo zilizomfanya aachane naye. Kwa mujibu wake, 50 Cent amekuwa na mwenendo wa ukatili wa muda mrefu unaowalenga wanawake aliowahi kuwa nao katika mahusiano. Hii si mara ya kwanza kwa 50 Cent kukumbwa na tuhuma kama hizo. Mnamo mwaka 2013, alikabiliwa na mashtaka ya kumshambulia Daphne Joy na kuharibu mali, lakini alikubali makubaliano ya mahakama na kupewa kifungo cha nje pamoja na adhabu ya kufanya kazi za kijamii. Tuhuma hizi zimeibua mjadala mitandaoni, huku wafuasi wa Shaniqua na wanaharakati wa haki za wanawake wakitoa wito wa kuchukuliwa hatua. 50 Cent hajajibu rasmi tuhuma mpya, lakini amewahi kuyakana madai ya aina hii awali akiyaita ya kupotosha.

Read More
 Rapa 50 Cent Azua Gumzo kwa Kauli Kuhusu Maisha Bila Utajiri Mkubwa

Rapa 50 Cent Azua Gumzo kwa Kauli Kuhusu Maisha Bila Utajiri Mkubwa

Rapa na muigizaji nguli kutoka Marekani, Curtis Jackson maarufu kama 50 Cent, amesema kuwa mtu anaweza kuishi maisha ya furaha na heshima hata bila kuwa na utajiri mkubwa. Akizungumza katika podcast ya Brian Roberts, msanii huyo aligusia masuala ya biashara, sanaa, na mbinu mbalimbali za kufanikisha maisha. Kwa mujibu wa 50 Cent, watu wengi hukosea kwa kudhani kuwa mafanikio ya kweli hupimwa kwa kiwango cha pesa walicho nacho. Alieleza kuwa kuna watu wanaoishi maisha yenye thamani na utulivu mkubwa hata bila kuwa na fedha nyingi, kutokana na uwezo wao wa kujiendesha kimaadili, kifikra na kwa mitazamo chanya ya maisha. Katika mazungumzo hayo, msanii huyo pia alisisitiza umuhimu wa ushindani kwenye kila juhudi anazofanya mtu. Alibainisha kuwa ushindani ni kichocheo cha maendeleo, kwani humpa mtu sababu ya kujituma zaidi, kuwa mbunifu, na kutafuta njia bora za kuboresha kile anachokifanya. 50 Cent, ambaye pia ni mjasiriamali aliyewekeza katika sekta mbalimbali kama vile burudani, vinywaji, na utayarishaji wa vipindi vya televisheni, ameendelea kuwa mfano wa mafanikio yanayotokana na nidhamu ya kazi, maamuzi sahihi na uthubutu. Kauli zake zimeibua mjadala mitandaoni, wengi wakitafakari nafasi ya pesa katika ubora wa maisha, huku wengine wakikubaliana na msimamo wake kuwa mafanikio si lazima yahusishe utajiri mkubwa bali kujitambua, kushindana kwa njia ya haki, na kuishi kwa misingi ya maadili.

Read More
 50 Cent Apinga Uwezekano wa Trump Kumsamehe Diddy

50 Cent Apinga Uwezekano wa Trump Kumsamehe Diddy

Rapa maarufu 50 Cent amejitokeza waziwazi kupinga kauli ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kuhusu uwezekano wa kumsamehe Sean “Diddy” Combs, ambaye anakabiliwa na mashtaka mazito ya usafirishaji wa binadamu kwa ajili ya ngono na uhalifu wa kupanga. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, 50 Cent alionyesha kutoridhishwa na kauli ya Trump, akieleza kuwa Diddy amekuwa akiongea vibaya kuhusu Trump kwa muda mrefu, na hivyo si sahihi kwa kiongozi huyo wa zamani kufikiria kumsamehe mtu ambaye hakumuunga mkono.  “Alisema mambo mabaya sana kuhusu Trump, sio sawa. Nitawasiliana naye ili ajue jinsi ninavyohisi kuhusu mtu huyu.”  aliandika Instagram Kauli hii ya 50 Cent inakuja baada ya Trump kusema katika mkutano na waandishi wa habari kwamba hajapokea ombi rasmi la msamaha kwa Diddy, lakini yuko tayari kuangalia ukweli wa kesi hiyo kabla ya kufanya uamuzi wowote. Diddy anakabiliwa na mashtaka mazito ya usafirishaji wa binadamu kwa ajili ya ngono, njama ya uhalifu, na usafirishaji kwa ajili ya ukahaba.  Iwapo atapatikana na hatia, anaweza kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani. Uhusiano kati ya 50 Cent na Diddy umekuwa na mvutano kwa muda mrefu, na 50 Cent amekuwa akitoa maoni ya ukosoaji dhidi ya Diddy mara kwa mara.  Kauli yake ya sasa inaonyesha nia ya kuzuia msamaha wowote kutoka kwa Trump kwa Diddy.

Read More
 Eminem ana mchango mkubwa kwenye muziki wa Hiphop – 50 Cent

Eminem ana mchango mkubwa kwenye muziki wa Hiphop – 50 Cent

Rapa 50 Cent hakubaliani na hoja isemayo kwamba Jay-Z ana mchango mkubwa kwenye muziki wa Hip Hop kuliko Eminem. 50 Cent ameipinga hoja hiyo ambayo imesemwa na nyota wa zamani wa NBA, Jamal Crawford kwenye podcast ya Shaquille O’Neal, 50 Cent alishuka kwenye comment na kusema ni upuuzi mtupu. Sio mara ya kwanza kwa 50 Cent kumkingia kifua Eminem hasa pale inapokuja mijadala mizito ya muziki wa Hiphop, itakumbukwa Oktoba 2022 kwenye mahojiano na Ebro in The Morning, 50 Cent alisema “Rap God” Eminem hapewi heshima ambayo anastahili.

Read More
 Rapa 50 Cent adokeza ujio wa ngoma mpya na mtayarishaji nguli Dr. Dre

Rapa 50 Cent adokeza ujio wa ngoma mpya na mtayarishaji nguli Dr. Dre

Baada ya hivi karibuni kudokeza kuwa anafanyia kazi ujio mpya wa kazi zake za muziki kwa mwaka 2023, Rapa 50 Cent ametusanua kuhusu ujio wa ngoma mpya na mtayarishaji nguli Dr. Dre. Kwenye mahojiano na mtangazaji Big Boy, 50 Cent amekaririwa hapo akisema tutarajie ushirikiano wao tena kwa mara nyingine kwani baada ya kutangaza kurudi kwenye muziki alipokea ujumbe mfupi kutoka kwa Eminem ambao ulisema, Dr. Dre ana midundo kwa ajili yake. Ujio wa 50 Cent kwenye dunia ya muziki miaka 20 iliyopita ilifanikishwa na kazi kubwa ya Mtayarishaji Dr. Dre ambaye alipika midundo mizito iliyoweza kunata vyema kwenye mistari ya Rapa huyo ambaye alishikwa mkono na Eminem.

Read More
 50 Cent atangaza kuachia nyimbo mpya mwaka 2023

50 Cent atangaza kuachia nyimbo mpya mwaka 2023

Mkongwe wa muziki wa Hiphop ambaye pia ni muigizaji na muandaaji wa filamu kutoka Marekani, 50 Cent, ameeleza mwaka huu anaachia ngoma mpya, series mpya pamoja na filamu mpya. 50 Cent ambaye jina lake halisi ni Curtis James Jackson ameandaa series na filamu kama, Director, Power, Den of Thieves, Before I Self Destruct, na The Frozen Gro. “Nawakumbusha tu watu kwamba mwaka huu nipo vizuri, ngoma mpya, series mpya na movie mpya”, Aliandika. 50 Cent ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram wakati akimsifia rapa Eminem juu ya taarifa ya kwamba ndiye rapa ambaye ametazamwa zaidi kwenye mtandao wa Youtube kwa mwaka 2022, akifikisha jumla ya views Bilioni 5.

Read More
 50 Cent mbioni kuja na filamu kuhusubmaisha ya tapeli maarufu wa Nigeria, Hushpuppi

50 Cent mbioni kuja na filamu kuhusubmaisha ya tapeli maarufu wa Nigeria, Hushpuppi

Rapa, muigizaji na muandaaji wa show za Tv na filamu kutoka Marekani, Curtis James Jackson III maarufu kama 50 Cent, ametangaza mpango wake kwa mashabiki kwamba anaandaa series itakayohusu maisha ya Ramon Abbas maarufu Hushpuppi ambaye ni raia wa Nigeria aliyejipatia umaarufu mkubwa duniani kwa utapeli mitandaoni. 50 Cent ambaye ameshatayarisha series kama Power, Power Book II, Power Book III: Raising Kanan ameeleza kupitia ukurasa wake wa Instagram kuhusu ujio wa series ya Hushpuppi na kusema ni hivi karibuni. “Kwa walaghai wangu nilipaswa kufanya hivi, tamthilia kumuhusu Hushpuppy inakuja hivi karibuni” – Unasomeka ujumbe wa 50 Cent kupitia ukurasa wake wa Instagram. Hushpuppi ambaye wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miaka 11 gerezani, hata hivyo kulingana na tayari alishakaa jela Marekani kwa takribani miaka 2 tangu mwezi Juni mwaka 2020 baada ya kukamatwa huko Dubai na kisha kuhamishiwa Marekani, hivyo kwasasa ameanza kukitumikia kifungo chake cha miaka 9 tu gerezani.

Read More
 50 cent adai Eminem hapewi heshima anayostahili

50 cent adai Eminem hapewi heshima anayostahili

Rapa mkongwe kutoka nchini Marekani 50 Cent amesema rapa Eminem hapewi heshima ya kutosha. Kwenye mahojiano yake na ‘Ebro In The Morning’ wakati akiitangaza series yake mpya (Hip Hop Homicides), 50 Cent amesema kwa mchango ambao Eminem ameuweka kwenye huu muziki wa Hiphop, anafikiri anastahili heshima zaidi ya ambayo anapewa kwa sasa. Ikumbukwe ‘Eminem’ ndiye rapa mwenye rekodi nyingi za mauzo yaani Most Certified Artist katika historia ya muziki nchini Marekani, mpaka sasa ana jumla ya certificate Million 73.5 kwa upande wa Gold & Platinums. Eminem anashikilia rekodi ya msanii aliyeuza singo nyingi zaidi katika kiwango cha (Gold) na (Platinum) yaani mauzo kuanzia nakala laki tano hadi milioni moja, akishika namba moja katika historia ya RIAA Awards.

Read More
 Kendrick Lamar ashinda Tuzo ya Msanii Bora wa  Hiphop kwenye BET Hip-Hop Awards 2022

Kendrick Lamar ashinda Tuzo ya Msanii Bora wa Hiphop kwenye BET Hip-Hop Awards 2022

Rapa Kendrick Lamar ameibuka mshindi wa kipengele cha Hip-Hop Artist Of The Year kwenye Tuzo za BET Hip-Hop 2022 ambazo zinatolewa usiku wa kuamki leo nchini Marekani. Kendrick Lamar pia ameondoka na ushindi kwenye vipengele vya Lyricist Of The Year, Best Hip Hop Video “Family Ties”, Best Live Performer na Hip Hop Album Of The Year (Mr. Morale & The Big Steppers) Kwa upande mwingine Rapa 50 Cent ameibuka mshindi wa Tuzo ya ‘Hustler Of The Year’ akiwaangusha DJ Khaled, Drake, Cardi B, Jay-Z, Kanye West na Megan Thee Stallion. Kolabo ya Future, Tems na Drake “Wait For You” imeshinda Tuzo ya Best Collaboration kwenye Tuzo za BET Hip Hop 2022.

Read More
 50 CENT ATOA YA MOYONI KUHUSU WASANII WALIOKUWA WANAUNDA KUNDI LA G-UNIT

50 CENT ATOA YA MOYONI KUHUSU WASANII WALIOKUWA WANAUNDA KUNDI LA G-UNIT

Rapa mkongwe kutoka Marekani 50 Cent amedai kwamba bado waliokuwa wasanii wa kundi la G-Unit wanamtupia lawama kwa kushindwa kwao kufanikiwa katika muziki. Kwenye mahojiano yake na 97.9 The Box, 50 Cent ambaye alikuwa kichwa cha kundi hilo (Label) amezungumza na kusema siku zote watu au wasanii humtupia lawama kiongozi na sio taasisi au kampuni waliopo. “Kuna ambao huwa wananiomba radhi kwa maneno yao. Lakini unajua kidonda kipo sehemu moja, unapokuwa kwenye nafasi ya kuendesha gari, kiti cha dereva, mara nyingi pale mambo yakiwa hayaendi sawa sio kosa lako. Ukiwauliza wasanii kwanini walishindwa kufanikiwa, siku zote wataitupia lawama Record Label” alisema 50 Cent na kuendelea “Hivyo mimi binafsi nilipata kuwa Record Label, hivyo wasanii wote ambao walikuwepo na mambo yao hayakwenda vile walivyotarajia, ni makosa yangu kwamba sikufanikisha mambo yao. Wananitupia lawama Mimi binafsi na sio kampuni tena.” alimaliza 50 Cent. Chini ya uongozi wa 50 Cent, Kundi la G-Unit lilikuwa na wasanii kama Lloyd Banks, Young Buck, Tony Yayo, The Game na DJ Whoo Kid.

Read More
 50 CENT AMTOLEA UVIVU JAY Z KWA MADAI YA KUTOMTAKA KWENYE SUPER BOWL HALF TIME SHOW

50 CENT AMTOLEA UVIVU JAY Z KWA MADAI YA KUTOMTAKA KWENYE SUPER BOWL HALF TIME SHOW

Rapa kutoka Marekani Jay-Z hakutaka 50 Cent atumbuize kwenye Halftime show ya Super Bowl 2022, ilimbidi Eminem atie mgomo kwa kusema hatofanya show kama Jay-Z hatomruhusu 50 Cent awe kwenye orodha ya watumbuizaji kwenye fainali hizo. Siri hii imevujishwa na Mtangazaji N.O.R.E kwenye podcast ya Drink Champs wakati akifanya mahojiano na Snoop Dogg. Kauli hiyo ilimuibua 50 Cent jana kwenye akaunti zake za mitandao ya Kijamii ambapo alimshutumu vikali Jay-Z kwa kuiga mtindo wa nywele wa mchoraji maarufu duniani Jean-Michel Basquiat huku akimkejeli kwa kumuita shoga. “Kwa nini alilazimika kusema hilo liwe swali? NORE Mke wako mkubwa anakimbia huku na huko akijaribu kuonekana kama mchoraji shoga,” 50 Cent alifoka. 50 hakuishia hapo. Rapper huyo alipinga madai ya Noreaga kwamba Jay-Z alimwita Eminem “mzungu.” Kwa kusema kwamba “Kwanini alisema yule kijana wa kizungu, kwanini hangesema msanii mkubwa wa rap duniani? Pasaka njema ! mtu kufurahia likizo. @bransoncognac @lecheminduroi,” 50 Cent alihitimisha kupitia Instagram yake.

Read More
 RAPPER 50 CENT ATISHIA KUACHANA NA KAMPUNI YA STARZ

RAPPER 50 CENT ATISHIA KUACHANA NA KAMPUNI YA STARZ

Rapper kutoka Marekani 50 Cent ameingia kwenye headline mara baada ya kutishia kuondoka Starz, kampuni ambayo imechangia mafanikio makubwa ya series yake iitwayo ‘Power’. 50 Cent alisaini mkataba wa miaka minne na Starz tangu mwaka wa 2018 kwa kiasi cha shilling billion 17 za Kenya wa kufanya kazi ya kutengeneza series mbalimbali. Hata hivyo 50 cent hajaweka wazi chanzo cha kutaka kuachana na kampuni hiyo Mkongwe huyo wa rap ambaye jina lake halisi ni Curtis James Jackson III, kupitia ukurasa wake wa Instagram amewataka wafanyakazi wake chini ya kampuni yake ya G-Unit Film & Television kuanza kufungasha vitu vyao na kuondoka.

Read More